VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Monday, September 26, 2005
KUTOKA KIMARA MPAKA POSTA
Jogoo anawika, anawika tena.Namsikia kwa mbali.Mvua inanyesha na usingizi bado umenitawala. Jana nilichelewa sana kulala.Nilikuwa kwenye kikao cha harusi cha mfanyakazi mwenzetu. Ameamua kufunga pingu za maisha.Ama kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa, hakuna mtu alikuwa anapinga kuoa kama huyu bwana. Leo hii kakata shauri, anadai hakuna mafanikio katika mwanaume yoyote bila mwanamke! Hatuna budi kumuunga mkono.Michango inahitajika.
Nafumbua macho na kuangalia saa yangu, kumekucha na nikifanya mchezo nitachelewa kibaruani. Nimehamia nyumba hii siku si nyingi. Nimeanza juzi tu maisha ya kujitegemea baada ya miaka mingi ya kuishi na wazazi wangu pale Sinza-Makaburini. Nimehamia Kimara-Baruti.Nimepanga chumba kimoja-self contained.
Nakaa kitandani na kuwaza, utumwa huu utaisha lini? Hivi ni lazima niende kazini kila siku ndio niweze kuishi? Na kazi hii namfanyia nani kama sio yule yule mkoloni aliyetesa babu zangu? Hivi kizazi changu kimemkosea nini mwenyezi mungu? Utumwa uliisha kweli?

Nimesimama kwenye kituo cha daladala.Mkononi nimeshikilia shilingi mia na hamsini zangu,ndio nauli hiyo.Naogopa isije ikaniponyoka.Kugombana na kondakta wa daladala yataka moyo.Nimeketi dirishani,nawaza siku itakavyokwenda. Natazama abiria wenzangu, naona wote wamenuna.Ninatabasamu, huenda siko peke yangu mwenye kuonja makali ya maisha.Mbona hatuungani basi tukajikomboa kwa pamoja? Umoja sio nguvu tena?

Kutokea dirishani naona mengi.Naona picha za wagombea ubunge na uraisi zimetanda kila kona.Zina rangi za kila namna.Karibuni kila picha mgombea anatabasamu.Anacheka nini huyu?Au anatucheka sisi kwa ujinga wetu? Tutamchagua hata kama tunajua anatoa na kupokea rushwa kwa kwenda mbele.Tutamchagua kwa sababu tumeshakula pilau lake,hatuna jinsi.Anatudai kura yake.

Pembeni namuona jamaa anajisaidia haja ndogo.Hivi ustaarabu huu unatoka wapi?Au tuitupie lawama serikali kwa kutokuwa na vyoo vya kutosha mitaani? Ama! Namuona kibaka anamwibia dada mmoja mkufu wake.Asubuhi yote hii jamani.Dada anapiga makelele lakini hakuna anayemsaidia.Hasira zinanishika,natamani nishuke nikamsaidie huyu dada. Nikishuka nauli nyingine nitapata wapi? Sina jinsi.Kondakta ananipigia filimbi yake ya sarafu kiganjani.Usilale mkuu,kumekucha!

Nyuma yangu jamaa wawili wameanzisha mjadala wa kisiasa.Kila mmoja ana lake la kusema wakati huu.Nakumbuka jioni mtaani kwetu kuna mkutano wa kampeni.Itabidi niwahi kurudi nyumbani.Nasikia jamaa atagawa tisheti za bure.Nataka pia kumuuliza swali fulani.Sijui swali gani kwa sasa.Ninayo mengi.

Tunakata kona ya maktaba.Tayari tupo katikati ya jiji.Wauza magazeti wametapakaa kila sehemu.Wametoka kuchukua magazeti tayari kuyatembeza na kuuza.Siku hizi sinunui magazeti,yamejaa uongo na umbeya.Sijui unatusaidia nini. Kituo kikuu cha mabasi Posta mpya,tayari tumefika

Nanunua vitumbua kutoka kwa mama mchuuzi.Nimekumbuka sijapata kifungua kinywa.Sina mke na ukapera hauniruhusu kujitengenezea chai bado. Tutaendelea baadaye.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 1:11 PM | Permalink |


Maoni: 3


  • Tarehe: 2:22:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Indya Nkya

    Kaka hapa umenipeleka nyumbani. Ndio maisha ya kila siku. Hilo la kupora mkufu linahitaji makala nzima. Dar unaporwa halafu kila mtu anaangalia tuu. Ukiweza kupiga kelele jamaa akikamatwa anaweza akachomwa moto. Kazi ipo. Umenifurahisha sana kwa kila mgombea kutabasamu kwenye picha ya kampeni. Inafurahisha sana. Kila mmoja anaonyesha tabasamu.Tabasamu ya nini kwenye kampeni tuu?

     
  • Tarehe: 11:59:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Dennis Mponji

    Tabasalamu la hao wagombea ni la kutukebehi sisi wadanganyika katika hizo kelele wanazoziita shampeni akh sorry kampeni maana wanafurahia ulaji endapo watashinda nafasi wanazogombea.

     
  • Tarehe: 5:26:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Ndesanjo Macha

    Tunahitaji visa zaidi namna hii. Vinafurahisha lakini pia vimebeba mengi mno, kama Nkya alivyosema kuhusu suala la kupora mkufu ambalo linahitaji makala ndefu kabisa.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker