Tarehe: 8:05:00 PM, Mtoa Maoni:- boniphace
Tarehe: 1:30:00 AM, Mtoa Maoni:- John Mwaipopo
Tarehe: 9:31:00 AM, Mtoa Maoni:-
Kuna wimbo wa Ziggy Marley unaitwa Dream of Home. Sasa picha kama hizi ndio huleta alichoimba Ziggy Marley. Picha zina namna yake ya kusema mengi bila maneno mengi. Ndio maana kuna msemo wa "picha moja ni zaidi ya maneno elfu moja."
Kuna swali umeuliza kuhusu ukimwi kutumaliza sisi. Nitachangia. Najua Nkya wa Pambazuko amekuwa akifuatilia masuala haya kwa muda mrefu na kwa kina.
Tarehe: 12:41:00 PM, Mtoa Maoni:- MICHUZI BLOG
mie unanikumbusha mwaka 1992 nikiwa natoka berlin na tv aina ya grunding na dola kama mia 400. nikawa natoka jasho nitapitaje nayo tv na dola 400 nikii-declare ina maana nitauza bei ya benki na sio pale empress.
kwa bahati jamaa wa forodha walikuwa bize kuitathmini tv yangu na kusahau kunipekua, hivyo 400 zangu nikasevu.
ila tv nilii-declare na kupewa fomu kujaza na hatimaye huko mjini nikaenda kuitafutia kadi kama ya gari tra ya enzi hizo. kadi hiyo ya tv, ambayo umbo na rangi (binzari) ni sawa na ya gari, nnayo hadi leo. ila wakati napiga picha hii sikuwaza hayo hadi makene ulipouliza
Tarehe: 2:08:00 PM, Mtoa Maoni:- Jaduong Metty
Jeff,
Siku naondoka (najaribu kutoelezea jinsi moyo ulivyokuwa unanidunda) jamaa wa uhamiaji aliniomba nitoe vitu vyote kwenye "woleti" yangu. Kuona nina vidola vichache nilivyopewa na mfadhili wangu, jamaa si akanibomu? Nikatoa nje, nikamtonya kwamba niendako simjui mtu na hivyo visenti ndo vitanifadhili.
Jeff shida yangu ni jina hilo, hivi hakuna uwezo wa kujenga viwanja vingine vikapewa hilo jina. Kuna haja gani kila siku kuwa tunabadili majina. Tena kuna haka kanaitwa Mwalimu Nyerere Foundation kanakoongozwa na mgombea urais ambaye aliwahi pia kuwa Katibu Afrika na Barozi wa Tanzania achilia mbali Waziri Mkuu na Mwenyekiti wa MSI na vingine sijui... hivi wameshindwa kukaa na kuibuka na wazo la ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere ambacho sambamba na masuala mengine kitahusika kutoa taaluma ya Conflict Resolusion na masuala kama African Studies na Kilimo. Ee bwana hivi, ok nirudi hapo Ea port. Kuna washenzi fulani wanapokuona unakatiza mtoni wanadhani umeshaula, wanataka kukuomba virushwa hapo. Nikiingia hapo rushwa ngo hampati hata mfanyeje, sitoi wala sipokei na tena nadhani itabidi kubadili kushukia uwanja wa Arusha kabisa maana Bongo hapo Majambazi kibao.