VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, February 15, 2006
NDESANJO NA .COM

Nimetoka kumuaga rasmi Ndesanjo kutoka kwenye uwanja wake wa kutumia tekinolojia ya blogger kwenda kwenye uwanja huru wa .com ambao kwa moyo wake wa upendo wa kuelimika na kuelimisha ametoa faranga kadhaa ili sote tuendelee kufaidi hazina ya fikra zake na uchambuzi wa masuala mbalimbali kwa urahisi na uhuru zaidi. Hii ni ishara ya mapendo. Ni ishara kama ile ambayo hunifanya nimsamehe Mwalimu Nyerere kwa kuitumbukiza Tanzania kwenye umasikini.Aliipenda Tanzania,akatupenda watanzania,akawa mwenye nia njema kabisa.Makosa yake yakawa ya kibinadamu.Mungu amlaze mahali pema peponi! Nadhani sote tunakubali kwamba nia ya Ndesanjo ni njema.Hana nia ya kutuacha solemba.Nimemuaga rasmi kwa kuitikia ombi lake la kubadili kiungo kile cha zamani kwenda hiki kipya.Binafsi naheshimu sana tafakuri za bwana Ndesanjo.Naheshimu tafakuri zake kwa sababu mara nyingi zinalenga katika ukombozi wa fikra.Hii ni vita ndefu pengine kuliko vita nyingine zote zinazotukabili wanadamu.Vita ya kufunua vyungu na mahandaki kusaka na kuutambua ukweli na kuutumia ukweli.Kwa bahati mbaya sana dunia imejaa uongo na unafiki mwingi sana.Ndio maana utaona zile semi za binadamu wote ni sawa zinakuwa kama mwangwi usio na mwisho.Mimi nasema binadamu wote sio sawa ila ni lazima wawe sawa.Hii ndio vita ya milele na milele. Mtembelee kwenye uwanja wake hapa kama bado hujafanya hivyo.Pichani juu ni ishara ya jinsi ambavyo Ndesanjo kakusanya vitu vyake na kuanza safari ya kuhama.Hongera Ndesanjo,aluta continua.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:31 AM | Permalink |


Maoni: 0


   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker