Wednesday, August 08, 2007
UMEYASIKIA YA "PILAU"?
Leo katika pitia pitia yangu ya magazeti ya Tanzania,nilikumbana na habari hii ya mbunge aliyekuwa anaweka wazi kuhusu "slang" ya mtaani iitwayo pilau au biriani kumaanisha picha za ngono zilizo katika mifumo mbalimbali kama vile picha za video,dvd,cds nk. Kwa mujibu wa mbunge huyo,jiji la Dar-es-salaam ndio linaongoza kwa kuwa na pilau aka biriani katika mitaa yake.
Lakini hili hakukuniumiza kichwa kwani tangu enzi na enzi picha hizi zimekuwepo.Uongo? Kilichoniwazisha kidogo ni kwamba hivi picha za ngono ndio zinaambukiza ukimwi au ni watu ndio wanaambukizana ukimwi? Hivi tukipiga vita picha za ngono,wakati vipindi vya televisheni vile tunavyoangalia na watoto wetu au tunaowaachia watoto waangalie,hata zile ambazo zimeandikwa kabisa kwamba watoto wenye umri usiopungua miaka fulani wasiangalie,kuna tofauti yoyote?Mbunge huyu anaongelea ngono za aina gani ambazo kama taifa bado hatujaruhusu watoto au hao vijana wazione?
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 5:49 PM
|
Permalink |
-
Watanzania tunajichanganya - Usasa na Ukale vyote twavitaka. Tatizo ni kuwa hata viongozi wetu hawajui wachukue lipi waache lipi. Ni kweli kuwa mambo tunayoiga au tunayoacha yaendelee kwa kudhani kuwa ndiyo mambo ya kisasa mengi yanapotosha jamii. Ni lazima tujivumie utamaduni wetu wa kiafrika na tuwe tayari kuulinda wakati wote na mahali popote.
-
Maswala ya mpito haya!Ila tusipoangalia tunaweza kuendelea kukemea upande mmoja na kuruhusu jambo hilo hilo upande wapili.
-
Hili ndio tatizo la viongozi wa kitanzania, yeye anafikiria picha za ngono ndio zinaambukiza ukimwi? Watu wenye ukimwi ndio wanaoambukiza ukimwi. Jamani tuna safari ndefu sana kwa kweli.
Katika kuiga ya usasa inabidi jamani tuwe makini sana. Kwani sasa hivi nimeona tanzania watu ni kuangalia tv tu saa zote sijui ni saa ngapi watu wanafikiria kuhusu mwelekeo wa maisha yao. Sisemi kwa ubaya lakini aha jamani mfano ni haya mashindano ya urembo, hivi jamani tunawakumbusha mabinti zetu kwamba bado wanatakiwa kusoma?
Watanzania tunajichanganya - Usasa na Ukale vyote twavitaka. Tatizo ni kuwa hata viongozi wetu hawajui wachukue lipi waache lipi. Ni kweli kuwa mambo tunayoiga au tunayoacha yaendelee kwa kudhani kuwa ndiyo mambo ya kisasa mengi yanapotosha jamii. Ni lazima tujivumie utamaduni wetu wa kiafrika na tuwe tayari kuulinda wakati wote na mahali popote.