
Ukitembelea Paris- Ufaransa ni wazi kwamba utapenda kutembelea na hata kupiga picha kwenye mnara ujulikanao kama Eiffel(Eiffel Tower) .Ukifanya safari za jiji la New York si ajabu ukapenda kwenda kushuhudia ule mnara wa uhuru(Statue of Liberty). Vile vile ukitembelea jiji la Toronto,hapa Canada nina uhakika utapenda kuutembelea huu mnara ujulikanao kama CN (CN Tower) (pichani). Inasemekana kwamba huu ndio mnara mrefu kupita yote duniani ambao umesimama dede. Uliwahi pia mnamo mwaka 1995 kuingizwa katika yale maajabu saba ya kisasa ya dunia.Unaweza kusoma zaidi juu ya mnara huu hapa.
Majuzi nimesikia kwamba huko Chicago-Marekani na Tokyo-Japana inajengwa minara ambayo huenda mmojawao ukachukua nafasi ya CN Tower ambao ndio sahihi ya jiji la Toronto.Nilipiga picha hii wikiendi iliyopita.
Asante Jeff, kwa taarifa za kina juu ya minara ya duania. Umenikumbusha mnara wa uhuru pale mnazi mmoja Dar na ule wa Arusha, nashindwa hata kufananisha.