VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Thursday, March 23, 2006
MAJENEZA YANAYOPAA!!

Mara nyingine huwa naota ndoto za usawa duniani. Nathubutu kuziita ndoto kwani ni wazi kabisa kwamba katika siku za maisha yangu dunia haitokaa isheherekee "usawa na haki" ambazo wengi tunazipigia mbinja kila kukicha. Lakini hili lisitukatishe tamaa kwani imani ni kwamba vizazi vitakavyofuata vitaweza kufaidi matunda ya vuguvugu tunalolianzisha hivi sasa.

Leo nimekutana na habari ambayo imenigusa kidogo. Imenigusa kwa sababu sio tu muathirika wake ni Afrika bali kwa sababu chembe chembe za "usawa hazipo. Habari yenyewe inahusu
kupigwa marufuku kwa baadhi ya ndege za abiria za Afrika kuruka na kutua katika nchi zilizopo kwenye Umoja wa Ulaya.

Nilipoisoma habari hii baada ya kuwa nimeisikia kwenye vyombo vingine vya habari kama televisheni mara moja nikakumbuka suala la uchakavu wa ndege za "Ulaya" zinazorandaranda katika bara la Afrika.Kama umewahi kusafiri kutokea Afrika kisha ukatua Ulaya kabla ya kubadilisha ndege kuelekea huku America ya Kaskazini ni wazi kabisa utakuwa umegundua kwamba ndege zinazofanya safari zake baina ya Ulaya na Afrika(za mashirika ya ndege ya Ulaya) ni za viwango vibovu kabisa ukilinganisha na zile unazopanda ili kuja Marekani au Canada. Hili wao hawalioni au wanadhani sisi hatulioni. KLM inayokutoa
Dar-es-salaam mpaka Uholanzi ni tofauti kabisa na inayokutoa Uholanzi kuja Toronto. Hali ni hiyo hiyo ukipanda British Airways,Swissair,Lufthansa nk. Rafiki yangu mmoja aliwahi kuziita majeneza yanayopaa. Kwa maana hiyo naushangaa umoja wa Ulaya unapoona viwango kwa macho ya makengeza (samahani).

Kwa maana hiyo nchi zetu za Kiafrika nazo ziwe na haki kabisa ya kupiga marufuku ndege hizi kuruka au kutua barani Afrika. Ni nani anazikagua za kwao? Mbona hata kwa macho tu zinaonekana kuwa majeneza yanayopaa??
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:59 AM | Permalink |


Maoni: 0


   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker