VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, May 19, 2006
TAMADUNI ZETU!

Kila ijumaa jioni mimi hupata muda wa kukutana na vijana wadogo ambao aidha wao wenyewe wanatokea Afrika au wenye asili ya Afrika.Mojawapo ya shughuli za kitamaduni ambazo huwa tunazifanya ni ngoma. Ngoma bwana huwa kama sala wakati mwingine.Mimi hupenda kusema ngoma ni "meditation" ya kutosha sana kwetu sisi waafrika.Ukiusikiliza mlio wa ngoma kutokea moyoni na sio kichwani basi mwenyewe utaniambia kama kuna dawa ya asili nzuri kuliko hii.

Mtu asiyejua na kuthamini historia na tamaduni zake asilia ni kama meli isiyo na rada.Huishia pembezoni mwa bahari nyeusi.Pichani ni baadhi ya vijana wangu wakiwa wamepozi na ngoma.Ngoma hizi zilitoka pwani ya Afrika ya magharibi.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 10:01 AM | Permalink |


Maoni: 3


  • Tarehe: 10:54:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Zemarcopolo,
    Kwa bahati mbaya sana nina kijana mmoja tu wa kitanzania kwenye kundi hili.Ila mganda huwa unapigwa.Marehemu Hukwe Zawose ndio anatuhamasisha na ngoma za kwetu.

     
  • Tarehe: 11:06:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger MICHUZI BLOG

    ebwana umenikuna sana na khabari ya kucheza ngoma kila ijumaa kwani mie nafanya hivyo kila siku hiyo hapa dar pale nyumba ya sanaa. na nimeanzisha kampuni kapitoletaz entertainment itayoshughulikia masuala ya ukuzaji sanaa, na makao yangu nahamishia ambassador plaza (zamani gogo hotel) pale morroco. kila ijumaa nataka watu wale sindimba. ngoma kama hiyo nami nnayo chumbani. kanitengezea mbunju wa simba theatre.

     
  • Tarehe: 7:55:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger severine

    Ni kweli Mh.Jeff huwezi kuzungumzia tamaduni za mwafrika bila kuhusisha vitu muhimu kama vile ngoma.Ngoma inahusishwa na uhai katika jamii ndio maana mbali na burudani ngoma ina maana kubwa sana katika mambo mbali kama vile matibabu.Ili kujua kwa mfano namna ngoma inavyotumica katika matibabu katika africa na Tanzania kwa ujumla jaribu kutembelea(kusoma) kitabu hiki:

    "The Quest For Fruition Through Ngoma: The Political Aspects Of Healing In Southern Africa. Oxford:Kimehaririwa na kuandikwa na James Currey.

    Katika kitabu hiki kuna mambo mengi ya kuvutia hasa kutoka katika makabila ya wanyamwezi na wasukuma.Nilipigwa na butwaa kujua kwamba ndani ya makabila ya wanyamwezi na wasukumuma pekee kulikuwa na aina zaidi ya 107 tofauti za ngoma.kwa leo sijui zipo aina ngapi!

    Nafikiri mpango alio nao nd.Michuzi ni mzuri sana na ninaamini kwamba kwa njia hiyo utaweza kudumisha utamaduni wa ngoma kwa kiasi kikubwa.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker