Wednesday, August 09, 2006
AFRICAN GUITAR SUMMIT
Hawa ni baadhi ya wanaojulikana kwa pamoja kama African Guitar Summit. Ni kwamba wanacharaza magitaa kuliko kawaida.Hapa walikuwa wakifanya vitu vyao kwenye tamasha la AfroFest hapa Toronto mwezi uliopita. Ukiikuta CD yao popote ulipo na kama unapenda muziki wenye nakshi za magitaa na ngoma basi usisite kuinunua.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:42 AM
|
Permalink |
-
Jeff, ina maana kuwa hawa jamaa wanacharaza nyuzi hata kuliko hata Komandoo Hamza Kalala au marehemu Moshi William na Ndala Kasheba?
Halafu Jeff, inaelekea hapo Toronto shughuli za sanaa na utamaduni ziko mbele sana maana kila mara unatuletea habari kama hizi. Hivi ile tovuti ya muziki uliyoniambia ni ipi tena?
-
Jeff, nakupongeza kwa habari na picha. Najisikia niko Toronto kila nikipita hapa. U mzima lakini?
-
wajameni amasisheni wana blog waweze kuandika habari mara kwa mara na ikiwamo wewe jeff. tunaitaji kupata habari toka kwenu.
-
Ndesanjo,
Itafute hiyo cd! Ninaipendekeza kwa dhati. Miziki yake itakutuliza tangu nyimbo ya kwanza hadi ya mwisho. Adam Solomoni atakurudisha nyuma kwenye ule mtandao wa Wanyika ukazisikie nyuzi za kina Marehemu Wilson na George Kinyonga, Marehemu Profesa Omar Shabani, na Marehemu John Ngereza. Kwa ufupi, Africa Guitar Summit ni mkusanyiko wa all stars.
F MtiMkubwa Tungaraza.
-
Nakubali hapo Toronto Mzee Jeff ni kiboko kwa mchanganyiko wa matamasha ya kila aina.Nimeisikiliza Africa Guitar Summit na nimekoshwa na roho!
Jeff, ina maana kuwa hawa jamaa wanacharaza nyuzi hata kuliko hata Komandoo Hamza Kalala au marehemu Moshi William na Ndala Kasheba?
Halafu Jeff, inaelekea hapo Toronto shughuli za sanaa na utamaduni ziko mbele sana maana kila mara unatuletea habari kama hizi. Hivi ile tovuti ya muziki uliyoniambia ni ipi tena?