Thursday, August 31, 2006
FELA ANIKULAPO KUTI
Afrika ndio asili ya muziki,muziki na afrika ni mapacha.Haya ni maneno yangu lakini ukweli unabakia kwamba Afrika ni bara ambalo limeshawahi kutoa(pengine linaendelea kutoa,sina uhakika) magwiji wa muziki wa aina yake. Unapoanza kutaja majina ya magwiji wa muziki wa Afrika huwezi kuacha kulitaja jina la Fela Anikulapo Kuti wa kule Nigeria. Ana rekodi ya kutoa santuri zaidi ya 77 na pia kuoa wake wanaofikia 27! Fela hakuwa mwanamuziki tu bali mwanasiasa,mwana-mapinduzi,mpigania haki,mwafrika wa kweli na mengineyo mengi.Leo nimepitia mahali fulani na kukuta maandishi mazuri sana kumhusu Fela Kuti na mapicha kibao yanayoelezea historia yake vizuri sana.Bonyeza hapa usome. Ndesanjo hii ni zawadi yako na wengineo wapenda muziki na tamaduni za Afrika.Mti Mkubwa sijui kapotelea wapi.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 9:47 AM
|
Permalink |