VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, November 30, 2005
BLOGU YANGU YA KIINGEREZA
Nimekata shauri.Sio lile shauri ya kujipandikiza pepo usio nao bali shauri langu ni la kuanzisha blogu ya kizungu au kiingereza maana ukweli ni kwamba wataliano,wapolish,wamagazijuto na wengineo wote ni wazungu pia. Nafikiri mtakumbuka kwamba nilianza kwa nia ya kuwa nachanganya lugha za kiswahili na kiingereza.Hilo limenifanya kukosa hadhira ya wasiojua kiswahili(kama wengi niishio nao hapa). Mawazo yangu,hisia zangu,misimamo yangu,mapendeleo yangu na jinsi gani ninavyoupenda uafrika wangu haukuwa na nafasi sana machoni mwa watu hawa.Hivyo ili kufikisha ujumbe wangu kikamili nimeamua kuanzisha hii hapa. Nimeiita proudafrican ili kutuma ujumbe maridhawa. Bado niko kwenye ujenzi wake lakini.Wakiniuliza kwanini nitawajibu.Nilitaka kuiita Kilimanjaro kwa sababu zangu za kiroho ila nikakuta kuna mzungu mmoja alishalichukua jina hilo na alivyo mtovu wa nidhamu mara ya mwisho aliigusa hiyo blogu yake mwaka 2001 au 2003 hivi.Hivi hamna utaratibu wa kuweza kurudisha kwa wahusika majina kama haya ambayo kwetu sisi wengine ndio makaburi ya wazee wetu?
Aluta Continua!
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 1:28 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 4:27:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    congrants Jeff, Blogu yako mpya inazalwa siku ya kuzaliwa kwangu n hivyo nakupongeza maana kweli kwa unayeishi nje ya Tanzania kuna hadhira inayotaka kupata cheche zako na kama ukiandika Kiswahili pekee hawawezi kukuelewa. Niko mbioni kuingia ukurasa huko lakini kwanza ngoja nilikomaze hili Kasri langu.

     
  • Tarehe: 10:38:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Ahsante Boniphace,
    Hongera ya siku ya kuzaliwa.Hongera sana.

     
  • Tarehe: 6:16:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mloyi

    Nadhani bado hujakiaga kiswahili, hivyo hapa utakikubali....
    Sio wote tunazungumza kiswahili, hivyo uamuzi wako unaelekea kuwa na lengo la kupanua upeo, wadau kuongezeka, mawazo mapya kuingia na kuwapa nafasi pia.
    Endelea hivyohivyo lakini usisahau kwamba hapa bado tunakuhitaji.
    ...umekumbuka kuiomba msaamaha mizimu kwa kutotumia lugha iliyokaribu nao?...

     
  • Tarehe: 8:26:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Ndesanjo Macha

    Jeff, uamuzi wako sio mbaya. Unajua tunapoamua kublogu kwa Kiswahili hatumaanishi kuwa tuna ubaya na kiingereza, kifaransa, kichina, n.k. Tunachosema ni kuwa kuna mambo ambayo tunaongea sisi kwa sisi kwahiyo hatuhitaji kutumia lugha ya watu wengine. Pia tunasema kuwa kuna watu wetu wengi ambao hawaelewi lugha ya kiingereza kwahiyo itakuwa ni kosa kubwa kama tunataka kuelimishana juu ya utamaduni wetu, demokrasia, historia yetu, n.k. kwa kutumia lugha ambayo watu ambao tunataka kuelimishana nao hawaielewi. Kwahiyo tunapoongea sisi kwa sisi hatuhitaji hata kidogo kuazima lugha wakati tunayo lugha ambayo wote tunaielewa.

    Jambo jingine tunalofanya ni hili ambalo ni sawa na lile ambalo Ngugi aliliandikia kitabu. Kitabu kiliitwa "Decolonising the Mind." Hata ndugu Chinweizu wa Nigeria (Mloyi unampata sana huyu bwana) aliandika kitabu kiitwacho, "Decolonising African Literature." Sasa sisi tunachofanya kwa lugha hiyo ya kimombo ni "Decolonising Blogosphere" au "Decolonising Cyberspace." Tunaondoa ukoloni kwenye ulimwengu wa blogu. Tunaondoa ukoloni kwenye mtandao wa kompyuta. Ukoloni huo ni hali ile inayotulazimisha kutumia lugha waliyotupa wakoloni hata pale tunapoongea sisi kwa sisi.

    Na pia bila mjadala wowote, hii ni lugha yetu! Au sio?

    Tuje sasa kwenye kiingereza. Kwanza niseme kidogo juu ya lugha. Lugha ina kazi moja kuu: chombo cha mawasiliano. Lakini ina kazi nyingine kuu: lugha ni benki ya maarifa, utamaduni, desturi, na historia. Kutokana na sababu hii unaona kuwa unapotaka kummaliza mtu unamyang'ganya lugha yake. Mtu akipoteza lugha anakuwa amejipoteza. Amepoteza utamaduni na historia yake. Lugha inapopotea duniani ni sawa na kuchoma moto maktaba yenye orofa maelfu na maelfu. Hapo ndio unaona umuhimu wa kutumia zana za teknolojia mpya kutunza historia yetu na kurekodi mambo kwa lugha yetu.

    Mimi sina ubaya na kiingereza kama chombo cha mawasiliano. Huwa ninapenda kusema hii hoja mara kwa mara maana watu wengi wanaponisoma wanadhani kuwa nina "siasa kali" dhidi ya kiingereza na ninahukumu Waafrika wanaokitumia. Kumbe sivyo. Siwezi kuwa na ubaya na lugha ambayo inaniwezesha kuwasiliana na watu wengine wema duniani. Inaniwezesha kuwasiliana na kaka na dada zangu Marekani waliochukuliwa utumwani. Imeniwezesha kufaidia mafunzo ya muziki wa Bob Marley. Imeniwezesha kumsoma Wole Soyinka, Dambudzo Marechera, na wengine. Ninatumia lugha hii katika kazi zangu kwenye mradi wa Sauti za Dunia.

    Tatizo langu linakuja pale tunapozungumzia lugha kama benki ya maarifa. Hapo kiingereza kinakuwa hakina nafasi kwangu kwani nina lugha nyingine za kiafrika ambazo zinatunza utamaduni na historia yangu. Hapo ndio ninaingia na kampeni yangu ya kublogu kwa lugha za Kiafrika.

    Ninapokuja katika suala la kuwasiliana na dunia, nitasema kuwa kiingereza kina nafasi yake na heshima yake. Tena kina nafasi kubwa sana maana tunaishi katika dunia ambayo inatuchambua Waafrika katika mantiki ya njaa, vita, ukimwi, ufukara, n.k. Kwahiyo tunaweza kutumia lugha wanayoielewa hao wanaotuchambua namna hiyo kuwaonyesha afrika ni nini kwetu? Kwamba Afrika kwetu ni zaidi ya vita vya Sudan, mauaji ya Rwanda, utawala songombingo wa Somalia, n.k.

    Hongera, Jeff.

     
  • Tarehe: 10:20:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Ndesanjo,
    Umenihamasisha isivyo kawaida kwa ukweli ulivyouchambua hapa.Naomba ruhusa yako nifanye tafsiri ya uliyoyasema hapa kwenye blogu yangu ya kiingereza.Naamini hata hawa wazungu wanahitaji kuelimishwa kuhusu masuala haya ya lugha.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker