VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Thursday, December 08, 2005
HEKA HEKA ZA PASIPOTI MPYA!

Mambo mawili muhimu sana yanatokea nchini Tanzania mwaka huu.Jambo la kwanza ni hili la uchaguzi mkuu ambao unafanyika wiki ijayo baada ya kuahirishwa kwa muda kufuatia kifo cha mgombea mwenza wa nafasi ya uraisi katika Chadema. Macho na masikio yetu bado yameelekezwa katika uchaguzi huo.Leo sina mengi kuhusu uchaguzi.
Jambo la pili ambalo ndio msingi wa habari hii ni hili zoezi adimu la kubadilisha pasipoti.Kisingizio kinajulikana.Ni amri kutoka kwa wenzetu wa magharibi katika juhudi zao za kupambana na ugaidi duniani.Tunaambiwa kwamba pasipoti zetu za zamani zilikuwa hazisomeki kwa machine kama za nchi nyingine duniani kwa hiyo ilitubidi tuzibadilishe,tupende tusipende.Nathubutu kuiita amri kwa sababu kama isingekuwa amri basi utaratibu mrahisi sana ungetumika kwamba kama una pasipoti ya zamani basi ikiisha muda wake, ukienda kubadilisha unapewa mpya. Na kama hujawahi kuwa na pasipoti kabla ya hapo basi moja kwa moja unapewa mpya. Katika kipindi cha miaka mitano watanzania wote wangekuwa na pasipoti mpya na fedha chungu mbovu zingeokolewa na kupelekwa kwenye miradi ya kimaendeleo. Lakini kwa sababu za kiusalama,sababu za kijasusi dhidi ya ugaidi duniani wafadhili wangekataa.Wangetuelewa endapo tu tungekuwa na viongozi wenye uwezo wa kutetea maslahi ya nchi bila woga.Kwa hivyo basi zoezi hili la kubadilisha pasipoti lingekuwa limetazamwa kwa undani,kitaalamu ili kujua jinsi gani lifanyike.
Badala yake zoezi hili limegeuka kuwa kero ambayo inawafanya wengi(hususani waliopo nje ya nchi na wasio na moyo) kuamua kuukana moja kwa moja uraia wao halali wa Tanzania.Siwalaumu kwa kweli. Hili lina madhara yake.Wachumi na wanajamii wanajua zaidi kuhusu masuala kama hayo.Kero kubwa ni katika utaratibu mzima wa kubadilisha pasi hizo za kusafiria. Mengi yameandikwa kuhusu uzembe, ukiritimba kuhusiana na suala zima la kubadilisha pasipoti.
Nilipokuwa nikisoma habari mbalimbali katika vyombo vya habari kuhusiana na utaratibu mzima wa kubadilisha pasipoti nilidhani ni mapungufu yetu ya kawaida ambayo yanaongeleka.Kimbembe kimekuja nilipojaribu kuyavulia nguo maji ili kubadilisha pasipoti yangu kupitia ubalozi wetu hapa Canada. Labda niseme wazi kwamba ndio kwanza nimeanza zoezi hili la kubadilisha pasipoti. Na mpaka hapa nilipo nimeshakwama.Poleni wenzangu ambao mpo kwenye hali kama yangu.Najua mpo wengi.
Nimeagiza fomu kutoka ubalozini.Nikaambiwa kwamba ni lazima niilipie hiyo fomu $ 20. Kwanza nilishtuka kwa sababu nimeshaanza kuzoea utaratibu wa hapa Canada kwamba hamna hata fomu moja utakayopewa kwa mauzo.Iwe ni ya kuomba uraia,makazi ya kudumu n.k.Unaweza kuletewa hata fomu kumi kwa mkupuo ukitaka.Kwanini uuziwe fomu??Kodi wanazokatwa wananchi zinafanya nini? Nikaona isiwe tabu nikaagiza washirika wangu waliopo huko ulipo ubalozi wetu(Ottawa- mwendo wa kama masaa sita kutoka hapa Toronto kwa gari).

Kichefuchefu kilianza kunipata baada ya kufungua hiyo fomu yenyewe na kugundua kwamba ni fomu sawa sawa kabisa na zile tulizojaza miaka ile wakati tukiomba pasipoti zinazobadilishwa.Sana sana nimeona vifungu vichache sana ambavyo vimebadilishwa.
Wakati naanza kusamehe hayo yote nikagundua kwamba hii fomu imetengenezwa zaidi na inafaa zaidi kwa mtu ambaye bado yupo nyumbani Tanzania.Haijatengenezwa kukidhi haja ya mtanzania aliyeko nje ya nchi. Sababu ni nyingi ila ngoja nijaribu kueleza chache hapa chini.
Fomu imeandikwa kwa kiswahili kitupu bila hata tafsiri ya neno moja la kiingereza. Lazima tukubali kwamba kiswahili chetu bado sio cha kimataifa kiasi cha kutumika ulimwengu mzima. Maelekezo ya jinsi ya kujaza fomu hiyo kwenye tovuti ya ubalozi yote yameandikwa kwa kiingereza! Nadhani hata wao wanakubaliana nami kwamba kiswahili hakina nafasi hapa. Lakini pia nashindwa kuelewa kwamba kwanini tovuti kama hii ya ubalozi haina uhuru wa kuchagua lugha ya kiswahili au kiingereza? Mapungufu mengine haya.Fomu inanitaka nijaze sehemu zinazouliza mtaa/kijiji.Sijui naishi kijiji gani hapa Toronto! Hamna vijiji hapa ninapoishi.
Tayari nipo hapa,fomu inanitaka nijaze madhumuni ya safari na nchi ninazokwenda.Safari gani? Siendi popote kwa hivi sasa
Fomu inanitaka nijaze kazi ninayofanya,kiswahili chake sikijui
Fomu ina kipengele cha shuhuda kwa mwombaji
ambaye anaweza akawa jaji.kabidhi wasii,hakimu.wakili/kamishna wa viapo akiwa yeye mwenyewe ni raia wa Tanzania.Nimtoe wapi mtu kama huyo hapa Canada ndugu zangu? Hata kama nitampata hakimu,jaji nk wa hapa, nani atafanya kazi ya kutafsiri fomu hiyo?
Shuhuda anatakiwa aandike nyuma ya picha kwamba hiyo ni sura yangu.
Pili zimetolewa sampuli za picha pale,sijui wazungu wa wapi wale.Yaani tumeshindwa kabisa kuweka picha za watanzania wenzetu kama sampuli za jinsi gani picha hizo zipigwe?

Maswali magumu yenye majibu haba yananijia.Hivi sisi watanzania tuna nini jamani? Hawa tunaowaita viongozi wa nchi,mawaziri,mabalozi,wabunge ni kina hasa?Wizara za mambo ya ndani na nje wanafanya kazi gani?Kuna jamaa aliwahi kuniambia kwamba Tanzania hatuna mameneja wazuri. Sijui nikubaliane naye au nikatae?
Najua serikali yetu ni bingwa wa kupuuzia mambo.Hili nadhani lisipuuziwe.Ni aibu kwa taifa letu. Lazima serikali ikiri kwamba zoezi hili halikuangaliwa kwa makini.Walioboronga wasihamishiwe wizara zingine bali wajiuzulu au waachishwe kazi kwa nguvu.
Majuzi nimesoma mahali kwamba bidhaa za kutengenezea pasipoti mpya hamna/zimekwisha! Muda wa kusubiri pasipoti mpya ni kama miezi sita hivi. Kwa nchi yenye watu milioni 37 na ambao kati yao asilimia ndogo sana wanatumia pasipoti zao ambayo ni haki yao ya kikatiba. Kwanini utake kujua mtu anakwenda wapi,kufanya nini? Kwanini hilo lisiachiwe balozi husika?Lina uhusiano gani na pasipoti?
Kero ni nyingi sana juu ya suala hili.Wakati umefika,tuseme ukweli.Tuishauri serikali yetu,tuikosoe na isione aibu kukubali kama imekosea. Tuanzie hapa kwenye ulimwengu wa blogu.


 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 12:00 PM | Permalink |


Maoni: 6


  • Tarehe: 2:33:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Bora umeanza kuogelea katika bahari ya Wafalme Juha wa Tanzania. Una kazi ya kuvuka mto hapo ni bado. Niko bize wiki hii lakini ngekuandikia mengi kuhusu namna nilivyotaabika kupata hicho kijitabu mwaita Pasipoti. Sasa kichefuchefu ni pale nilipokuwa napita kuingia Uwanja wa ndege sehemu ya abiria, kakaja kakijana umri wangu hivi kanauliza dokumenti zangu za kusafiria kuja Marekani! Zinakahusu nini haka utadhani kanafanya kazi ya ukonsula ubalozi wa Marekani? Nikakatazama, kisha nikakajibu kwa kizungu feki, kakanitazama pia. Sasa acha tu nikirudi huku wakati utakuwa ni kuwafanyia vituko mpaka wakome maana wamezidi hawa.

     
  • Tarehe: 4:49:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger patashika

    hako kakijana kama ni hakohako hata mimi kalinifata siku moja nikakadharau wanapenda kutishia watu kama hujielewi wanakuletea za kuleta halafu wanachukua rushwa, kazi mbovu sana.

     
  • Tarehe: 11:28:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Ndesanjo Macha

    Ngoja nitawasaidieni kukitie kelbu hako kakijana!

    Msangi: sijui ni lini serikali yetu itaamua kufanya mambo jinsi yanavyotakiwa kufanywa. Lini?

    Umenishangaza sana kuwa mfano wa picha zinazohitajika kupata pasi ya kusafiri ya Tanzania ni za wazungu. Naona kama hii ni zaidi na utumwa wa kimawazo. Tunatakiwa kuipelekea serikali Milembe?

     
  • Tarehe: 12:24:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Ndesanjo,
    Kwa kweli hili la kuweka picha za wazungu kama mfano hata mimi limenikera sana.Ninapanga kuonana na balozi wetu hapa Canada kuhusu hili suala.Nikikaa kimya kizazi kijacho kitanilaumu.

     
  • Tarehe: 5:18:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Hizo picha si kuwa ziko Canada tu bali hata pale Dar Uhamiaji nilikutana nazo na kuanza kuulizia lakini mshambenga mmoja akanipa jibu kuwa wanaochukua pasipotio wengi ni ninyi wenye asili ya kizungu au Kihindi na sisi akina Makene pasipoti za nini kaka maana hata pesa ya kununulia ugali tabu hivyo picha yangu ya kwenye Kasri itumikeje kuwa mfano wa picha safi ili kuchukua pasipoti za Tanzania. Tumejidharau sisi au kupenda vitu vyepesi vyepesi, bila shaka Marekani ilipeleka aina ya picha inazotaka zitokezee katika pasipoti. Si unakumbuka kuwa taarifa zetu zilikuwa page ya kwanza na hapo ndipo palikuuwa pakibandikwa picha. Nini kiliwafanya kugeuza na kuweka kule nyuma. Au kutafuta zifanane na za Canada na Marekani? Safari safari safari Jeff Msangi kaza Buti Mheshimiwa Waziri Mkuu nakufahamu wewe si kama Suamaye. Unawajibika kwelikweli kisa cha kuandika na kuelezea safari yako ya kutoka Kimara kwenda Posta. Usisahau makala hiyo ulionyesha mkakati wa kupambana na hali hii. Amua kuanza safari sasa, ila lile la kukakimbia kauraia silizingumzii sasa naogopa mkong'oto mheshimiwa Waziri Mkuu.

     
  • Tarehe: 12:52:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Pole sana bwana Msangi kwa usumbufu huo. Mwenzio hayo matatizo ya kubadili pasi ya kusaifiria nilikutana nayo pia; tena makubwa tu.

    Mimi ninaishi Kanada pia, nipo ktk miji pacha ya Kitchener-Waterloo. Sasa nilikuwa nina mpango wa kusaifiri kwenda D'salaam mwaka jana kwenye mwezi wa 7 na kukaa kwa miezi miwili. Hivyo nilipopata habari juu ya zoezi hilo la ubadilishaji wa pasi za kusafiria nikaona bora nikafuatilie huko huko mwenyewe ambapo naweza 'kuichakarikia' na nilikuwa na imai kuwa katika muda wa miezi miwili niliyokuwa napanga kukaa nyumbani ningeweza kukamilisha zoezi hilo.

    Bahati mbaya safari hiyo ikaahirishwa dakika ya mwisho na nikalazimika kwenda mwanzoni mwa mwezi Novema. Tatizo ni kuwa muhula wa chuo wa majira ya kipupwe ulikuwa umeshaanza hapa, hivyo nilikuwa siwezi kukaa kwa muda wa zaidi ya wiki 2 maana ninasomea shahada yangu ya 2 katika Chuo Kikuu cha Waterloo.

    Basi bwana usiombee balaaa niliyokutaan nayo huko. Kama unafikiri "kufukuzia" pasi hiyo ni adha wakati hauna haraka wala safari yoyote; jiulize inakuwaje kama uko katika nafasi niliyokuwepo mimi.

    Kuzungushwa kila sehemu, kujazishwa fomu kadha wa kadha na kila ukirudisha wanakuonyeha upungufu mmoja ambao ukienda kuukamilisha na kurudi tena, watagundua kosa jinginie na kukurudisha mara ya 2, na ya 3.

    Ila kinachoudhi zaidi ni pale ambapo unaanza kuambiwa ukusanye kila cheti na kila kitu upya wakati walishaweka "documents"zote katika kumbu kumbu zao. Sasa ya nini kufungua jalada la kumbu kumbu kama kila siku itakuwa ni suala hilo hilo la "nenda kaleet cheti hiki na barua ile, n.k."

    Kama ulivyobainisha bwana Jeff, iwapo suala hili lisingewekewa shinikizo na wababe wa ulimwengu huu mabadiliko haya yangeweza kuchukua utaratibu unaofaa na hivyo kuokoa fedha nyngi ambazo zingeweza kutumika kuboresha ofisi hiyo ya uhamiaji na kuongeza ufanisi wa shughuli zao.
    Inasikitisha na kutia aibu kuona ofisi kubwa na ya muhimu kama ile haina hata "computer" ndio maana wanashindwa kutunza nakala na kumbu kumbu ipasavyo. Mafaili yamelundikana hovyo kila mahala, sijui hata utaanzia wapi kutafuta faili la mtu. Ndio maana wenyewe wanaona bora tu wakukusanyishe vyeti vyote upya kila uendapo kubadili pasi hiyo.

    Kimbembe ni kuwa sasa nilikuwa nachelewwa kurudi chuo hivyo kujiweka hatarini kupoteza udhamini wangu ktk masomo... na kasheshe liliibuka pale nilipotonywa na mmoja wa maofisa hapo uhamiaji kuwa kulikuwa na upungufu mkubwa sana wa vitabu vya kuchapishia pasi ikilinganishwa na maombi yaliyowasilishwa. Ilibidi ujuane na wakubwa kweli kweli kuweza kupata kwa muda mfupi amao mi nilikuwa naihitaji.
    ===================================

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker