Friday, December 02, 2005
MAREKANI NA HUKUMU YA KIFO!
Hukumu ya kifo nchini Marekani imechukua mtu wa 1000 tangu ianzishwe mwaka 1976. Suala la hukumu ya kifo ambayo serikali yetu ya Tanzania bado inalikumbatia( sina takwimu za watu walionyongwa kutokana na hukumu ya kifo) bado linazua mijadala mikali miongoni mwa wanasheria,wanaharakati wa haki za binadamu duniani.Canada haina hukumu ya kifo. Marekani pamoja na kuwa mtekelezaji mkubwa wa hukumu hiyo(sio katika majimbo yake yote) bado inaendelea kuwa miongoni mwa mataifa yanayoongoza duniani kwa vifo vinavyotokana na kuuawa iwe kwa mtutu wa bunduki ama vinginevyo. Suala gumu katika masuala haya ya hukumu ya kifo ni je kwa mfano huyo tunayemhukumu kifo hakuua,nini hatma yetu? Tunaweza kujadili.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 3:07 PM
|
Permalink |
-
Inasikitisha sana kuona mtu anashupalia kumuua mwenzake. anajifanyz hasikii anavyolia kuomba huruma.
Leo ansema ametubu kaso lake na amejirekebisha kesho anmchoma sindano ya sumu, nimesikia wengi waliofanywa hivyo lakini siku niliyosikitika sana ilikuwa siku walipomuua carla dana faye, mwanamke aliyeua, akajirekebisha gerezani, gereza likampenda kwa sababu alikuwa na faida sana gerezani, aliwasaidia sana magereza kuwaelimisha wafungwa wengine, lakini siku uaua aliposikia hamu ya kuua alianza naye kutimiza hamu yake!
Nia yao ni kuua tu sio kubadili tabia za watu, bora waseme watawaua mara tu adhabu itolewapo, bila kuwaweka miaka takribani kumi wakivuta njaa zao za kuua.
Inasikitisha sana kuona mtu anashupalia kumuua mwenzake. anajifanyz hasikii anavyolia kuomba huruma.
Leo ansema ametubu kaso lake na amejirekebisha kesho anmchoma sindano ya sumu, nimesikia wengi waliofanywa hivyo lakini siku niliyosikitika sana ilikuwa siku walipomuua carla dana faye, mwanamke aliyeua, akajirekebisha gerezani, gereza likampenda kwa sababu alikuwa na faida sana gerezani, aliwasaidia sana magereza kuwaelimisha wafungwa wengine, lakini siku uaua aliposikia hamu ya kuua alianza naye kutimiza hamu yake!
Nia yao ni kuua tu sio kubadili tabia za watu, bora waseme watawaua mara tu adhabu itolewapo, bila kuwaweka miaka takribani kumi wakivuta njaa zao za kuua.