VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, May 10, 2006
BARUA KWA GEORGE BUSH!

Dunia inawayawaya. Msemo huu nimewahi kuusikia na kuukubali katika kamusi yangu.Kwa bahati mbaya sikumbuki vizuri niliusikia wapi.Kumbukumbu ya mbali inanionyesha kwamba niliwahi kuusikia kwenye masuala ya "injili".Enzi zile nilipokuwa sijajua kwamba dini sio uhuru bali inaweza kuwa utumwa wa aina yake.

Kuna jambo ambalo nimekuwa nalitamani na nitaendelea kulitamani sana.Sio jingine bali la kuona siku moja viongozi/kiongozi wa nchi yeyote duniani w/anasimama imara dhidi ya Marekani.Hapo ndio nishawahi kuhoji akili za viongozi wa yale mataifa yanayounda lile kundi la G8.Kwamba inakuwaje na wao wanabakia kuwa walalamikaji dhidi ya Marekani badala ya kuwa wepesi(uwezi wanao) wa kuiambia Marekani,imetosha?

Hivi sasa kuna kiongozi mmoja (kwa bahati mbaya au nzuri yeye hatokei katika lile kundi la G8).Huyu si mwingine bali
Mahmoud Ahmadinejad,raisi wa Iran(pichani). Majuzi amefanya jambo ambalo limenifurahisha sana.Amemuandikia barua George W.Bush (Ndesanjo humuita George Kichaka). Kilichonifurahisha sio barua tu bali yale yaliyomo kwenye barua hiyo. Unadhani dunia ingekuwaje kama kungekuwa na viongozi kumi tu wenye msimamo wa aina hii dhidi ya Marekani? Kumbuka ufedhuli wa Marekani unaathiri dunia nzima. Isome barua yenyewe hapa(samahani kwa wasiotumia kiingereza)

Mwisho nimetegua kitendawili cha ile nyumba yenye bendera ya Tanzania nje. Jibu lipo kwenye comments za ile picha.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 4:49 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 5:32:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger John Mwaipopo

    Barua hii nitaisoma leo usiku nikishiba ugali na maharage.

    Lakini natanguliza msemo huu: "Ni heri kufa ukiwa umesimama kidete kuliko kuishi ukiwa umepiga magoti".

     
  • Tarehe: 9:32:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Barua hii ni nzuri iliyojaa mantiki. Kama alivyosema Ahmadinajad kwamba yeye kikazi ni mwalimu - katumia utaalamu wake.(kama sio utaalamu wa waandishi wake wa hotuba)

    Nadhani Ahmadinajad kaiandika hii barua akijua wazi walengwa wake ni umma kama sisi - na ndio maana imetufikia kwa haraka.

    Kadhalika inasemekana kuwa kichaka ana ugonjwa unaomzuwia kusoma au kuelewa mambo kwa haraka.

    Vile vile barua hii nadhani imeandikwa kuwatayarisha wanamgambo ikiwa irani itashambuliwa. Pia imeandikwa ili kumuweka Ahmadinajad katika vitabu vya historia kama mwanadiplomasia wa kimataifa - siyo wengi wanaoandika kwa viongozi wenzao kama binaadamu wawili wanaotaka maelewano.

    Jambo la kuhusisha udini na jina la Yesu kwenye ugomvi huu nadhani ni karata mojawapo ya mizungu ili ajiweke vizuri kwenye mchezo na kujipa wajihi mzuri kwa walio wengi.

    Tusisahau wote hawa wanatumia dini kama mwongozo wa kutawala - na wangekuwa ni wao pekee wanaotawala dunia nzima, wote wasioamini kama wao wasingekuwa na haki yoyote ya "kibinaadamu".

    Wanachogombania ni nguvu za kibeberu kwa upande wa marekani na nguvu za kujihami kwa upande wa Irani. Mengine yote hayaleti maana. Na Irani ana haki ya kufanya uchunguzi wa "nookelaar" kama wengine wanafanya - Brazil imefungua mitambo hivi majuzi tu bila tatizo wala kelel kutoka kwa yeyote.

    Kwamba kichaka anataka kuzuia nguvu za "nookelaar" za iran ili asiangamize Uyahudi sielewi hili - kama Irani akidondosha bomu Jerusalem si ataangamiza maeneo matakatifu ya Waislamu? Si ataangamiza wapalestina anaotaka kuwasaidia na kuwanywesha mionzi Jordan na Misri?

    Kama kuna la msingi hapa ni kwamba irani inasimama kupigania haki ya kujiunga na klabu ya wenye nguvu za maangamizi.

     
  • Tarehe: 3:06:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    kUNA AYA ANAZUNGUMZIA aFRIKA NA UNYONYAJI WA MATAIFA YA KIGENI KATIKA MADINI. Hivi ndugu Mkapa yuko wapi aweze kusoma barua hii au nani anafahamu e mail yake personal aniwekee hapa nimtumie attachment hii? Na nini afasi ya viongozi wetu katika kusimamia haya ambayo jamaa huyu anatusemea katika barua yake kwa ichaka?

     
  • Tarehe: 8:17:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Sultan Tamba

    Mimi hii barua naiprinti niisome chumbani usiku, maana tukio lenyewe tu limenisisimua.

     
  • Tarehe: 3:45:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Brazil has joined the select group of countries with the capability of enriching uranium as a means of generating energy.

    A new centrifuge facility was formally opened at the Resende nuclear plant in the state of Rio de Janeiro.

    The Brazilian government says its technology is some of the most advanced in the world.

    The official opening follows lengthy negotiations with the United Nations nuclear watchdog, the IAEA.

    Brazil has some of the largest reserves of uranium in the world but until now the ore has had to be shipped abroad for enrichment - the process which produces nuclear fuel.

    In future some of that enrichment will take place in Brazil.

    The government says that within a decade the country will be able to meet all its nuclear energy needs.

    Brazilian scientists insist their technology is superior to that of existing nuclear powers. They claim the type of centrifuge in use at Resende will be 25 times more efficient than facilities in France or the United States.

    Safeguards:
    Sensitivity over that technology led to a standoff two years ago with the International Atomic Energy Agency, the UN watchdog.

    Keen to protect its commercial secrets, Brazil was reluctant to give inspectors full access to its facilities and politically the negotiations were complicated by simultaneous concerns about Iran's nuclear plans

    But in the end Brazil and the IAEA agreed a system of safeguards to ensure that the new facilities would not be channelled into weapons production.

    opening at Resende is being hailed as a major step forward in Brazil's development and it comes amid renewed concerns about energy supplies in South America.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker