VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Monday, May 29, 2006
POW WOW!




Majira ya summer ndio yashaanza kupiga hodi. Jana joto lilikuwa nyuzi joto 25,leo ni nyuzi joto 31.Hii ina maana kwamba leo hapa Toronto pana joto kuliko Dar-es-salaam. Joto la hapa linakuwa baya zaidi kwa sababu ya kinachoitwa na wanasayansi "humidity".Ukizingatia pia kwamba hapa hakuna "upepo wa bahari unaonukia"(hivi ule pale nyuma ya Aga Khan hospital na Kigamboni ni upepo unaonukia au unaonuka?) basi kajoto ka kukera huwa kanazidi kupamba moto.

Lakini kwa jinsi yeyote ile wenzetu hujua sana kufurahia majira haya.Mtu unatamani wikiendi isiishe.Kila kona ya jiji ni midundo ya ngoma,muziki na pia makelele ya kilevi nk.Nyama choma na masanga ndio usiseme.Ndio raha au karaha ya summer.Huu ndio ule wakati wa "licenced to walk naked".Utaona chuchu na makalio mpaka uchoke.Utahisi watu wote wametoroka "Mirembe".

Jambo moja ambalo nimetokea kulipenda sana wakati huu wa summer ni kuhudhuria sherehe za wahindi wekundu(wenye nchi asilia) zinazoitwa
pow wow .Mimi huzipenda sherehe hizi kwa sababu nyingi zikiwemo zile za kuutukuza utamaduni wao. Ni sherehe poa sana hizi na nazisubiri kwa hamu mwaka huu. Pichani ni mwaka jana nilipohudhuria pow wow katika mojawapo ya kambi wanazokaa hawa wahindi wekundu. Wazungu wamewapora jamaa nchi yao.

 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:57 AM | Permalink |


Maoni: 4


  • Tarehe: 7:12:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger John Mwaipopo

    Jeff umenikuna roho ulipouliza kuwa upepo wa Dar unanuka ama unanukia. Ni mchanganyiko wa kunukia na kunika. Kwa mbaali kuna kaharufu ka samaki. Mengineyo ni uvundo anuai. Si mnajua bado hatujafanikiwa katika maji taka.

     
  • Tarehe: 9:14:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger MICHUZI BLOG

    ina maana joni tayari uko bongo? mbona hatuambiani, ama zemarcopolo kachomekea tu. anyway, jeff naomba kuuliza. hivi sisi kila sherehe ya taifa kuwa na ri-gwaride kama vile tuko chini ya himaya ya jeshi (!) inalipa? kwa nini mtu wa kawaida hapati nafasi kusherehekea na anaishia kukodolea macho maafande tu?

    jeff picha zako na maelezo nimevipenda. kaza buti kaka.

     
  • Tarehe: 9:36:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Zemarcopolo,
    Nude Beaches hapa Canada zipo kibao tu.Unataka picha nini?

    Mwaipopo
    ahsante kwa msaada wa majibu kuhusu bahari yetu na harufu-manukato

    Michuzi,
    Swali lako zuri sana na pia hoja yako.Nadhani kuna haja ya kubadilika jamani.Tamaduni zetu tunaziua sisi wenyewe kwa kuthamini mtutu kuliko ngoma.

     
  • Tarehe: 9:18:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Jeff hivi wakubwa wa kaya wanatambua namna ulivyo mzalendo? Wenzangu kama hamjaona msishangae Jeff akapelekwa lupango segerea kwa kupiga wimbo mtukufu kila dakika katika gazeti tando lake? Polisi wa kwetu watakwambia, haka kamjamaa kanajifanya kamtu kaserikali wakati hakana nafasi yoyote? Nashukuru kwa kuonyesha kuwa hata sisi tunaweza kutumia mali za umma kama hizi na sio vigogo tu.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker