Wednesday, February 15, 2006
NDESANJO NA .COM
Nimetoka kumuaga rasmi Ndesanjo kutoka kwenye uwanja wake wa kutumia tekinolojia ya blogger kwenda kwenye uwanja huru wa .com ambao kwa moyo wake wa upendo wa kuelimika na kuelimisha ametoa faranga kadhaa ili sote tuendelee kufaidi hazina ya fikra zake na uchambuzi wa masuala mbalimbali kwa urahisi na uhuru zaidi. Hii ni ishara ya mapendo. Ni ishara kama ile ambayo hunifanya nimsamehe Mwalimu Nyerere kwa kuitumbukiza Tanzania kwenye umasikini.Aliipenda Tanzania,akatupenda watanzania,akawa mwenye nia njema kabisa.Makosa yake yakawa ya kibinadamu.Mungu amlaze mahali pema peponi! Nadhani sote tunakubali kwamba nia ya Ndesanjo ni njema.Hana nia ya kutuacha solemba.Nimemuaga rasmi kwa kuitikia ombi lake la kubadili kiungo kile cha zamani kwenda hiki kipya.Binafsi naheshimu sana tafakuri za bwana Ndesanjo.Naheshimu tafakuri zake kwa sababu mara nyingi zinalenga katika ukombozi wa fikra.Hii ni vita ndefu pengine kuliko vita nyingine zote zinazotukabili wanadamu.Vita ya kufunua vyungu na mahandaki kusaka na kuutambua ukweli na kuutumia ukweli.Kwa bahati mbaya sana dunia imejaa uongo na unafiki mwingi sana.Ndio maana utaona zile semi za binadamu wote ni sawa zinakuwa kama mwangwi usio na mwisho.Mimi nasema binadamu wote sio sawa ila ni lazima wawe sawa.Hii ndio vita ya milele na milele. Mtembelee kwenye uwanja wake hapa kama bado hujafanya hivyo.Pichani juu ni ishara ya jinsi ambavyo Ndesanjo kakusanya vitu vyake na kuanza safari ya kuhama.Hongera Ndesanjo,aluta continua.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:31 AM
|
Permalink |