VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Monday, April 24, 2006
LEO NI SIKU GANI?

Ni jioni ya tarehe ya leo kwa saa za hapa Toronto. Jua ndio linazama(picha kulia shahidi) huku manyunyu nayo yakitiririka( kwa bahati mbaya kamera yangu imeshindwa kuyapata manyunyu-Michuzi utaniambia wakati ujao nifanyeje).Kwa hadithi na simulizi zile za zamani,simba anazaa! Leo ni mojawapo ya zile siku zenye mchanganyiko wa hisia kadha wa kadha,siku zenye maswali mengi yenye majibu machache.Sina uhakika kuhusu machozi ya huzuni au ya furaha kwa sababu sikumbuki mara ya mwisho kupata machozi ilikuwa ni lini. Hii isije ikakudanganya kwamba sijawahi kulia kamwe,la nilishawahi na nilipata ahueni nilipohakikishiwa siku moja kwamba kulia ni sawa,ndio ni sawa hata ukiwa mwanamume! Nadhani hii ni tofauti na tulivyolelewa kuamini tangia utoto wetu..."mwanaume halii bwana,jikaze" Kuna haja ya kuwaambia watoto wetu msemo huu kwa umakini siku hizi.Wakijikaza,wakifa kiume matokeo yake huwa ni yale wanayoyapenda sana watengeneza habari wa vyombo vikubwa vya habari..ni damu na maafa.

Mchanganyiko huu wa mawazo niliuanza jana baada ya kuongea kwa simu na
Makene. Lazima nikiri kwamba Makene amekuwa akinipa mwamko wa mawazo yenye msingi sana kila mara tunapopata nafasi ya kuongea. Hivi sasa anamalizia kitabu chake, namuahidi kuwa mmojawapo wa wanunuzi wake wa mwanzo. Jana tukajadili suala moja ambalo mara nyingi huwa hatulitilii maanani sana. Hivi kwanini katika mitaala na orodha ya vitabu vya kusoma shule za sekondari hususani kwenye somo la kiingereza hakuna kulichoandikwa na mtanzania? Kwanini watanzania hawamo katika lile kundi la African Writers Series? Kwanini tusome vya akina Ngugi, Soyinka, Achebe, Kwei na wengineo bila kuwepo kina Msangi, Macha, Makene, na wengineo. Kama tumeshindwa kuandika kwanini basi tusitafsiri tu hata kazi kama za Kuli (unaweza kukisoma kitabu kizima hapa mtandaoni,shukrani kwa tekinolojia!) na vile vya akina Ngoswe vikawa katika kiingereza?Nia ni kuwa na upande wa shilingi ambao una picha zetu,historia yetu,hadithi za tamthilia zetu,tamaduni zetu,shida na raha zetu nk.

Wakati tukiyajadili hayo nikamuuliza Makene kama amewahi kusoma vitabu vya mtanzania
Godfrey Mwakikagile? Wangapi tunamjua huyu bwana na kwamba vitabu vyake vinatumiwa hata katika vyuo mbalimbali duniani? Kitabu chake kimojawapo nilicho nacho ni kile kiitwacho "Africa is in A Mess: What Went Wrong and What Should Be Done" Ni kwanini hiki kisiwemo kwenye orodha ya vitabu vya kusomwa nchini mwetu? Au ukweli unauma? Katika kitabu chake kingine kiitwacho "Relations Between Africans and African Americans: Misconceptions, Myths and Realities",Mwakikagile anatoa hoja nzuri sana kuhusu mahusiano ya waafrika na wamarekani weusi au waafrika wamarekani. Kama unafuatilia maandiko yangu mara kwa mara utakuwa umegundua kwamba hii ni hoja ambayo huwa napendelea sana kuijadili. Soma "chapter five" ya kitabu hicho kwa kubonyeza hapa.Ukivutiwa na hoja zake basi nenda dukani ukanunue kitabu hicho na kile pale juu, uwe nacho kwenye maktaba yako.Kwa bahati mbaya sijui G.Mwakikagile yuko wapi wala anafanya nini hivi sasa.Kuna mtu anafahamu hilo?

Nikiwa bado mwenye mawazo tele,napata ahueni kusoma kwamba mwanablogu mwenzetu,
Ndesanjo Macha,amepata tuzo kutoka kwa jirani zetu Wakenya. Hili linanitia moyo na kuamini kwamba tunachokiandika hapa sio bure,ujumbe unawafikia wengi na mapinduzi yapo njiani. Watanzania huwa tuna sifa ya kuanza mbio taratibu kabla hatujawapita washindani wengine kwa kasi ya ajabu. Nikiwaita wakenya washindani wetu nadhani nitakosea,hivyo nitawaita wakenya wenzetu na jirani zetu.Washindani wetu,daima watabakia kuwa wamagharibi.

Nikiangalia vyombo vya habari vya nyumbani Tanzania vyote vitejaa habari za
ujambazi,ushujaa,na kupandishwa vyeo kwa polisi waliohusika. Ni habari ya kusikitisha lakini yenye kutia matumaini kwamba angalau safari hii tuna raisi ambaye anajitahidi kuwa karibu na wananchi. Angalau anatambua kwamba kuwa raisi haimaanishi kuunguza mwili na suti masaa 24!
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:59 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 7:17:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Mwezi ujao tarehe tatu kuna majadiliano kuhusu kitabu cha Mwakikagile kuhusu mahusiano ya waafrika wamarekani na waafrika. Mwenye wasaa anaweza kusikiliza majadiliano hayo mtandaoni. Tangazo la mjadala huo hili hapa:

    Wednesday, May 3rd, from 6 - 7:30pm EST

    TUNE IN VIA INTERNET to the
    'Voices from the Drum' (VFTD) Radio Book Club
    on WCLM 1450/AM Radio with host, GLORIA TAYLOR EDWARDS

    VFTD interviews Professors:
    ALBION MENDS and Adisa Alkebulan
    Subject: Relations Between Africans and African Americans

    Tune in at:
    http://www.wclmradio.com/pages/home.html and click on the 'Listen Live' tab.

    Details...
    Focus: GODFREY MWAKIKAGILE’s book, 'Relations Between Africans and African Americans: Misconceptions, Myths and Realities'.

     
  • Tarehe: 8:44:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Ahsante Ndesanjo kwa taarifa hii.Ni muhimu kusikiliza majadiliano hayo

     
  • Tarehe: 9:09:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Christian Bwaya

    Maandiko haya nimeyahusisha na kile ulichokiandika kwenye Tanzania Daima Jumapili hii.

    Kwmaba maktaba 1 eti inatumika kwa watu milioni 36! Ulinikuna kwa mjadala huo kwa namna ulivyolieleza vizuri tatizo letu la kutokusoma.

    Nadhani kuna haja ya kufanya kampeni ya makusudi kabisa katika jamii yetu kuwafanya wananchi wetu wapende kujisomea vitabu.

    Ni tabia hii ya uvivu wa kusoma ndiyo inatuzalishia hata hawa anonymous tunaowajadili mara kwa mara. Watu wanapenda kusoma vitu rahisi rahisi vyenye mwelekeo wa udaku.

    Nimekaa miji kadhaa hapa nchini ambayo huwezi kukosa baa na sehemu za kuoneshea filamu kwa kila umbali wa hatua kadhaa. Lakini maktaba huwezi kukuta! Duka la vitabu ndio usiseme, hakuna. Na hata kama makataba ikiwapo wahudhuriaji ni wakubabaisha (wanahesabika). Na mara nyingi wanakuwa ni wanafunzi ambao nao wakishakamilisha masharti ya mitihani wanaungana na jamii yao isiyopenda maandiko.

    Utatuzi wa tatizo hili unahitaji watu "waliojikana" watakaoamua kulibeba jukumu hili pasi kuzingatia hasara watakayopata.

    Hapa kila mtu anahusika. Na naamini kwamba tutaweza tukiwa na dhamira ya dhati ya kubadili mfumo wa mambo.

    Kuanzia na mitaala yetu inayofunga fahamu za wanafunzi wetu. Mitaala inayobana hata suala la uandikaji huru kwa wanaoweza kufanya hivyo.

    Nimnukuu Makene: "Tunaweza cheza karata yako!"

     
  • Tarehe: 10:46:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Jeff hiyo para ya mwisho kabisa ndiyo imenikuna sana. Je nimuuombe Ndesanjo afikishe salamu hizi kwa Freddy, kazi zake zile sasa zaweza kuwa kitabu kipya kabisa na kikubwa mno ambazo zaweza kutumika kwetu kama ambavyo zile za Ndesanjo na wewe Jeff zaweza kuchukua mkondo huo. Kama naona hivi Jeff umetangaza Azimio la wamiliki wa Magazeti Tando kuhamia kukusanya mawazo yao na kujipanga yawe vitabu hivi au vipi tena?

     
  • Tarehe: 3:32:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Jeff ahsante kwa kuamsha fikra. Haya mambo au habari hizi ziko pale zinasubiri tu kusomwa au kusikilizwa.

    Kwa mwendo huu wa kuamshana tutawajua akina sidi (wazigua wa Hyderabad na Gujarat) kama ulivyoandika makala iliyopita na akina Mwakikagile na michango yao kwetu.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker