Tarehe: 9:56:00 PM, Mtoa Maoni:- boniphace
Tarehe: 3:08:00 AM, Mtoa Maoni:- Indya Nkya
Tarehe: 7:10:00 AM, Mtoa Maoni:- mwandani
Hao wanaokopiana chuo kikuu mie nikipata kufundisha pale nitakuwa mnoko sana. Nitawapa misahafu mirefu mirefu kwa maksi chache mpaka wataelewa... Haya twende kwenye hoja:
Ndugu mnaokaa ughaibuni, hivi katika tazama tazama zenu mnawaona watu wengi wa kawaida huko majuu wanaopenda kujisomea masuala mazito mazito? Au ni wasoma hadithi za upelelezi kama za Wili Gamba?
Wanaweza kukumbuka na kujua mambo yao, pamoja na sababu nyingine, kutokana na vipindi vyao vya televisheni na vyombo vyao vya habari. - masomo ya shule za msingi yanaonyeshwa kwa undani kila asubuhi, jioni vipindi vya ushujaa wa mashujaa wao vimejaa -Wamarekani weusi kuijua Timbuktu mpaka wakanunue vitabu - ukiangalia sanaa zao hao wabaguzi...nazo ni mambo hayo hayo, huko marekani kila mtu anajua habari ya first and fifth amendment... sijui kama wamesoma katiba yao...
Pengine hatupendi kujisomea,sitabisha sana, lakini wanaoendesha maendeleo ya huko ni wasomi na wafanyabiashara wabunifu kadhaa.Sio watu wowote tu. Wanasayansi walioko hapo NASA kuna wachina, wahindi, na waafrika, manesi waafrika ndio wamejaa kwenye mahospitali, wote wamesoma vitabu... na huko kwenye bonde la Silikoni kwenye makompyuta ndipo wageni walipojazana.
Wasomi, mkijumuishwa na wanablogu wote wa kiafrika ughaibuni... nyote nyie mnapenda kujisomea.
Huyo mwandishi mmbaguzi anatupiga madongo kinamna...
Anataka tuamini matusi anayotukana, na tukiamini tu tumekwishaa!
Tumeshaamini mengi waliyosema na ndio maana tunakwisha...
Haidhuru, nalotaka kusema ni kuwa ugonjwa mkubwa sio kutopenda kujisomea tu bali pia ni ugonjwa wa "kuamini kuwa tumeshindwa - au hatuwezi" haswa jambo analotaka kutufanyia huyo mwandishi.
Tarehe: 8:55:00 AM, Mtoa Maoni:- Egidio Ndabagoye
Hii inasikitisha sana.Kweli hatuna utamaduni wa kujisome vitabu.Padre Karugendo alisema kuwa ..."ukienda katika maduka ya vitabu utakuta vitabu vimejaa vuumbi..." havinunuliwi.Ukitaka kuutafuta umaskini basi jaribu biashara ya kuuza vitabu.Ndio maana watanzania tulio wengi hatuna uwezo wa kupambanua hoja.
Makene,hili sula la vyuo vikuu kama alivyosema Indya ni nyeti mimi niko huku naona... ni kitu cha kawaidaa sana kunakiliana kazi walizotupa wahadhiri.Kila siku hili jambo linanikera sana kusomea mitihani! na kusoma yale tu yanayofundishwa darasani na hii ya kusoma magazeti ya 'udaku'? Hapo nitapigwa
Jeff tazama mfano mdogo tu wa maandishi haya unayoandika, je wadhani hadhira yako ni ipi kama si ile ile siku zote na inaweza kuwa inapungua? Huu ni ugonjwa mkubwa, plae Chuo Kikuu Mlimani siku hizi kuna tabia ya wanafunzin kukopiana maandishi na utakuta wanakopiana neno kwa neo wanafunzi zaidi ya 20 lakini bado profesa anatoa maksi zinazotofautiana! Usaliti huo wa moyo...yafanye haya huku kama chuo hakijaota mbawa?
Nifunge domo langu kwanza ili wajitokeze wengine na yao!