VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, September 22, 2006
ZANZIBAR NDANI YA TORONTO!

Siku za nyuma niliwahi kuibandika hii picha hapa ubaoni. Niliahidi kwamba ningali namsaka mmiliki wa sehemu hii ili aeleze kwa kifupi uhusiano wa visiwa vya Zanzibar na hii sehemu ambayo shughuli zake haziendani na maadili ya visiwa vya Zanzibar ambavyo ni sehemu muhimu sana ya nchi yetu ya Tanzania.Ukitoa Zanzibar hakuna tena Tanzania bali Tanganyika. Ukibonyeza juu ya hiyo picha ukasoma maandishi yaliyopo nje utagundua nini naongelea kuhusu shughuli zinazofanyika humo ndani.

Kwa bahati mbaya mpaka hivi leo sijafanikiwa kuonana na mmiliki wa kibanda hii. Nilimuachia simu yangu anipigie lakini naona mpaka leo kimya. Nimeamua kuibandika tena picha hii ili kama kuna ambaye anajua uhusiano wa Zanzibar hii ya Toronto na ile ya Pemba na Unguja atusaidie.Unadhani hii inapotosha watalii wanaotaka kuvitembelea visiwa vya zanzibar au ndio inachangia watalii wengi kumiminikia Zanzibar wakiwa na yao kichwani? Unaweza oanisha habari hii na ile ya majuzi kumhusu Mercury? Isome
hapa.

Uchunguzi kidogo nilioufanya unaonyesha kwamba hizi Zanzibar ziko nyingi sana huku ughaibuni. Zote zina shughuli zinazoendana.Mfano angalia hapa au hapa Kwanini?Kulikoni?
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:06 AM | Permalink |


Maoni: 6


  • Tarehe: 2:26:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Jeff
    Ipo Zanzibar night club nyingine hapo Leicester labda wadau wako watakuwekea picha
    Abdul

     
  • Tarehe: 9:14:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Na hapa ninapoishi palikuwa na kilabu cha dansi - Zanzibar, kimefungwa hivi sasa.

    Kitu nachoweza kuwaza haraka haraka ni kuwa Zanzibar ni brand name inayoweza kuuzika.

    Hawa watu wanaotumia hilo jina bila kulipa ushuru kwa sababu zao binafsi ambazo mara nyingi hazina uhusiano na tamaduni za kisiwa hicho - wamegundua kuwa hilo jina lina-sound exotic. Kwa hiyo linatia mvuto fulani.

     
  • Tarehe: 3:24:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Ni sawa alivyosema Mwandani, jina Zanzibar linauzika. Wanasema eti linaleta hisia za kitu "exotic" vile! Karibu kila ninapokwenda lazima nikutane na "Zanzibar."

     
  • Tarehe: 8:40:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mzee wa mshitu

    Zanzibar aaahhh Zanzibarrr, kama Ndesanjo na Tungaraza wanavyosema inauzika, hivyo inabidi tufungue kesi ya kudai fidia ya pesa zinazotokana na mauzo ya mvuto wa jina la Zenj labda tutaweza kupata.

     
  • Tarehe: 5:13:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger NDABULI

    Kwa mtaji huo wa kuuzika inabidi kwanza tulisajiri hilo jina ili tupate haki miliki yake ndio tuwauzie watu

     
  • Tarehe: 10:41:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Zanzibar ni mojawapo ya visiwa murua sana duniani.Watu wa magharibi wamekuwa wakivifahamu kabla ya uwepo wetu mimi na wewe.
    Kuanzia wareno,Wajerumani,Waingereza,Wachina ,Waarabu na Wahindi wamekuwa wakifanya biashara na visiwa hivi kwa miongo mingi.
    Kama umefika Zanzibar utaona ni nini naongelea!
    Hainishangazi kusikia kuna sehemu mahali duniani wanatumia jina hili
    Labda siku moja wabongo watajifunza kwenda holidays kama huko ulaya na kuanza kuja Zanzibar (karibuni sana)

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker