Tarehe: 8:04:00 AM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 1:41:00 PM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
MtiMkubwa,
Umenigusa kweli na nia yako ya kuendeleza kukuza "muziki wa kweli".Naamini kabisa,toka ndani ya moyo wangu kwamba mafanikio yako yatakuwa si haba.Watu bado tunataka muziki,bado tunapenda vionjo vya kwetu.
Kila la kheri.Kuna Cds fulani za muziki wa kiafrika ninazo nitakutumia sampuli zake ili uwe nazo kwenye maktaba yako..niandikie kaji-email jeffmsangi@sympatico.ca tuongee.
Tarehe: 11:30:00 PM, Mtoa Maoni:- MICHUZI BLOG
mtimkubwa nakutakia kila la kheri. mie pale dar nimeanzisha kijikampuni kiitwacho kaptoletaz entertianment ambako nataka nijikite nako kwenye muziki wa asili.
kama ujuavyo, kilimanjaro band `njenje`sasa wanaendesha ambassador plaza zamani gogo hotel (siku hizi njenje plaza) na wamenipa kukaribisha vikundi vya ngoma za utamaduni na muziki asili kila ijumaa. nikirudi trip ntaanza, ntakufahamisha. je waonaje? jeff pia wasemaje?
Tarehe: 8:47:00 AM, Mtoa Maoni:-
Jeff,
Poa sana, ninashukuru sana kwa nia yako ya kutaka kuboresha maktaba yangu. Nitakuandikia mara tu nikimaliza kurandaranda ndani ya magazeti tando.
Muhidin,
Umenistua kidogo! Ina maana Wana Njenje ni majasirimali, ina maana wamenunua Embassador Plaza?. Hii inanikumbusha enzi za OMACO-Ochestra Marquis Company. Jamaa wa Marquis du Zaire walikuwa mfano wa kuigwa walikuwa na mashamba kibaha, nyumba, klabu yao wenyewe, sehemu ya kuuzia mazao yao pale Karikaoo sokoni, mavokswageni kombi yao. Nakumbuka nilikuwa nikimuona Marehemu Mbuya Makonga Adios akiendesha moja ya yale VW makombi. Pamoja na yote haya jamaa walikuwa wanataabishwa maswala ya residence and working permit!
Tanzanites pia walikuwa na investments zao kule Kimara.
Lakini kitu kimoja kinanikera kuhusu serikali kuwakatisha tamaa hawa jamaa kwa kutowasaidia hata kujenga studio ya kurekodi kaseti!
Haya mengine yameingia kwa sbabu ya shauku na jazba. Turudi tulipoanzia nitakuandikia sasa hivi.
Michuzi, natarajia kuingia jijini siku si nyingi toka sasa. Ikiwa kama yatakuwa kama nitakavyo nadhani nitabeba aipod au kisanduku kizima cha CD mia unusu ili kuja kuburudisha katika hizo siku nitakazokuwepo nchini.
F MtiMkubwa Tungaraza.
Jeff,
Huwezi amini! Kwamba leo hii nimechomoa CD ya African Guitar Summit ambapo nilikuwa nasikiliza nyimbo namba saba Pesa ni Ufunguo, iliyotungwa na Adam Solomon. Nilipotoa CD African Guitar Summit nikaingiza ya CD ya Les wanyika Amigo ambapo niliirudia nyimbo ya Sina Makosa mara mbili ili nisikilize vizuri mipigo ya drums ambayo iliyopigwa na William Muhina au Juma Iddi Mikulandi.
Wakati nasikiliza hizi cd nikakumbuka picha aliyoweka Michuzi ya pale Leaders Club kila Jumapili wanapopiga Twanga Pepeta. Nikajisemea moyoni kwamba ni lazima niwasiliane na jamaa zangu Dar ili kwamba tuanzishe klabu ya miziki ya kikweli haswa miziki kama ya Wanyika, Nuta Jazz, Afrosa, Safari Trippers, Dar Jazz, Jamhuri Jazz, Ochestra Makassi, Marquis du Zaire, Matimila, nk.
Kwa ufupi tu, mimi ni mwanaharakati wa miziki ya Kiafrika na huku ughaibuni nilipo huwa natayarisha madisko ya miziki ya kinyumbani. Ijumaa ijayo nitamwaga vumbi kwenye Klabu ya Dubrovnik (ukigoogle 'afro fusion dubrovnik' utaona matangazo yangu). Katika harakati zangu hizi nategemea kuingiza muziki wa Kiafrika katika main stream music scene ya huku nilipo. Inshaallah mambo yakienda kama ninavyotarajia mwezi wa sita au wa saba nitakuwa napiga disko la Kiafrika katikati ya jiji.
Yote tisa umenichengua kumkuta Adam Solomoni ukumbini.
F MtiMkubwa Tungaraza.