Wandugu,Kuanzia wiki hii nitakuwa naweka hapa kwenye tovuti yangu mashairi ambayo nimekuwa nayaandika mara kwa mara.Nitakuwa nikiweka shairi angalau moja kwa wiki.Nikisahau ruksa kunikumbusha. Ukiniita mshairi sitakataa.Ila naomba ufahamu kwamba mashairi yangu hayana kanuni, naandika nitakavyo, kwa raha zangu,kero zangu,hasira zangu nk.Unaweza pia usinielewe naongelea nini.Hiyo itakuwa ni sehemu ya sanaa ya ushairi. Hili hapa chini nimeliita NIAZIMENI AKILI ZENU.
Udhia huu unatoka wapi na unatokana na nini?Adhama hii itadumu mpaka lini,au ni ya muda mfupi tu?Jana tumeadhimisha sikukuu gani au shujaa gani kazaliwa?Au pengine amechipukia wapi,kaambiwa na nani ukweli?Kengele ya adhuhuri imepigwa,waungwana waende kujisafiMaadili yangali yanahitajika, ingawa naona kama yameshatuponyokaAu yamekuwa adimu na bila maafikiano ya kiungwanaLakini tusiahirishe mkakati wetu wa ukombozi, tusitende dhambi hiyo kamweNoeni visu na kuweka ala zenu mahali pake, hatujui mbeleni kunaniAmbatana na ufananao, lakini usikatae usiofanana nao piaTutakuita mbaguzi, tafadhali usikatae tukifanya hivyoAnga limejaa harufu mbaya, pua zangu zinanusa damu zaidiNajiapiza kwamba sitaki kuona vita, halafu najiona mbumbumbuVipi kama wenzangu wanataka vita, mimi ndio nibaki ndani?Ardhi hii ni ya nani?Au mpaka wale waketio Areopago waamua kunikabidhi?Wanipe na kipande cha karatasi chenye jina langu?Ishara hizi ni za nini ,wewe unaziamini?Unataka na mimi niasi? Majuha si watanishangaa?Nimechanganyikiwa kwa sababu napinga uzunguAu nisimame madhabahuni kama askofuNipayuke kwa nguvu zangu zoteKisha nisitende hata moja nisemalo, nipunge mkono niende zanguHivi hapo awali mambo yalikuwa ya aina gani?Nataka kujua lakini sioni wa kumuulizaWengi wananitazama kwa jicho baya, wananiombea dua mbayaNimeazimia kukomboa wengi,nimeanza na kaya yangu kwanzaNaomba mnikopeshe akili kwenye vichwa vyenu nyoteMasikio siihitaji,yanaingiza na kutoa Nataka kubatilisha kitendawili, hiki kigumu kuliko vyote.
Jeff waweza himili, akili zetu hifadhi?
Nadhani wataka jina, siri zidi fukiani
Jinalo ukurasani, vema tulishakupani,
Kisha akafika yule TUME, ushindi kakunyimani?
Funuka sasa tazama, hapana kuogopani
Kunywa damu ya kiama, umimi umezidini
Kwa sasa ninainama, Natulia Kasirini
Karibu Malenga Jeff, zindiko tuligangeni.