VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Tuesday, April 04, 2006
ENZI ZILEEE.....

Kuna nyakati huwa nazikumbuka sana enzi zile za kushinda vijiweni na kwenye vigenge vya hapa na pale tukidanganyana na kuuziana nyeti zisizokuwa na unyeti wowote.Enzi zile ambapo tulikuwa tukikutana "maskani" tukapigishana stori juu ya raha ya kupata msuba na jinsi unavyoweza kukuliwaza kutokana na mawazo uliyonayo ya kukosa kazi. Unajua Tanzania imekuwa na recession ya kudumu kwa muda mrefu sana na ndio maana vijiwe havikauki. Bado nakumbuka jinsi tulivyokuwa tukipanga madili na kuweka mezani kabisa jinsi tutakavyogawana mapato. Tukapigishana hadithi za kununua Mercedez Benz Convertible wakati hata baiskeli ya miguu mitatu hatuna!

Lakini kali zaidi ni lile la baadhi ya "wajuaji" walivyokuwa wakipakaza na kueneza "ukweli" wa wakati huo kwamba eti yule mwanamuziki wa Marekani aliyekuwa anaitwa Marvin Gaye alichapwa risasi(aliuawa) na baba yake mzazi kwa sababu alikuwa msenge. Hukuwahi kusikia hivyo wewe?Basi kijiwe chenu kilikuwa hakina mabingwa wa kuleta hadithi za Ulaya na Marekani. Hizo ni zile enzi ambazo njia pekee ya kwenda "mamtoni"ilikuwa kuzamia meli,potelea mbali yanayoweza kukukumba mbele ya safari. Enzi zile wafagizi na wapishi katika meli za nje wanaotokea mitaani kwetu tuliwabatiza "zungu la unga".

Unajua kama hadithi/kashfa ile ya Marvin Gaye ilitungwa ili kila mtu aogope ushoga kama ukoma basi ilifanikiwa sana.Kampeni za namna ile naweza nikaziunga mkono.Najua hata wewe unazo hadithi/visa kutoka maskani kwenu. Kwanini basi tusikumbushane hapa kwenye blogu? Hebu tukumbushane ENZI ZILE.....
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 1:33 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 11:53:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger MICHUZI BLOG

    enzi nzikumbukazo mimi ni za akina dj (marehemu) kalikali na neagre jay pale ymca , dj john peter pantelakisna dj (marehemu) choggy sly kule silversands, dj gerry kotto na dj seydou mbowe na dj emperor (huyu joseph kusaga bosi wa clouds fm) akiwa motel agip.

    enzi hizo sexual healing ya mavingei ilikuwa balaa kama zilivyokuwa dont stop til yu geti inafu ya maikojackson. mtindo tawala enzi hizo ulikuwa break dance na nakumbuka wimbo wa 'u cant stop us now, dancing' sie tulikuwa tunaimba: maiko jekson njoo, sitaki...kama hutaki nenda...

     
  • Tarehe: 8:14:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Kumbe Choggy keshatutoka! huku kupitwa na wakati kubaya. Mungu amrehemu.
    Hata mimi nilisikia hicho kisa cha Mavingei.
    Kikao kwenye gogo vivu mjomba magirini ndio yalikuwa yakitawala, kila mtu alikuwa na filingi za kujimbinjua. kitu kibaya zaidi kilikuwa kuwazikiliza wale masela pale lebanoni (magogoni), wakitoa stori za bichi la siria, bichi la misri, na mitemba ya manta laini, mo mac momack... Magirini ya kuzamia na kujificha kwenye hachi za meli, jinsi ya kuongea na kapteni akupe u-deki boi...
    nilikkuwa naijua meli na namba za hachi hata bila kuikwea hiyo meli.
    Mambo ya kijiweni hayajakwisha hivi karibuni tu pale bichi la Bombay niliwaona watoto wa kibongo wanapiga stori kama hizo, na wanafanya mabo kama yale ya stori za vijiweni, kuna yanki nilikutana naye ndio kwanza atoke bongo baada ya kuwekwa mazabe New jersey, akadanganya kuwa yeye ni muavori kosti, walipomshusha uwanja wa ndege kulikuwa na machafuko ilibidi aililie bongo, kufika nairobi akatoa kitu kidogo mara tu akajimbinjua bombay tulipokutana.
    Recession, vijiwe vipo mpaka leo ndugu yangu.

     
  • Tarehe: 8:24:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    MASELA KIJIWENI

    Ali Master: Ndiyo babu yangu!
    Hapo mitaa ya Instambuli hapo. Hapo babu yangu makabalee mpaka asubuhi. Humo mitoto ya Kimanga, Kizungu, inacheza na bikini tu. Likikuzimia linakufuata lenyewe " yu wanti go endi mi?" Usipapatikie maanake inaweza kuja zali nyingine hevi zaidi we unampa " Ai teli afta taimu"

    Paulo Mtanga: Aaah hiyo mitoto ya kimtoni wala haimaindi atakuambia tu "no sweti, ai weiti yu" Hapo Istambuli siyo poti mchezo. Hapo kila kitu; drai poti, auti anka, taneli kila kitu maanake. Meli zinaingia poti kwa trafiki laiti kama magari yanavyovuka daraja la Kajima. Siyo mchezo poti liko openi twenti foo awazi.

    Ali Master: Huko wiki moja mtu unatuna, moningi unapata uji uliopikwa kwa unga wa keki halafu umetiwa mapande ya siagi. Lanchi unakula poki na viazi vya kuponda, saladi, glasi ya maziwa. Jioni unapata bifu la kukaanga tena ile mipande hevi (anaonyesha kipimo cha kiganja cha mkono wake) na chipsi pembeni juisi.

    Paulo Mtanga: Wiki!? Hiyo menyu siku mbili tu unaumuka, mashavu utafikiri unapuliza moto! Ukijiangalia kwenye kioo wewe mwenyewe hujitambui. Hilo menu Bongo mawaziri hawaipati, fanya mchezo nini?

    Ali Master: Subutuuu! Hiyo misosi iliyopimwa na imepikwa na shefu aliyesomea kwa madigrii ya upishi. Mawaziri menyu kama hiyo wanaiskia kwenye bomba. Chakula unapikiwa na boi katoka shamba. Ukurutu kibao mikononi. Akisonga ugali matone ya jasho yanatiririkia ndani ya sufuria. Nyumba nzima kipindupindu. Kwani unafikiri Ostabei hamna kipindupindu? Dooo, basi huko ndiyo kipindupindu ndiyo kwao lakini wanafanya siri.

    Mshikaji mwingine yuko bangi nyingiii anasikiliza kwa makini.Ghadhabu za kujikata zinamwingia kama homa ya malaria. Inamtoka " No sweti safari lazima.Sasa hivi nikimalizia misheni yangu fulani nachukua simeni buku. Mkoba n'nao, vasinesheni kadi nayo n'nayo. Nasubiri Selebresheni an'tumie kidogodogo toka Kopenihajeni. Nikamilishe dokumenti zote niingie Beira au Msa.."

    Ali Master: Kwa nini usipige bboda la Sudani? Sasa hivi Beira na Msa vyuma havikamatiki. Chawa (Stolowei) wengi ile mbaya. Meli ikitoka poti inaingia auti anka siku tatu hata wiki kuanika chawa! Jamani mchango wa lanchi.

    Wanachangachanga wanapata pesa ya kutosha kula kodrai kwa mama n'tilie(ukoko wa chini wa wali)Wanaondoka kijiweni kwenda kula kodrai.

    F MtiMkubwa Tungaraza.

     
  • Tarehe: 11:58:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Tungaraza,
    Hii kumbukumbu ya aina yake..duh...hapa nilipo nimecheka mpaka jino la omega.

     
  • Tarehe: 1:58:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger John Mwaipopo

    Hii sikuisoma ni balaa. Haswa michango ya akina Michuzi, mwandani na Mti Mkubwa mwenyewe. Watu wazima hao walisemalo lilikuwapo. Mie wantia raha. Hiyo ya Michuzi ya "maiko jekson njoo, sitaki...kama hutaki nenda..." imeniacha kinomi. Tulizikuta hizi zikimalizikia malizikia. Old is gold hakika.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker