VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, January 18, 2006
BAHARI NA SAMAKI WAKE!
Mtanisamehe kama ninalotaka kutoboa hapa ni gumu kama paa la zege.Nimepata ndoto,nimeota nimekaa pembeni mwa bahari.Sina uhakika kama ilikuwa ni maeneo ya kigamboni au pwani ya raha leo pale jijini Tanga.Ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kifua wazi huku nimevaa msuli fupi.Nadhani wale mnaojua shughuli za uvuvi mnaelewa nilikuwa nimevaa nini.Ni majira ya jioni,karibuni jua linazama.Bado sijafanikiwa kupata samaki angalau wa kutosha kwa mlo wa familia na wengine nipeleke pale gulioni ili nipate faranga za kununulia mitumba ya waitaliano,nasikia ni mizuri kuliko ile ya waingereza.Kikwapa kinacheua harufu ya mferejini maana siku nzima pembeni ya maji chumvi sio mchezo,hata ukikoga hutakati,shombo ya samaki bwana,ah!

Cha ajabu bahari imejaa samaki mpaka nawaona wakielea juu juu.Wengine wanacheza kama vile kiwi,dolphino na chamaki nchanga.Nadhani ushawahi kumkurupusha chumbani mwako chamaki nchanga ukaona jinsi anavyotoka mkuku.Kijasho kitakutoka kwa sababu utabinua vitanda na makabati karibuni yote.Nguvu kipindi hicho unakuwa nazo maana chamaki huyu ashakutia hasara sana tu.Ashararua viwalo vyako vyote vya kutokea. Samaki wanazidi kunichenga ingawa nyavu yangu bado ni mpya. Au labda ujuzi wa uvuvi umeanza kunitoka?Mbona???? Taratibu jua linaanza kupotelea magharibi,miayo na uchovu vimenitawala. Nashtuka huku nikiwa nimeloa jasho.Nini maana ya ndoto hii??

Blogu naifananisha na bahari.Wavuvi ndio wanablogu wenyewe yaani waandishi.Wanunuzi wa samaki ni wasomaji,wachangia mada na hoja,wapambe,warekebishaji wetu. Na kwa sababu wavuvi nao hutokea wakawa wanunuzi(hususani katika zile siku wanaposhindwa kwenda kuvua au wanapokuwa kama mvuvi mimi niliyetoka kapa) basi sote tunahusika.Haijalishi kama tunafunga safari kwenda sokoni au tunaketi tu nje ya vibaraza vyetu tukisubiri sauti ya mchuuzi "haya tena samaki wa reo reo, kina baba na kina mama samaki kwa afya zenu,hero hero baba juu,mama chini, samaaaaaaki" nk

Sasa kama sisi ni wavuvi,wanunuzi wanatutegemea sana.Na wanatutegemea tuwaletee kila aina ya samaki sokoni.Wanataka changu,kambale,pweza,nk.Lakini hali inakuwaje kama wanunuzi wanakuja sokoni na kukuta hakuna samaki wa aina yoyote ile?Ni wazi kwamba watakuwa hawana jinsi zaidi ya kusaka mlo wa aina nyingine,pengine watakula dengu au choroko watulie wasubiri mashuzi.

Hii inaweza kuwa ndoto tu, ndoto ambayo haihitaji kwenda kwa babu chalii kupatiwa tafsiri.Msamaha niliouomba hapo juu unahusiana zaidi na kuona kwangu kwamba kuna "ubaridi" fulani katika uwanja huu wa blogu.Nimejaribu kupitia blogu kadha wa kadha,naona wengi shughuli zimewawieni nyingi.Wengi hamuandiki tena,hamtoi hoja,hampiti uwanjani,hata peku huku umande ukiwa umetanda.Wanunuzi tumewasahau.Najua hili jukumu ni la kujitolea,halina malipo ya moja kwa moja ingawa malipo ya kijamii ni mengi sana.Kwa vizazi hivi na vijavyo,vyetu na visivyokuwa vyetu.Naizungumzia dunia hapa.Nawasihi tuendelee kujitolea. Makene na Ndesanjo wamesimama mstari wa mbele katika kuleta wanablogu wapya.Hili ni jukumu letu sote. Lakini litawezekana tu endapo mualika anakuwa hima kuandaa mazingira ya mwalikwa.Kama ambavyo Ndesanjo amesema leo katika blogu yake,safari ni ndefu na sisi ndio tumeianza tu.Tunachojenga hapa ni msingi.Sasa kama mnavyojua zege halilali.Ninachoomba wanapokuja wanunuzi sokoni,wasikose samaki.Wakikosa hawatokuwa na hamu ya kugeuka kuwa wavuvi.Watahisi bahari imekauka! Ikiwezekana kila siku tutume japo chochote,hata kama ni dagaa wa kigoma.Hii itasaidia kuleta mapinduzi tunayoyatarajia. Aluta Kontinua!
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 1:08 PM | Permalink |


Maoni: 3


  • Tarehe: 2:56:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Nimesoma Jeff, nimesoma....

     
  • Tarehe: 2:52:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger FOSEWERD Initiatives

    nimekupata.....ni kweli kabisa....ni kweli kabisa.....

     
  • Tarehe: 8:34:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Ndesanjo Macha

    Jeff, lazima tuendelee kusisitiza kuwa tunachofanya ni kujenga msingi. Huu ni mwanzo tu. Mwanzo wenyewe mzuri. Jambo la kukumbuka ni kuwa faida ya redio sio pale ambapo kila mtu ana redio. Faida ya gazeti sio lazima kila mtu asome gazeti. Na blogu ndivyo hivyo. Sio lazima kila mtu awe na mtandao wa tarakilishi eti ndio blogu ziwe na faida. Tazama kwa mfano blogu ya Michuzi...zile picha tungezifaidi vipi na lini kama sio blogu yake?

    Nawaambia marafiki kila siku: tuko kwenye mapinduzi makubwa sana ingawa unaweza usiyaone.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker