VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Monday, December 17, 2007
PIGANIA UHURU WA KUJIELEZEA
Miaka michache iliyopita kulikuwa hakuna blogs. Kama ulitaka kusikika ilibidi utumie mlolongo mrefu sana. Mmojawapo ulikuwa ni ule wa kuandika barua kwa "mhariri".Na yeye,kutegemea na utashi wake au hongo aliyopokea juzi pale alipokutana na "mheshimiwa" katika ile baa karibu na wanaporandaranda "madada poa"(nasikia siku hizi wameingiliwa na makaka poa pia),mara nyingi zilikuwa zinaishia kapuni.

Matumizi ya blogs au uandishi huria kama ambavyo wengine wamependa kuuita, yameleta mapinduzi mapya. Bado yanaendelea kuleta mapinduzi mapya. Leo hii naweza kuandika na wewe ukasoma bila kupitia mlolongo mrefu. Unachotakiwa kuwa nacho ni tarakilishi na muda tu. Kizuri zaidi ni kwamba unaposoma nilichoandika unaweza kuchagua kukubaliana nami,kupingana nami au kunibeza tu na kuondoka zako kwenda uendako. Katika makundi yote hayo matatu unao pia uwezo wa kuniachia "vidonge" vyangu. Unaweza ukasema kwanini unakubaliana nami au unapingana nami. Mambo yanakwenda hivyo. Bila kurushiana ngumi wala kukunjiana ndita,tunaelimishana,tunajenga jamii.

Nasi, bila kukaa ndani ya yale masinagogi ya waandishi, tunaandika. Ukiamua kutuita waandishi au wacheza mduara ni juu yako.Tunachojua ni kwamba hivi sasa tuna uwezo wa kuandika na tukasomwa kuliko yule bwana mhariri mkuu.

Tatizo linakuja kwamba watawala walio wengi, wale ambao maisha yao yamejaa longolongo kila kukicha,huwa hawataki kusikia kitu kinachoitwa "uhuru wa kujielezea' achilia mbali uhuru wa vyombo vya habari wala waandishi. Ndio maana kuna mashirika au oganaizesheni kama PEN ambazo kazi yake kubwa ni kutetea uhuru wako wa kuandika,kusomwa nk. Hebu watembelee hapa, usichelee kujiunga nao. Soma visa mbalimbali vinavyowakuta waandishi. Pigania haki yako ya kujielezea.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 6:29 PM | Permalink |


Maoni: 1


   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker