VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, September 20, 2006
ANOTHER NIGHTMARE!

Wakati viongozi wa dunia wanakutana New York,Marekani yapo machache ambayo yananivutia. Kubwa ni hotuba ya raisi wa Iran Mahmoud Ahmadinejad kuhusu anachokiamini,kinachofanyika nchini mwake kuhusiana na tekinolojia ya nyuklia na jinsi ambavyo anaelezea ubabe wa nchi za magharibi. Unaweza isoma hutuba yake kamili kwa kubonyeza hapa.

Bado nasubiri kusikia atakachokisema(pengine ninavyoandika ashasema) raisi wa Tanzania-JK. Mpaka leo sijaweza kupata hasa msimamo wa raisi wangu. Nadhani hili linatokana na wingi wa siasa katika maneno yake. JK hapendi kuudhi mtu,anapenda kupendwa na kusifiwa tu. Ukimuuliza swali atakujibu unachotaka kusikia.Alichokisema huko Havana-Cuba siku chache zilizopita kilionekana kuwa cha maana. Lakini umaana huo unapotoshwa kabisa unapoona kutoka Havana alikimbilia Washington kuonana,kusabahiana,kunywa kahawa na kujikomba kwa raisi George Bush wa Marekani ambaye kimsingi nchi yake ndio adui mkubwa wa nchi zinazosema hazifungamani na upande wowote. Sishabikii viongozi wa dunia kuonyeshana ubabe kila mara ila nadhani kuna wakati maneno ya majukwaani lazima yaendane na vitendo. Msimamo wetu,wa raisi,au nchi yetu ni upi hasa? Nadhani lazima tufikie mahali tueleweke. Tutaheshimika zaidi namna hiyo. Political prostitution sio sifa nzuri hata kidogo.

Yote hayo tisa. Miezi michache iliyopita sinema ya Darwin's Nightmare ilizua janga huko Tanzania. Wimbo wetu wa taifa ukawa "mapanki". Wanasiasa kupitia bunge wakatuonyesha rangi zao halisi juu ya nini wanakijua,nini wanakizingatia nk. Wapiga kelele kama mimi tukaandika. Ukitaka kusoma nilichoandika
bonyeza hapa.

Sasa majuzi nimetumiwa sinema nyingine. Hii ni kuhusu child labour. Imepigwa kule Mererani,kule kule yanakochimbwa madini adimu ambayo serikali yetu imeshindwa kabisa kuyaona kama urithi wa kipekee wa nchi yetu. Najaribu kujiuliza,je safari hii raisi wetu atasema nini? Wabunge wetu watasema nini? Unaweza kuitazama sinema yenyewe kwa
kubonyeza hapa. Pia unaweza kusoma ripoti ya jamaa wa IRINnews kwa kubonyeza hapa.

Picha ya juu kwa niaba ya Michuzi wa www.issamichuzi.blogspot.com. Pichani ni vijana wa Mererani wakisaka Tanzanite. Huko ndiko child labor inapozidi kuota mizizi.


 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 9:56 AM | Permalink |


Maoni: 6


  • Tarehe: 12:21:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger boniphace

    Jeff waweza msoma hapa http://www.un.org/webcast/ga/61/pdfs/tanzania-e.pdf

    Kwa ujumla utahukumu mwenyewe mimi sina comment

     
  • Tarehe: 8:33:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Uwazi inabidi ukubalike. Hakuna kurudi nyuma.

    Hata kama watengeneza filamu wa kitanzania hawataki kutengeneza filamu ambazo hazitauza bali zenye ukweli, wengine wanaoweza kupata funding makwao wataendelea.

    Sijui kama kuna la kubisha, tunasubiri shambulio la filamu nyingine nyingi.

     
  • Tarehe: 8:49:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Egidio Ndabagoye

    Jeff yanayo fanyika huko ni ya kusikitisha sana niliwa hi kufika huko miezai ya nyuma.Kweli Child Labour ipo tena sana kuna wale watotom wanoyumbukia mule shimoni wenyewe wanaita "kuzama" hao watoto wanajulikana sana maarufu kama "manyoka".Hawaa watoto bwana adabu ni 'F' ule utumikishwaji machimboni umeewafanya wawe watukutuku sana kwa kweli ukiwaona utasikitika.
    Kwa sababu wengi wao ni wale waliokatika umri wa kwenda shule lakini wako "kazini"

    Swala na mapanki raisi wetu alipewa data nusu nusu.Wakazi wa Mwanza wanasema wanakula mapanki nafikiri karibu kila kitu kilichomo mule kwenye Filamu ya mapanki kina ukweli sema tu kuna vitru vimetiwa chumvi ile ya Kihollwood.

    Wale wanchama wa CCM na wabunge walioishambulia ile filamu ya bwana Sauper walioandamana sasa waandamane tena.

    Lazima tuukubali ukweli

     
  • Tarehe: 2:05:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Mimi pia nasubiri kuona "maandamano" ingawa kimsingi nadhani ni ujinga kuandamana wakati ukweli tunaujua fika.La maana ni kujenga nchi,kukubaliana na ukweli kwamba sekta nyingi za serikali zinahitaji kuamka,kufanya kazi na sio kuficha maradhi kungojea kuumbuliwa na mauti.

     
  • Tarehe: 10:29:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Wadau !
    Kama kuna jambo watanzania tunapaswa kujifunza ni kuwa challenged .
    Mambo mengi kwenye senema ile ni kweli ingawa watengenezaji walikuwa na ajenda zao kama kawaida.
    Mpaka pale tutakapoweza kusimulia hadithi zetu wenyewe hawa wataendelea kuzisimulia kama wanavyoziona na kufikiri wao !
    But the bottom line it take a Tanzanian to understand Tanzanians struggles.
    Mungu ibariki Afrika !

     
  • Tarehe: 2:48:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Mjengwa

    Jeff,
    Ukweli ni mzigo mzito, haupaswi kubebwa bali utawanywe. Nimefurahia blogu yako, kazi nzuri.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker