VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Thursday, March 16, 2006
UNAKUMBUKA??

Sitaki kuingilia kazi ya Michuzi ila picha hii ni mojawapo ya picha zinazonivutia sana. Pia picha kama hii huwa inakumbusha mengi. Nadhani hii picha ni tamu na chungu kwa tulio ughaibuni. Hivi unakumbuka siku ulipokuwa unaondoka nchini kwako mara ya kwanza kabisa? Ukiona picha kama hii unakumbuka kisanga chochote? Hebu tupige stori jamani! Wale walinzi walikuambia nini?Wale maafisa wa immigration walikupa lile jicho lao "suspect? Tizama hiyo picha halafu click ili uikuze zaidi uione kwa karibu ili uvute kumbukumbu zako.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 4:00 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 8:05:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Jeff shida yangu ni jina hilo, hivi hakuna uwezo wa kujenga viwanja vingine vikapewa hilo jina. Kuna haja gani kila siku kuwa tunabadili majina. Tena kuna haka kanaitwa Mwalimu Nyerere Foundation kanakoongozwa na mgombea urais ambaye aliwahi pia kuwa Katibu Afrika na Barozi wa Tanzania achilia mbali Waziri Mkuu na Mwenyekiti wa MSI na vingine sijui... hivi wameshindwa kukaa na kuibuka na wazo la ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere ambacho sambamba na masuala mengine kitahusika kutoa taaluma ya Conflict Resolusion na masuala kama African Studies na Kilimo. Ee bwana hivi, ok nirudi hapo Ea port. Kuna washenzi fulani wanapokuona unakatiza mtoni wanadhani umeshaula, wanataka kukuomba virushwa hapo. Nikiingia hapo rushwa ngo hampati hata mfanyeje, sitoi wala sipokei na tena nadhani itabidi kubadili kushukia uwanja wa Arusha kabisa maana Bongo hapo Majambazi kibao.

     
  • Tarehe: 1:30:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger John Mwaipopo

    Kumbu kumbu yangu sio hasa hapo mbele ya Uwanja bali kule mbali kwa nyuma kuelekea Kiwanda cha pepsi siku nilipozidisha 'juisi ya maembe' na kupotea njia. Thank God usiku huo ulikuwa Christmas eve hivyo hakukua na vibaka kwa hofu ya doria. Bahati njema sikukutana hata na polisi.

     
  • Tarehe: 9:31:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Kuna wimbo wa Ziggy Marley unaitwa Dream of Home. Sasa picha kama hizi ndio huleta alichoimba Ziggy Marley. Picha zina namna yake ya kusema mengi bila maneno mengi. Ndio maana kuna msemo wa "picha moja ni zaidi ya maneno elfu moja."

    Kuna swali umeuliza kuhusu ukimwi kutumaliza sisi. Nitachangia. Najua Nkya wa Pambazuko amekuwa akifuatilia masuala haya kwa muda mrefu na kwa kina.

     
  • Tarehe: 12:41:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger MICHUZI BLOG

    mie unanikumbusha mwaka 1992 nikiwa natoka berlin na tv aina ya grunding na dola kama mia 400. nikawa natoka jasho nitapitaje nayo tv na dola 400 nikii-declare ina maana nitauza bei ya benki na sio pale empress.

    kwa bahati jamaa wa forodha walikuwa bize kuitathmini tv yangu na kusahau kunipekua, hivyo 400 zangu nikasevu.

    ila tv nilii-declare na kupewa fomu kujaza na hatimaye huko mjini nikaenda kuitafutia kadi kama ya gari tra ya enzi hizo. kadi hiyo ya tv, ambayo umbo na rangi (binzari) ni sawa na ya gari, nnayo hadi leo. ila wakati napiga picha hii sikuwaza hayo hadi makene ulipouliza

     
  • Tarehe: 2:08:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jaduong Metty

    Jeff,

    Siku naondoka (najaribu kutoelezea jinsi moyo ulivyokuwa unanidunda) jamaa wa uhamiaji aliniomba nitoe vitu vyote kwenye "woleti" yangu. Kuona nina vidola vichache nilivyopewa na mfadhili wangu, jamaa si akanibomu? Nikatoa nje, nikamtonya kwamba niendako simjui mtu na hivyo visenti ndo vitanifadhili.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker