Saturday, September 03, 2005
VITA KATI YA BLOGGERS NA WENGINEO!
Wakati kama huu wa maafa ya kimbunga cha Katrina upatinakaji na upashaji habari ni jambo muhimu sana.Walio wengi tunakimbilia kwenye luninga kuangalia maendeleo ya shughuli za uokoaji,utafutaji wa waliopoteza maisha,upatikanaji wa misaada na hata sehemu ambazo kama unataka kusaidia,wapi upeleke msaada wako.Mtandao pia ni kiungo muhimu sana siku hizi.Ingawa kwa nchi zinazoendelea bado si watu wengi sana wenye uwezo wa kumiliki kompyuta ambazo zimeunganishwa kwa mawasiliano ya intaneti hali ni tofauti katika nchi zilizoendelea.Karibuni kila mtu anamiliki njia hii ya mawasiliano.Katika siku za karibuni technolojia ya kublog imezidi kuwa tishio kwa vyombo vya habari na mashirika mbalimbali ya habari ulimwenguni.Suala gumu ni kuhusu nani kati ya blogu mbalimbali za watu binafsi na mashirika makubwa ya habari anasema ukweli juu ya masuala mbalimbali.Soma zaidi hapa(samahani kwa wale wasiotumia lugha ya kiingereza)
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 12:44 PM
|
Permalink |
-
Habari nzuri hii. Mjadala na mzozo kuhusu uandishi asili na blogu utaendelea kwa muda. Nilikuwa kwenye mkutano fulani ambapo wanablogu walikuwa wakilalamika kuwa vyombo vikubwa vya habari vinawaita wao ni ma-amateur na wasithubutu kujiita ma-professional. Basi jamaa mmoja akasimama akasema kuwa neno "amateur" asili yake ni neno lenye kumaanisha "mtu apendaye afanyacho," hivyo akasema kuwa wanablogu wanapaswa kufurahi wakiitwa ma-amateur maana wanapenda wanachofanya!
Habari nzuri hii. Mjadala na mzozo kuhusu uandishi asili na blogu utaendelea kwa muda. Nilikuwa kwenye mkutano fulani ambapo wanablogu walikuwa wakilalamika kuwa vyombo vikubwa vya habari vinawaita wao ni ma-amateur na wasithubutu kujiita ma-professional. Basi jamaa mmoja akasimama akasema kuwa neno "amateur" asili yake ni neno lenye kumaanisha "mtu apendaye afanyacho," hivyo akasema kuwa wanablogu wanapaswa kufurahi wakiitwa ma-amateur maana wanapenda wanachofanya!