Tarehe: 8:49:00 AM, Mtoa Maoni:- boniphace
Tarehe: 3:20:00 PM, Mtoa Maoni:-
Jeff samahani lakini naona serikali yetu haifanyi kazi vizuri, kama tunaweza kuomba misaada kwa ajili ya kuwasaidia ndugu zetu kwa nini tusifanye hivyo? Angalia Israil, unafikiri pesa zote wanazotumia kuendeleza nchi zinatokana na mapato ya nchi yao tu? Mimi naona Tz ikiwa na watu wengi zaidi kama hawa atleast tutapiga hatua. Huyu dada amepata fursa kusaidia jamii ktk sekta anayofanya kazi. Kwa kweli mimi nampongeza kwa ujasiri wake. Harambeee
Tarehe: 11:10:00 PM, Mtoa Maoni:- mwandani
Katika proposal ya hao watanzania imeandikwa:
”People there commonly live in mud huts and, in many rural areas, without electricity. Running water is a luxury,”
There are so many problems’ in her homeland, she said. ”Poor infrastructure, poor housing, poor utilities. No clean water. Poor schools, it’s just overwhelming,’
Katika mistari hiyo kuna ukweli. Hawa watu wamechukua hatua kuomba misaada. Pengine kitu kinacholeta tatizo ni manipulation katika lugha iliyotumiwa kuomba msaada.
Pengine pia kwa kushindwa kwetu tulioko ughaibuni katika nchi hiyo husika kufanya harambee na kukusanya kipato kuweza kujisaidia kabla ya kuomba wafadhili ambao kutokana na stereotypes wametumia lugha ya kudhalilisha. lugha ambayo inafanya kazi ukiwa unaomba. baniani m'baya kiatu chake dawa.
Kama watu wangejumuika na kukusanya kipato kusaidia wangekuwa na ownership ya namna fulani ambayo ingesisitiza uwajibikaji katika huo mradi wa vitanda. lakini kama mimi binafsi na mke wangu tufanya jambo ownership inakwenda kwetu, chances are tunaweza kufanya tutakavyo.
Nimewahi kufanya kazi katika sehemu inayosaidia wakimbizi wanaongia ughaibuni. Ndugu zangu wa kutoka Afrika saa nyingine hata wakijua kimombo huwa wana-act kama hawajui, ikesha husema mengi mengineyo si ya kweli ili kuwafanya wafadhili wamwage pesa na misaada. Manipulation. Manipulation inayoendeleza taswira ya mwafrika kama mtu aliyeshindwa kabisa kujisaidia.
hasira inabaki pale pale kwa kushindwa kwetu kushirikiana na kufanya mambo ya maana.
NB: Suala la Israeli pengine ni la kisiasa zaidi geopolitics fulani. China pia ni nchi ambayo imekuwa ikipokea sana misaada kwa sababu hizo hizo za kisiasa.
Tarehe: 5:38:00 AM, Mtoa Maoni:- John Mwaipopo
Jeff hiyo mijamaa mitatu hapo juu imenisemea. Kwan za habari za sikunyingi.
Manipulation kama alivyosema mwandani hatitakiwi na pengine ipigwe vita. Lakini kama lengo hasa ni kufikisha misaada kunakohusika natamka hadharani kuwa Mungu awazidishie moyo wa huruma ndugu hawa.
Wakina Oweya ndio wale watanzania wasiokumbuka kwao na kukaa kwao nje kumefanya wasahau walikotoka. Kwa muda mchache niliokaaga Marakani niligundua kuwa wao huita spedi spedi na sio kijikokikubwa. Maneno waliyotumia katika kupeleka ujumbe ndio hasa sahii kwa hali halisi iliyopo Kajunjumele na kwingineko Tanzania.
Jana Radio One walikuwa na habari ya mrundikano wa wagonjwa katika Muhimbili hata wengine kulala wawili-wawili na wengine chini kabisa. Je huyo Oweyo analalamika nini kuwa tunadhalilishwa. Sio hali halisi hii.
Jeff nikupe pole sana kwanza! Sasa niingie katika hoja hivi ni nani anaandika ukweli kuhusu Afrika? Hizi ni makala tatu mfululizo nilizowahi kuziandika nyumbani gazeti la Mwananchi.
Je Tanzania inalingana na nchi za magharibi? Je namna hospitali za nchi tajiri na vyyombo vilivyomo hufanana na vya Tanzania? Je wakati vinatupwa ni aibu kuviomba ili vipelekwe katika jamii inayovihitaji? Nini maana ya mitumba?
Jeff, suala si kutumia jina la Tanzania au kudanganya ili kupata misaada. Wenye imani kama zangu tusiopenda misaada kabla ya kufanya nguvu zetu tupo kundi lingine lakini pia wenye kudhani misaaada pekee ndiyo itaweza kunusuru nchi zetu unadhani wafanye nini kuvutia misaada hiyo? Na wanapozungumza masuala yaliyo wazi na kweli je wanadhalilisha? Ni kweli serikali yetu inafanya vema katika afya? Jeff nikuulize wewe...nini maana ya kila kiongozi kwenda kusaka matibabu Ulaya? Je kama mambo yanaendelea huko wanafata nini ughaibuni na siku hizi wanajisifu kabisa kutoa taarifa hizo magazetini? Je hawa hawayapaki matope mataifa ya Afrika kuonyesha namna wasivyoweza hata kuebndeleza husuma za afya katika nchi zao na badala yake wao kutumia madaraka yao kutafuta tiba bora nje?
Swali lingine kwa sasa ni hizi NGO je tunasoama proposal wanazoandika zina madudu mangapi? Pita kwa Mwandani na kisha soma maongezi na mheshimiwa mgeni utabaini nini nazungumza. Nitue kwa msemo wa Kiswahili usemao, "Kwa mwoga huenda kicheko na kwa shujaa huenda kilio" Tujadili na tucheze karata zetu kila jambo linawezekana.