Thursday, August 25, 2005
UNAFUATILIA YA LIBERIA?
Wakati Tanzania inakaribia kwenda kwenye gulio la kuchagua washika mstakabali wa nchi kwa miaka mingine mitano taifa la Liberia nalo pia lipo kwenye changamoto ya aina yake. Mwanasoka mashuhuri barani Afrika na Ulaya, George Weah ameamua kuyavulia nguo maji.Anasema sio lazima kuwa na makaratasi ya digrii ili kuongoza nchi.Uzalendo tu unatosha. Umaarufu utamsaidia? Unakumbuka enzi zile (1995) ambapo Keneth Pius Mkapa wa Yanga alikuwa na umaarufu na kujulikana zaidi ya mgombea wa uraisi wa wakati ule Benjamin William Mkapa? Soma zaidi hapa.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 3:02 PM
|
Permalink |
-
Hii ya Ken Mkapa na Benjamin Mkapa imenikumbusha wakati wa mkutano wa jinsia kule Beijing. Watu wengi walikuwa wakimjua na kujali habari za Zamoyoni Mogella kuliko Mama Getrude Mongella aliyekuwa mwenyekiti wa mkutano huo!
Hii ya Ken Mkapa na Benjamin Mkapa imenikumbusha wakati wa mkutano wa jinsia kule Beijing. Watu wengi walikuwa wakimjua na kujali habari za Zamoyoni Mogella kuliko Mama Getrude Mongella aliyekuwa mwenyekiti wa mkutano huo!