VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, March 10, 2006
WAPI TUNAELEKEA?

Wiki chache zilizopita Michuzi alituwekea picha hii hapa.Nia ilikuwa ni kutuonyesha watoto wakiburudika na kufurahia maisha. Nakumbuka baada ya kuiona picha hiyo nilionya juu ya michezo tunayowaruhusu watoto wetu wacheze bila kusahau sinema tunazowaonyesha au kuruhusu tu kiholela waangalie bila kujali madhara tunayotengeneza kwenye akili zao. Kero yangu kubwa imekuwa jinsi ambavyo watu wengi wanachanganya maana ya maendeleo na jinsi tunavyotengeza taifa la kesho lenye mtindio mbaya kabisa wa akili.

Kuwaonyesha watoto wetu sinema za kihuni,uvutaji bangi,umalaya,kuwanunulia matoy ya bunduki nk ndio eti tunayaona ni maendeleo. Siku zinavyopita tunazidi kutupilia mbali tamaduni,mila na desturi zetu za asili, tunavyozidi kuuona na kuwaambia watoto zetu kwamba ni wa kizamani,haufai na sio wa kimaendeleo.Hili hunikatisha sana tamaa.Nakuwa naona kiza kikubwa mbele yangu kila niliwazapo taifa letu lijalo ambalo ndio tegemezi letu kubwa.

Katika pitia pitia yangu ya magazeti ya nyumbani hivi leo nimekutana na mkasa wa ulionisikitisha sana na ambao kwa kiasi kikubwa unabeba ninachojaribu kukiongelea hapa.
Mkasa wenyewe huu hapa. Tafadhali usome kwanza kisha uniambie je haya sio madhara ya wazi kabisa ya "maendeleo" ninayoyapinga mimi.Huoni kwamba si ajabu huyu mwanamke/mdada wa miaka 20 alidhani pengine anafanya kama anachokiona kwenye "Days of our lives" tu? Nani alimruhusu binti huyo mdogo awe na kitu cha moto kama bastola?Huu ndio uzazi jamani? Tunakoelekea ni wapi??

Kwa bahati mbaya hii familia iliyofanya haya ina jina sawa na mwanablogu mwenzetu Mark Msaki! Samahani Mark unamfahamu Msaki huyu ambaye binti yake amefanya dhahama hii?
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 3:33 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 1:45:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger John Mwaipopo

    Kwanza nampa pole yule mtoto wa shule ya msigi aliyesasambuliwa makalio. Mchezo aliokuwa akicheza, mpira, ndio hasa inayowafaa watoto. Wengine tulikosa mwelekeo wa michezo chanya hii kwa u-endelevu.

    Pili ni ulimbukeni. yafaa nini kuizagaza bastola pahala popote katika nyumba yako. Ona imesababisha binti kugeza vizungu na kumsasambua kijana. Ama ilikuwa kaiba chumbani kwa baba yake ama huachiwa pale 'aliliapo'. Si unajua kudeka.

    La tatu: yawezekana hatujajiandaa na ujio wa sinema kule Bongo. Huku nchi zilizoendelea, pamoja na ujinga wote huu kufanyika, wazazi wengi ni makini katika kujua nini watoto wanastahiki kuona na nini hawastahiki. Wamefikia hata hatua ya kuweza kuitawala TV kwa teknolojia. Yafaa tutambulishe vifaa hivi na mwamko huu Bongo.

    Nne: nalo ni ulimbukeni. Kumbuka Tanzania tumechelewa sana kujua TV ni nini. "Hii maneno" imetufanya tuwe mbumbumbu wa kuchambua mema na mabaya ya teknolojia hii. Kilichokuwa ni kuwa ilipoletwa tulikuwa sasa 'tumepumua.' Lijalo na lije bila censorship ya aina yoyote kutoka serikalini hata majumbani mwetu. Hebu fikiria pale ulipokuwa na njaa kwa muda mrefu halafu ghafla waletewa chakula. Nahisi utafakamia halafu utavimbiwa.

    Changamoto yangu hapa ni kuwa midhali Video Industry imeanza kupata wasaa Bongo, ni wasaa sasa tuwe na wataalamu wa kutengeneza filamu za kuwafaa watoto. Mathalani ni wasaa sasa kuweka katika filamu zile hadithi za jumamosi RTD za Mama na Mwana. Kilichopo sasa watu woote watoto wa wakubwa wanashabikia filamu zile zile za kikubwa mfano ile iliyotoka mwaka 2003 iliyoitwa girlfriend. Watengenezaji wa filamu Bongo watengeneze filamu za kuwafaa watoto na watu wazima tukumbushane umuhimu wa kulea maadili ya kibongo.

     
  • Tarehe: 5:02:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger FOSEWERD Initiatives

    Jeff, habari hii niliisoma jana na nilipata masikitiko makubwa kusoma lile jina lililohusika kuwa yule dada likuwa ni binti wa Mzee Msaki! kwa kweli hadi sasa sijamfahamu ila nitafanya uchunguzi nipate kumfahamu..maana habari yenyewe haikimfafanua sana!

    ila kwa kweli, nikiwa naanda chai yangu asubuhi leo nikawa ninawaza na kuwazua (maana na mie nina kijana matata kweli kwa michezo huyo)...kuwa ina maana hizi silaha unapomilikishwa si kuna masharti? lazima iwekwe ndani ya Safe, halafu hata ukisafiri nje ya eneo, lazima uikabidhi kwa polisi, ukirudi unaichukua, basi hata kama ni ya yule binti, lakini ana miaka 20 tu je ni kweli alimilikishwa silaha?

    nikawaza tena, maana watoto ni watoto tu, mtoto hana mpaka, mtoto hulelewa na jamii, nikajiweka kwenye nafasi ya mtoto yule ambaye aliianza siku kwa amani na furaha, pengine kwa uji uliomchengua vibaya sana hasa kwa kiwango cha maziwa ya unga, sukari na blu bendi! akapiga mpira, ukaenda paani, akaufuata akaona cha moto akakimbia (pengine asingekimbia angepigwa kifuani akafa)mtoto yule alipoona hali ngumu akakimbilia ndani na kujificha mathalani chini ya meza.....akamkabidhi mungu maisha yake....akasikia moto unapenya matakoni.....kwa kweli nilijisikia vibaya sana... mbona inaonekana kabisa mtoto huyu alikuwa kwenye mazingira ya kukamatika??

    kwa kweli, hii hadithi mimi ilinisononesha sana. tena wala sio kidogo. kwa kweli kuna haja ya kufanyia kazi hizi taratibu za kupiga risasi na kuzoea bunduki...au la ndio usugu unaojengeka sasa kutokana na picha za holiwudi zinazochezwa kweupe mchana mchana bongo?

     
  • Tarehe: 11:37:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Jeff hapa umenikumbusha tena kurushiana risasi kulikofanyika Toronto na kuua yule binti mrembo mchanga kabisa aliyekuwa mpita njia. Sasa tazama hapa haya ymetokea Bongo vipi mzee wa Kasri ningekuwa nakatiza mitaa hiyo na kukumbwa na sereka hilo ina maana ndio ningekuwa nimehamishia Gazeti Tando langu kuzimu?

     
  • Tarehe: 12:08:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Mwaipopo,
    Umeweka maoni ya msingi sana ndugu yangu.Umenifanya nikajiuliza hivi zile sinema kama Girlfriend na nyingine tele zilizofuatia ni PG,PG14,Rated au namna gani?Kuna umuhimu wa kuanza mapema kutengeneza sheria zetu za burudani upya.
    Mark,
    Watoto lazima sisi ndio tuwe walinzi wao namba moja.Huyo kijana wako anayependa kuchezea madude haya mkanye mapema.
    Makene,
    Hata mimi nilikumbuka kabisa tukio lile la Toronto.Kilichonisikitisha ni kwamba niliwahi kujitamba kwamba matukio kama yale nchini Tanzania ni nadra sana,nilikosea kumbe!naona aibu.

     
  • Tarehe: 11:41:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger FOSEWERD Initiatives

    Jeff ni kweli, mwanangu sio mchezeaji wa bunduki, ni mpenda michezo sana...nilimweka kwenye nafasi ya mtoto aliyekuwa anapiga mpira!! halafu siku hizi kuna machezo ya kuchezea kwa kompyuta.. si mnayajua? unaweza kuendesha gari au kupiga bunduki...au kwa kweli tuwe waangalifu!

    hoja ya mwaipopo ni imara sana. nadhani kuna haja kuweka vigezo katika sanaa.. lakini na huu utandawizi si mipaka haipoo siku hizi?

    leo nilikwenda kwenye duka la bunduki hapa SA. nikakuta bunduki, na niliulizia bastola nikaonyeshwa nyingi tu revolver ambayo ni bei rahisi kabisa ni rand 1500...ziko bastola mpaka za rand 7000.. nikaulizia masharti ya umiliki na utumiaji, kwa kweli SA wameweka sheria NGUMU SANA!!! of course lazima ukafundishwe kulenga siku 5, halafu upewe certificate of competence, na upate kibali toka Pretoria!!

    kumiliki si hoja, hoja ni kuitumia sasa!! sasa hivi SA ukiwa na bunduki, hata ukampiga mwizi, unapanda kizimbani...ni kesi ya kujibu, na wakati huo ina maana huwezi ukapiga mungine! kupewa lazima falilia yako ikubali kuwa ni sahihi na familia nyengine 2 za karibu .....hivyo ni rahisi mtu mwenye bunduki isiyosajiliwa (e.g mwizi kupiga bunduki kuliko iliyosajiliwa) - sasa hivi wanasema watu wameamua kununua bunduki za kupiga ndege, ili ukivamiwa unapiga juu, wezi wanaogopa wanakimbia, lakini kama wamedhamiria hakuna msaada!! - wenye maduka ya bunduki wanakiri kuwa biashara inadodo sasa hivi...

    nadhani hata sisi umefika muda tuangalie sheria zetu sasa na haswa lile duka la bunduki....sioni ni nini motivation ya lile duka kuwepo...wenzetu wanaziondoa kwenye circulation sie tunaziongeza

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker