VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, October 04, 2006
KAZI NI KAZI?

Waafrika au niseme watanzania tunao msemo unaosema kazi ni kazi, ili mradi mkono uende kinywani. Nadhani wazee wetu walipoutunga msemo huu walimaanisha tusichague kazi,tufanye kazi yeyote iliyopo mbele yetu. Nadhani nitakuwa sijakosea nikisema msemo huu ni mzuri na kama wengi wetu tungeuzingatia basi pengine yale makundi ya vijiweni kila kukicha yangepungua.

Unadhani msemo huu unazingatiwa? Nipe maoni yako. Pichani ni jamaa akiwa kazini jijini Toronto. Anatangaza bidhaa kwa ajili ya watoto huku akiwasaidia kupuliza maputo yao.Kazi ni kazi? Hebu malizia kwa kusoma
makala hii hapa.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 12:09 PM | Permalink |


Maoni: 4


  • Tarehe: 11:44:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Simon Kitururu

    Kwa mtazamo wangu wa Tanzania, kazi ni kazi ni msemo tu. Nakumbuka tokea shule ya msingi ilikuwa ujanja kukimbia kazi. Utakuta asilimia kubwa ya hata waliotaka kuwa viongozi, moja ya motisha ilikuwa kurahisisha kazi. Angali hata maoni katika haya ma blogu.Ni kawaida kukandia kazi kama za ufagizi, kulelea wazee na zinginezo. Mimi nahisi hili ni baadhi ya jambo ambalo liko katika ubongo wa Mtanzania ambalo bila kubadilika safari ya maendeleao itaendelea kuwa ndefu sana.

     
  • Tarehe: 3:47:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger MICHUZI BLOG

    Naam Jeff!

    Ingawa ni kweli kwamba kazi ni kazi, lakini si uwongo kwamba kazi zingine kweli ni kazi, chukulia mfano ujambazi. jee nikipora mkono hauendi kinywani? na hapo sizungumzii bastola na ngeta, nazungumzia pia rushwa, utapeli na uozo mwingine kama huo. hapa nakumbuka maneno ya Che Mkapa ya: Mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe...

     
  • Tarehe: 11:41:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Simon,
    Umenifanya nifikirie,kumbe suala hili lina ile ile mirija ya utumwa wa akili sio?

    Michuzi,
    Labda tuseme kazi halali,yaani ile isiyovunja sheria na taratibu za nchi husika.

     
  • Tarehe: 9:09:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Kazi ni kazi, katika kiungo ulichoweka kuhusu machina kuwa machinga tanzania... Wale ndio wanavyoenda kama wajinga wajinga, ukishtuka unakuta wanamiliki kila kitu.

    Nenda kokote utakuta wamejenga China-town...

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker