Tarehe: 11:40:00 AM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 4:49:00 AM, Mtoa Maoni:- Egidio Ndabagoye
Nakubaliana na Ndesanjo kuwa hii i tovuti ni ya wapenzi wa Kikwete.Kulikuwa na malumbano katika gazeti fulani la kila wiki kuhusu ni hipi tovuti ya Kikwete(kutolea maoni ya wananchi).Sasa mmoja wa watu aliitoa Tovuti hii.Nami nikaipandisha mtandaoni.Mimi Nimeshagundua kuna mkono wa mshikaji mmoja katika tovuti ile
Tarehe: 2:43:00 AM, Mtoa Maoni:- Rama Msangi
Wakati nilipokuwa huko Makao makuu ya kwenye risala na makabrasha, kipindi wana-CCM wanachukua fomu za kumpata atakayechukua nafasi ambayo kwa sasa anayo JK, nakumbuka kilichotokea siku yeye JK alipokuwa anachukua fomu. Kuwa tofauti na hali ilivyokuwa kwa wagombea wengine katika kuulizwa maswali, huyu yeye aliulizwa maswali ambayo kwa mtu yeyote mwenye kujua maana ya ushabiki, upenzi na umamluki, angeligundua kuwa kulikuwa na kitu fulani ndani yake.
JK ni mtu ambaye hutumia kikamilifu kila fursa anayoipata (Opportunist nyie huko Ulaya mnawaita) na ndio maana haikunishangaza sana pale niliposikia kuwa siku hiyo alipandikiza watu wake kwa ajili ya kumuuliza maswali fulani kwakuwa alikuwa na yake ambayo katika mazingira ya kawaida asingeliweza tu kusimama hadharani na kuanza kuyatoa.Hili nalo bilashaka ni moja ya hizo hizo fursa ambazo anataka kuzitumia kwa lengo lake fulani ambalo huenda mimi na wewe hatulijui.
Kuna mambo mengi ambayo mtu unaweza kujiuliza kuhusu hili jambo, lakini naomba tu niulize moja kati ya maswali mengi: KERO YA RUSHWA IKO WAZI KWA KILA KIONGOZI, JK ALITAMKA HADHARANI KUWA ANA MAJINA YA WALARUSHWA, LAKINI AKASEMA ANAWAPA TENA MUDA WA KUJIREKEBISHA, KUNA UMUHIMU GANI WA MAONI AU KERO ZA WANANCHI IKIWA TUNAKWAMBIA TUNAUNGUA UNASEMA KUWENI NA SUBIRA MOTO HUENDA UKAPUNGUA WENYEWE?
Ninavyofahamu Jeff ni kuwa hii tovuti sio ya serikali bali wapenzi wa Kikwete. Kuna majaribio yanayofanywa na serikali nyingi kujenga uhusiano wa karibu kati ya wananchi na viongozi kwa kutumia teknolojia za serikalipepe (egovernment). Nadhani kama Kikwete anataka kufanya hivyo au mtu yeyote anataka kufanya hivyo ni vyema akajua kuwa kuna mifano mingi ya kujifunza toka katika nchi mbalimbali na taasisi mbalimbali za kitafiti. Serikalipepe ni jambo ambalo, ingawa litachukua muda kuiva, lina nafasi yake fulani katika miaka ijayo.