Tarehe: 9:45:00 PM, Mtoa Maoni:- John Mwaipopo
Tarehe: 1:38:00 AM, Mtoa Maoni:- boniphace
Jeff kweli umefungua fikra zangu. Sikupata kusoma kwa umakini majina hayo kwani mimi target yangu ilikuwa kutaka kuthibitisha kuwa wahusika wa ujambazi kweli ni CUF na hapa Tibaigana anaungana na jambazi mwenzake mAHITA. Anataka kutuonyesha kuwa TEMEKE na huko uswahilini ndiko kitovu cha wizi na huko wanaketi wana CUF. Fikiri kwa kina kuna ajenda ya siri katika majina hayo lakini naamini majambazi wa kwanza kabisa ni maRPC WALIOGAWANYWA
Tarehe: 1:45:00 AM, Mtoa Maoni:- boniphace
Mikoa mbalimbali. Jeff ni haya haya ya rushwa na hongo. Mwizi wa kuku anashikishwa pesa za moto za PCB au hakimu wa mahakama ya mwanzo. Vipi kuhusu mikataba feki inayoghalimu fedha nyingi za umma. Tazama tena suala hili la ujambazi, hao wanashikwa hawana uhusiano moja kwa moja na kumiliki silaha, kutambua kama kuna fedha mabenki na inawezekana wasifanane na kuyajua magari. Vipi hapa polisi wetu, mbona wanaonyesha wasiwasi mapema hivi! Tutapata ushahidi kuwa hao wanahusika lakini nani anawapa silaha kama kweli wanahusika? Je watanzania tunahitaji anayetumwa kuiba au huyu anayetuma kuua ili apate anachiokitaka! IPO KAZI LAKINI SAFARI LAZIMA IENDELEE.
Tarehe: 8:24:00 AM, Mtoa Maoni:- mwandani
Si utani, hivi karibuni kuna washikaji zangu naona wametinga kwenye magazeti kama majambazi tena waliopiga watu risasi. Nilijiuliza sana inakuwaje? Tumekua sote, tumecheza chandimu sote, inakuwaje mtu anafikia hali ya kutumia silaha kwa ujambazi? Na hao washikaji naowazungumzia walikuwa ni watu wenye nafasi nzuri tu, usingeweza kujua kama wana dhiki yoyote ya mali kuwafanya waingie ujambazi.
Haidhuru, kuna makala nimeiona inayowataja wanaoshukiwa ujambazi.
Nukuu:
"Kutokana na kasi ya kusafishwa kwa jeshi hilo, vigogo mbalimbali hivi sasa wameonekana kubanwa mavazi yao kwa hofu ya kuibuliwa na kuunganishwa katika sakata la mtandao wa ujambazi.
Licha ya habari ambazo gazeti hili imezipata kuhusu RPC mmoja wa mikoa ya Kaskazini ana akauti yenye zaidi ya sh. milioni 200, akaunti hiyo imezuiwa naye kuzirai."
Fuata kiuongo hiki:
http://www.ippmedia.com/ipp/alasiri/2006/03/09/61705.html
Majambazi wako kila mahala, haswa kwenye wale wenye nafasi.
Tarehe: 9:49:00 PM, Mtoa Maoni:-
Mwandani, kiungo ulichotoa huenda kimekatika maana hakifunguki. Wakati mwingine viungo virefu huwa vinakatika baada ya kubonyeza "tuma." Kwenye mwongozo wa blogu pale nimeandika jinsi ya kufupisha viungo virefu kwa kutumia huduma ya jamaa wa: http://www/tinyurl.com
Hivi Msangi, huyu Massawe ni yule mwenye hoteli kariakoo na pia aliyewahi kuwa "mfadhili" wa timu yako ya Yanga?
Tarehe: 8:20:00 AM, Mtoa Maoni:- FOSEWERD Initiatives
duh kweli prez Jakaya si mchezo! yaani majina kutoka naye akayashukia kama mwewe kuwa list haitoshi! kweli watumishi wa serekali wanafundwa kuwa watumishi wa umma sasa hivi!!
hawa vijana wenye miaka 19 ambao wanakuwa majambawazi ni wale watoto waliokosa kuendelea na ekimu ya sekondari miaka mitano iliyopita kisa hakuna "madarasa"! walioweka hii mifumo walijua maana yake!
Tarehe: 12:35:00 PM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Urewedi jeff,
Hao waliowataja ukiona hivyo hawakugawa-ga 'mauzo'.
Kilichonitisha ni kuwa kumbe majambazi makuu wamejificha katika 'wafanyabiashara'. Tuna kazi kubwa sana ya kufanya Bongo irejee katika amani ya awali.
Hili mimi nilikuwa nalifahamu zamani. Kwa mfano kule mbeya hawa 'bisnesmeni' wako kibao na tunawatambua. Ujahili wao ni kuteka magari ya safari ndefu halafu asubuhi unamkuta anafungua duka lake kama kawa.'Hatuwasemi tunaogopa mkong'oto'
Prez Jakaya amesema hiyo list ni fupi mno. Kumbe anawafehemu. Na tusubiti tuone list hiyo anayoijua Prez Jakaya. Pia haitoshi list tu. We want to see justice not only done but also, and most importantly, seen to be done.
Yasije yakawa tunastaajabu ya filauni, je tukiona ya Musa.