Tarehe: 4:33:00 PM, Mtoa Maoni:- John Mwaipopo
Tarehe: 6:15:00 PM, Mtoa Maoni:- boniphace
Tarehe: 8:19:00 AM, Mtoa Maoni:-
Tena Jeff hapa umenikumbusha jambo muhimu sana katika historia ya mababu zetu, tukizingatia wakati ule wa vita ya kwanza ya dunia, hivi kweli mababu zetu walirejea wote kutoka kule Burma na maeneo kama hayo enewei nitapita tena kuchota taarifa hii ni muhimu sana katika historia ya weusi.
Hii ndiyo inadhihirisha nguvu ya mawasiliano ya umma kama anavyosema Mwaipopo hii rangi nyeusi ni lazima sasa isaidiane si tunawaona hawa wenzetu weupe wanavyosaidiana.
Jamaa yangu mmoja amenichekesha aliposema weusi noma ndiyo maana tukisugua ngozi zetu halafu tukanusa inanuka mavi ya kuku.(joke)
Tarehe: 4:29:00 AM, Mtoa Maoni:-
Hapo Jeff umetugusa wengi sana!Nikiriria jinsi waafrika au watu weusi walivyotawanywa duniani kwa kweli inauma!Hii habari ya India ni nyeti sana kwani mara nyingi tumezoa kusikia wamarekani weusi au Afro-american lakini hatukuwahi kabisa kusikia weusi waliopelekwa India na Uarabuni!Kama navyosema Mwaipopo sisi wenye ngozi nyeusi inabidi tusaidiane sana!
hii makala nzuri sana bado naendelea kuimeza!
Tarehe: 6:57:00 AM, Mtoa Maoni:-
Utafiti umefanyika wa kina kuhusu Waafrika waliosambaa dunia nzim. Kuna vitabu kama African Presence in Early Europe, They Came Before Columbus (African Presence in Ancient America), African Presence in Early America, n.k. Ukiachilia ndugu Runoko, mwingine ambaye amechimba sana haya mambo ni Dk. Ivan Van Sertima (ambaye amewahi kufanya kazi kule Morogoro).
Historia hizi huwa hatufundishwi mashuleni. Tunafundishwa historia kwa mujibu wa wazungu na sio kwa mujibu wetu.
Sijui kama mnawafahamu ndugu zetu kule India wanaoitwa Sidis ambao walitoka Afrika Mashariki na hadi leo wana mambo mengi ya kitamaduni (vyakula, ngoma, majina, hadithi, n.k.) vinavyoendana na tamaduni za Afrika Mashariki.
Labda niongeze pia kuwa mto Ganges unatokana na jina la jemedari wa Kihabeshi (Ethiopia). Kama ilivyo jila "Europe" linatokana na malikia wa Kiafrika.
Jeff, masomo haya nadhani inabidi tuongeze bidii kuandika maana tusipoandika sisi na kufunza wadogo zetu nani ataandika?
Shukrani zikujie.
Hii inabidi niirejee baadaye. Umefika wakati sasa sisi wenye rangi mbaya tusaidiane wenyewe kwa wenyewe maana hatuna mjomba wa kutusaidia kokote kule.