VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Thursday, June 22, 2006
TOGO

Ingawa timu yao ya taifa ya soka imeshindwa kufurukuta huko Ujerumani watogo bado wanacho cha kujivunia;ngoma na midundo kama hii.Hiki ni kikundi cha ngoma kutoka Togo kikiburudisha katika tamasha liitwalo Carassauga katika jiji la Mississauga hapa Greater Toronto Area hivi karibuni. Walikuwepo kwenye banda la Afrika.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 12:14 PM | Permalink |


Maoni: 5


  • Tarehe: 11:15:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Jeff, hapo Toronto kila siku kuna matamasha ya kitamaduni nini?
    Togo wametoka, lakini Ghana wametupa fahari ya kutosha. Nasikia Marekani wamechukizwa kiasi ambacho Joji Kichaka anataka kuiwekea Ghana vikwazo!

     
  • Tarehe: 9:55:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Ndesanjo,
    Wakati huu wa majira ya joto,Toronto ni mahali poa kupita kiasi kuishi.Matamasha ya kitamaduni yanakuwa kila siku,jumatatu mpaka mpaka jumapili.Hiyo ya Joji kichaka poa sana,imenivunja mbavu kabisa

     
  • Tarehe: 2:30:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mloyi

    Unajua hawa jamaa wa afrika magharibi ni wepesi sana kwenye kutangaza utamaduni wao , wanatuacha sisi watanzania kwa mbali sana. Sidhani sababu ni umahiri wa sanaa zao kuliko zetu, ila ni ushiriki wao kwenye maonyesho.
    Mlioko ughaibuni najua huwa mnayasikia haya matamasha na kuhudhuria, fikiriene ni mara ngapi watu wa nyumbani huwa wanahudhuria, nini kinaweza kufanyika ili wapewe mialiko zaidi.
    Changamoto jaribuni kuwa karibu na waandaaji wa matamasha hayo na kuomba nafasi kwa ajili ya wasanii wa kinyumbani.

     
  • Tarehe: 6:28:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    hi Jeff hi!
    Mimi bado natoa dukudku langu langu kwenye makala ulioandika kwenye gazate la mwananchi kuwa vyu vyetu vinazalisha manamba.

    Utaifa uwe na nafasi hiyo moja sidhani kama ulikuwa sahihi vile uwe balozi wa nchi yako .

    Tuna wataalam wanaoheshimika wakiwa wamesoma Tanzania huko NASA , Erickson kampuni ya simu.

    Tunahitaji changamoto lakini sio kubezwa nilitaka kukupigia simu siku ile .
    kwa her

     
  • Tarehe: 8:56:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Kwa bahati mbaya au nzuri umeficha jina lako.Sio mbaya kwani huo ni moja ya mitindo huru ya kujielezea.Wakati mimi siandikii gazeti la Mwananchi(huwa nina makala kila jumapili Tanzania Daima) ni wazi kabisa hoja ya vyuo vyetu kuzalisha manamba inaweza kuwa ilitoka kwangu kwa sababu naamini kwamba huo ni ukweli.Ni wazi kwamba vyuo vyetu havimfundishi mwanafunzi kuwa mbunifu ili baadaye aweze kujitegemea,kuanzisha chake,kuwa na ujuzi wa kugundua mambo mapya na sio kubobea kwenye sayansi za kina Newton na Abbot tu.Ndio maana kauli ni kwamba "soma ili upate kazi" kwa maana nyingine soma ukamtumikie mtu,sio usome ili ukajitumikie wewe mwenyewe,ili uboreshe jamii yako.Siku hizi ndio mambo yanazidi kuwa magumu kabisa,mwanafunzi anafanya mtihani wa "alternative to practical".Anasikia kuhusu test tubes wakati hajawahi kuziona.Unategemea huyu anaandaliwa kuwa nani?Chunguza vizuri hao unaosema wanafanya kazi za kuheshimika NASA au Erickson.Chunguza je,walitoka vyuoni kwetu moja kwa moja mpaka huko au walipitia mahali kupigwa msasa?Ahsante kwa mchango wako.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker