Thursday, February 16, 2006
MAHITA NA CHUO CHA POLISI ONTARIO
Katika muendelezo wa uchunguzi wangu kuhusiana na chuo cha polisi cha Ontario (pichani) na kivuli cha uhitimu wa mkuu wa jeshi la polisi Tanzania leo nimewasiliana na wahusika wa chuo hicho kwa njia ya simu.Kwa bahati mbaya sera zao za ubinafsi haziwaruhusu kutoa habari zozote za kitaaluma kumhusu mtu yeyote aliyewahi kuhitimu au kupitia kwenye madaraja na korido za chuo chao. bila ruhusa ya kimaandishi ya mhusika.Nikawa nimekwama.Ila nilichoweza kudadisi na kugundua ni kwamba chuo kinatoa certificates na diploma tu na kuna vyeti vya hata kozi za siku mbili ama tatu.Lakini uchunguzi bado unaendelea.Je kuna mtu anaweza kunisaidia na mwaka ambao mheshimiwa wetu alihudhuria chuo hiki?Kivumbi na jasho.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:20 PM
|
Permalink |
-
Jeff nazidi kushukuru jitihada hizi. Maana wasishangae watu tunatafuta taarifa za kuandika Orbituary si unajua waandishi tunazitunza kabisa kwenye Rpways kusubiri tu siku. Lakini tukikamilisha taarifa hizi lazima niruke naye huyu kwenye makala Bongo.
-
Jeff kwa kweli umepiga mzigo! kitendo cha kujua kua kuna kozi za siku mbili, certificate na diploma peke yake kimetengua ile kauli kuwa ni GRADUATE. sio kama nadharau chochote, kuna kina Mrema walisakata gozi vyema na diploma zao pia, lakini ukweli ubaki kuwa ukweli!
Jeff nazidi kushukuru jitihada hizi. Maana wasishangae watu tunatafuta taarifa za kuandika Orbituary si unajua waandishi tunazitunza kabisa kwenye Rpways kusubiri tu siku. Lakini tukikamilisha taarifa hizi lazima niruke naye huyu kwenye makala Bongo.