Tarehe: 7:17:00 AM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 8:44:00 AM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Tarehe: 9:09:00 AM, Mtoa Maoni:- Christian Bwaya
Maandiko haya nimeyahusisha na kile ulichokiandika kwenye Tanzania Daima Jumapili hii.
Kwmaba maktaba 1 eti inatumika kwa watu milioni 36! Ulinikuna kwa mjadala huo kwa namna ulivyolieleza vizuri tatizo letu la kutokusoma.
Nadhani kuna haja ya kufanya kampeni ya makusudi kabisa katika jamii yetu kuwafanya wananchi wetu wapende kujisomea vitabu.
Ni tabia hii ya uvivu wa kusoma ndiyo inatuzalishia hata hawa anonymous tunaowajadili mara kwa mara. Watu wanapenda kusoma vitu rahisi rahisi vyenye mwelekeo wa udaku.
Nimekaa miji kadhaa hapa nchini ambayo huwezi kukosa baa na sehemu za kuoneshea filamu kwa kila umbali wa hatua kadhaa. Lakini maktaba huwezi kukuta! Duka la vitabu ndio usiseme, hakuna. Na hata kama makataba ikiwapo wahudhuriaji ni wakubabaisha (wanahesabika). Na mara nyingi wanakuwa ni wanafunzi ambao nao wakishakamilisha masharti ya mitihani wanaungana na jamii yao isiyopenda maandiko.
Utatuzi wa tatizo hili unahitaji watu "waliojikana" watakaoamua kulibeba jukumu hili pasi kuzingatia hasara watakayopata.
Hapa kila mtu anahusika. Na naamini kwamba tutaweza tukiwa na dhamira ya dhati ya kubadili mfumo wa mambo.
Kuanzia na mitaala yetu inayofunga fahamu za wanafunzi wetu. Mitaala inayobana hata suala la uandikaji huru kwa wanaoweza kufanya hivyo.
Nimnukuu Makene: "Tunaweza cheza karata yako!"
Tarehe: 10:46:00 AM, Mtoa Maoni:- boniphace
Jeff hiyo para ya mwisho kabisa ndiyo imenikuna sana. Je nimuuombe Ndesanjo afikishe salamu hizi kwa Freddy, kazi zake zile sasa zaweza kuwa kitabu kipya kabisa na kikubwa mno ambazo zaweza kutumika kwetu kama ambavyo zile za Ndesanjo na wewe Jeff zaweza kuchukua mkondo huo. Kama naona hivi Jeff umetangaza Azimio la wamiliki wa Magazeti Tando kuhamia kukusanya mawazo yao na kujipanga yawe vitabu hivi au vipi tena?
Tarehe: 3:32:00 AM, Mtoa Maoni:- mwandani
Mwezi ujao tarehe tatu kuna majadiliano kuhusu kitabu cha Mwakikagile kuhusu mahusiano ya waafrika wamarekani na waafrika. Mwenye wasaa anaweza kusikiliza majadiliano hayo mtandaoni. Tangazo la mjadala huo hili hapa:
Wednesday, May 3rd, from 6 - 7:30pm EST
TUNE IN VIA INTERNET to the
'Voices from the Drum' (VFTD) Radio Book Club
on WCLM 1450/AM Radio with host, GLORIA TAYLOR EDWARDS
VFTD interviews Professors:
ALBION MENDS and Adisa Alkebulan
Subject: Relations Between Africans and African Americans
Tune in at:
http://www.wclmradio.com/pages/home.html and click on the 'Listen Live' tab.
Details...
Focus: GODFREY MWAKIKAGILE’s book, 'Relations Between Africans and African Americans: Misconceptions, Myths and Realities'.