Tarehe: 5:37:00 AM, Mtoa Maoni:- Reggy's
Tarehe: 12:07:00 PM, Mtoa Maoni:- mzee wa mshitu
Jeff na Reginald
Msisahau kuwa Tanzania ni ule pale askari Monument ambao kuna askari kama yule wa kule Moshi ambapo tunaelezwa ndugu zake Msangi wa kutoka pale Kisumundu walikuwa wakitupa mikungu ya ndizi na kukimbia zao.
Hebu angalieni wenzetu wanavyotukuza vyao haishangazi kwamba siku moja ile minara ya pale Mnazi mmoja (wa uhuru) na mingineyo kukuta imebomolewa halafu kikasimikwa kitu cha ajabu ajabu.
Tarehe: 7:39:00 PM, Mtoa Maoni:- John Mwaipopo
Tarehe: 7:52:00 AM, Mtoa Maoni:- MICHUZI BLOG
john umenikumbusha warsha ya bagamoyo ya wadau wa muziki ambao mojawapo ya maazimio ni kuzindua 'orofea' zilizokuwepo kila wialaya kwa ajili ya kutumiwa na jamii ya mahali husika kama vile muziki, kwaya, maigizo n.k. nakumbuka pale tukuyu siku ya sikukuu jamaa alikuwa-ga anapiga ngoma na filimbi orofea ya polisilaini, na kutuchaji thumni kiingilio.
sasa hii minara yote iliyoko dar na kwingineko, mingi ni ya mkioloni, ukiondoa wa saa dar, na wa azimio la arusha arusha, na sijui wapi. jeff asante kwa habari na picha. nadhani umeng'amua kuwa mineno mitupu nayo ikizidi inaboaga. hongera sana, nadhani wengine wataiga mfano, hasa we mwaipopo.
Tarehe: 1:02:00 PM, Mtoa Maoni:-
Hii habari ya minara kuna wakati nilikuwa nafuatilia sana. Kwanini binadamu tunapenda minara? Je kuna uhusiano wa upenzi wetu wa minara na ile hadithi ya wayahudi ya mnara wa babeli? Nyumba za wachagga za asili, ingawa hazina mnara, umbo lake, pale kwenye paa, liko kama mnara. Makanisani unakuta minara. Misikiti unakuta minara. Majengo ya bunge unakuta minara. Makumbusho ya kitaifa katika nchi mbalimbali yanatumia minara.
Asante kwa picha, Jeff!
Tarehe: 9:03:00 AM, Mtoa Maoni:- Christian Bwaya
Asante Jeff, kwa taarifa za kina juu ya minara ya duania. Umenikumbusha mnara wa uhuru pale mnazi mmoja Dar na ule wa Arusha, nashindwa hata kufananisha.