Katika zile makala zangu za kila jumapili kule Tanzania nimewahi kuandika kuhusu tofauti ya kimtazamo juu ya unene na wembamba baina ya Afrika na nje ya Afrika.Wakati huku katika nchi za magharibi unene ni ugonjwa katika sehemu nyingi za bara la Afrika unene ndio mambo yote.Ukiwa mnene utapewa kila aina ya heshima.Ukiwa mwembaba kikiibiwa kitu halahala kama hujaambiwa ni wewe,mwenzako mnene atapeta tu.Hapa Canada kwa mfano ukinenepeana watu wanakuonea huruma,kwa maana unaumwa wewe.Hebu soma kisa hiki kutoka huko Mauritania.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:15 PM | Permalink |
Suala la unene limenikumbusha jamaa yangu mmoja kule Moshi ambaye alikuwa akipata huzuni sana mara kitambi chake kinapopungua! Na jamaa mwingie aliyeshangaa kuwa nimetoka Marekani bila kitambi!
Suala la unene limenikumbusha jamaa yangu mmoja kule Moshi ambaye alikuwa akipata huzuni sana mara kitambi chake kinapopungua! Na jamaa mwingie aliyeshangaa kuwa nimetoka Marekani bila kitambi!