VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, January 13, 2006
ETI NANI MASIKINI?
Jana jioni nilihudhuria mdahalo kuhusu umasikini au niseme kampeni ya kuufanya umasikini ubakie historia tawi la hapa Canada. Mdahalo huo ulikuwa umeandaliwa na shirika hili hapa na kufanyikia hapa. Mdahalo huu ulilenga kutaka kujua msimamo au muelekeo wa vyama mbalimbali vya siasa hapa Canada kuhusu umasikini duniani na hata hapa Canada tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu tarehe 23 mwezi huu.Upande wa waulizwa maswali walikuwa ni wawakilishi(wote walikuwa ni wagombea ubunge) wa vyama vyao.Kuna vyama vinne vikuu vya siasa hapa Canada. Mmojawapo wa watu muhimu na mashuhuri waliokuwepo upande wa wauliza maswali na watoa hoja mbalimbali ni Stephen Lewis ambaye pia anaendesha shirika hili hapa.

Umasikini unapoongelewa huwa Afrika inaongelewa.Dunia inaamini kwamba sisi ni masikini.Mwishoni nilipata nafasi ya kuongea na waandaji na pia Stephen Lewis.Niliwaambia jambo moja.Afrika sio masikini hata kidogo.Umasikini wa Afrika ni hoja ya kimagharibi na kwamba kama kampeni hii haitabadilisha mwelekeo na kutafuta jina jipya badala ya "umasikini" basi hakuna watakalofanikiwa milele.Kwanini?Nikawaambia kwamba binadamu yoyote ana jinsi yake ya kupokea anayoyasikia mara kwa mara.Ukimwambia mtoto mdogo au hata mtu mzima kwamba ana sura mbaya,kila siku,inafikia mahali,hata kama ana uzuri wa Cleopatra,ataamini kwamba yeye ni mbaya.Atakachoanza kufanya ni kutafuta "urembo kutoka dukani kwa mangi". Hilo ndilo linaloendelea hivi sasa duniani,kwa kampeni kubwa kubwa mpaka za matamasha makubwa kama Live8 ya mwaka jana.Kitakachofanyika au kinachofanyika hivi sasa ni sumu mbaya kuliko yoyote ile iliyowahi kutokea.Watu watakaa,vichwa chini,wakiamini kwamba wao ni masikini wasioweza kufanya chochote.Kinachotakiwa ni kuhamasisha wananchi kutumia rasilimali walizonazo,zilizowazunguka kuinua hali zao za kiuchumi.Chukua mfano mdogo ambao Ndesanjo aliwahi kunikumbusha,hivi kwanini na inakuwaje makabila au watu walioko kwenye sehemu kama zinazozunguka "dhahabu" za utalii kama Mlima Kilimanjaro,mbuga kama Ngorongoro na Serengeti wanabakia masikini??
Jamaa walibaki midomo wazi hawakuwa na majibu ya haraka.Wameniomba kukutana nao tena ili tuchanganue hoja hii kwa mapana na marefu zaidi.Unasemaje?
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:56 PM | Permalink |


Maoni: 2


  • Tarehe: 7:09:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger FOSEWERD Initiatives

    sawa hasa kaka jeff. ninachokufurahia wewe ni balozi mzuri wa mawazo yaliyochekechwa na bunga bongo kwa wadau. umefanya vyema kabisa. sasa ukiwa unajadili nao hili ambalo walikuwa hawalijui, pia uwakumbushe kile kilio cha kila mara cha mkapa kuwa kwa sasa hatupendi sana kupokea misaada lakini tunalilia fursa sawa ya biashara - au level ground. nilisoma juzi european market imefinya mgao wa kuchukua bidhaa toka afrika na hapo hapo inaongeza misaada! - kwa ujumla ni mfumo, nina uhakika unajua mengi sana katika uwanja huu! kila kheri!

     
  • Tarehe: 1:26:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Ndesanjo Macha

    Dhana kuwa Afrika ni masikini inafanya kazi moja kubwa sana: kuendeleza sekta ya misaada ya fedha/utaalamu na kuyapa mashirika ya "misaada" kazi na kuwalipa wenye mashirika hayo mishahara na marupurupu. Sababu kubwa ya kuita blogu yangu Jikomboe ni kutokana na imani ya dhati niliyonayo kuwa sisi Waafrika wenyewe tuna suluhisho na dawa ya matatizo yetu. Lakini suluhisho hilo litapatikana pale tutakapoamua kusema kuwa "tunaweza." Tukiamini kuwa sisi masikini tukakubali kuongozwa na serikali zinazozunguka na mabakuli Ulaya na Marekani kuomba na wasomi wetu nao na mabakuli wakiomba fedha kwa ajili ya mashirika yao yasiyo ya kiserikali, tutayasikia maendeleo kwenye bomba. Sisi na vizazi elfu kadhaa vijavyo.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker