Thursday, August 17, 2006
SANAA KAMA NJIA YA KUELIMISHA.
Mambo yanayoendelea kwenye mkutano wa 16 wa masuala ya ukimwi hapa Toronto ni mengi.Inabidi uwe makini sana katika kuchagua mihadhara na shughuli zinazoendelea. Kama unapenda longolongo za wanasiasa utazipata,nyingi tu.Ukipendelea kukutana na watu ambao wamegeuza ugonjwa hatari wa ukimwi kuwa miradi na biashara zao binafsi utawapata pia. Kama unapendelea mambo ya sanaa kama njia muhimu sana ya kuelimishana kuhusu masuala ya ukimwi kama mimi basi hutobanduka kwenye sehemu inayoitwa Global Village. Pichani hao ni vijana wa Msumbiji wakitumia sanaa kuelimisha. Soma habari zao na mchezo wanaocheza kwa kubonyeza hapa.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 9:41 AM
|
Permalink |