Saturday, January 14, 2006
MICHEZO KWA WOTE!
Mojawapo ya maadhimio yangu ya mwaka 2006 ni pamoja na kuwa naweka kwenye blogu(neno mbadala bado halijapatikana) matukio na maadhimisho mbalimbali yanayotokea duniani kote na zaidi hapa Canada.Hivyo nitakuwa nafuata Kalenda yangu ili niweze kutopitwa na wakati.Nadhani ni vizuri pia kama wanablogu wengine wote mliotanda sehemu mbalimbali za dunia mkawa mnatuletea matukio na maadhimisho kutoka huko mlipo.Hii itatusaidia sote kujua tamaduni,sanaa,siasa,vituko,ndebwe nk kutoka sehemu mbalimbali duniani ili dunia iwe kijiji kama kile nitokacho mimi.Basi kuanzia jana tarehe 13 mpaka 15 Januari kuna michezo hii hapa kwa ajili ya walemavu hapa Ontario katika mji wa Huntsville.Sina uhakika kama Tanzania ina michezo kama hii kwa ajili ya walemavu.Kama hakuna ni muhimu ikawepo.Kuna haki nyingine za walemavu ambazo nitazizungumzia siku nyingine.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 12:55 PM
|
Permalink |
-
Msangi,
Nimesoma habari katika Mwananchi Jumapili nikakumbuka mjadala uliouanzisha juma lililopita.
"majambazi yamtumia salamu Mwapachu...yafunga mtaa, yapora kweupee...ni wiki moja baada ya kuwatemea cheche!" ndicho kichwa cha habari kilichonistua. Yaani pamoja na kauli ya vitisho hivyo bado wanavamia mitaa? Hawaogopi? Hawakusikia? Kwa nini lakini?
Huo ni uthibitisho kuwa kuwatishia eti watauawa, ni kupoteza muda tu. Mheshimiwa Waziri atafute mbinu nyingine, hiyo aliyoanza nayo itaigharimu jamii. Vitendo hivyo vidhibitiwe kisayansi na sio kwa vitisho.
Makala yako katika Tanzania Daima sijaikosa. Hongera mzee, nisalimie Ughaibuni.
Msangi,
Nimesoma habari katika Mwananchi Jumapili nikakumbuka mjadala uliouanzisha juma lililopita.
"majambazi yamtumia salamu Mwapachu...yafunga mtaa, yapora kweupee...ni wiki moja baada ya kuwatemea cheche!" ndicho kichwa cha habari kilichonistua. Yaani pamoja na kauli ya vitisho hivyo bado wanavamia mitaa? Hawaogopi? Hawakusikia? Kwa nini lakini?
Huo ni uthibitisho kuwa kuwatishia eti watauawa, ni kupoteza muda tu. Mheshimiwa Waziri atafute mbinu nyingine, hiyo aliyoanza nayo itaigharimu jamii. Vitendo hivyo vidhibitiwe kisayansi na sio kwa vitisho.
Makala yako katika Tanzania Daima sijaikosa. Hongera mzee, nisalimie Ughaibuni.