Tarehe: 1:16:00 PM, Mtoa Maoni:- Egidio Ndabagoye
Tarehe: 3:05:00 PM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Egidio,
Ukimuona au kumsikia mtu wa namna hiyo(anayetaka kuimba au kughani kama hao kina Jay Z)usimtenge,mwite pembeni msaidie kimawazo,ni mtumwa wa akili,wapo wengi.Mimi sina tabu na kuiga mambo fulani fulani kutoka kwenye tamaduni za wengine(kama tunaona yanafaa).Tabu yangu ni pale vya kwetu tunapoona havifai,tunapoviponda badala ya kuviboresha.Hapo naumia kichwa na kusikitika sana.
Tarehe: 6:09:00 AM, Mtoa Maoni:- Simon Kitururu
Duh! Kama ni kweli siku hizi watu hawafuati mdundiko basi kuna aina moja ya sanaa BOMBA ambayo inakufa Bongo na inasikitisha sana.Kwa sababu mimi hua naamini Wazungu walifuata Brazi Bendi, na mara nyingi iliwekwa kama fomaliti na sio watu wenyewe kuamua kufuata. Sisi bongo sijawahi kuona ngoma ambayo ilikuwa inavuta na iko mobile kama mdundiko. Watu walikuwa wanafuata kwa kupenda.Jeff, Unakumbuka KAMUACHA MUME WAKE KAFUATA MDUNDIKO!
Jeff, ngoma hizi za Mdundiko zikipigwa Bongo watu hawasogelei kwa sana kama zamani.Siku hizi bwana watu wanataka mashindano ya kucheza na kuimba kama akina Jay Z