Friday, November 24, 2006
UNAWEZA KUOA WAKE WAWILI KATIKA SIKU MOJA?
Maajabu ya dunia yetu hii hayaweza kuisha hata siku moja. Labda huo ndio ukweli mzito kuhusu dunia yetu. Hivi karibuni huko katika kitongoji kijulikanacho kama Ibrahim Koodnur, karibu na mji wa Hargeysa jamaa mmoja ajulikanaye kwa jina la Ismail Osman Abdullahi alioa wanawake wawili katika siku moja kama anavyoonekana katika picha hiyo hapo juu. Majina ya wake zake hao wawili ni Gasira Mohamed Hussein na Shukri Osman Mohamed.
Habari hii ambayo nimeletewa na rafiki yangu mmoja anayetokea katika nchi hiyo anayeishi hapa Canada hivi sasa, imeniacha kinywa wazi kidogo. Hivi inawezekana kweli? Chanzo cha habari hii kinapatikana hapa kwa wale wanaojua kisomali.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 2:29 PM
|
Permalink |
-
Imenikumbusha tu 1978 Fela Kuti alivyooa wanawake 27. Lakini sidhani kama Tanzania ni kinyume cha sheria kuoa wake wengi siku moja
-
Hivi wenzangu mnaipata site ya Ndesanjo?
-
Braza Simon hii site hata mie siipati.Mimi tatizo hilo limenipaa tangu jana nikajua labfa ni kompyuta yangu lakini nikawa naona ujumbe toka word Pres.Nashangaa kulikoni!
-
Hata mimi haipatikani kutokea hapa kwangu.Nadhani wenyeji wake(hosts) wordpress wanahamisha servers au kitu kama hicho.
-
Jeff wakati fulani nilijaribu kutoa komenti lakini sikufanikiwa kuingia humu.
Temeke iliwahi tokea inayofana-fanana na hii. Jamaa alichumbia binti ambaye alikuwa identical twin na dada yake na walikuwa wakipendana usipime. Dada ambaye hajaolewa akadai hakieleweki mpaka nayea alolewe na mchumba wa pacha mwenzie. jamaa akaulizwa kama anaweza kuwamudu akadai hapana shaka na hatimaye alikabidhiwa mizigo yote miwili kwa mkupuo.
alamsiki
Imenikumbusha tu 1978 Fela Kuti alivyooa wanawake 27. Lakini sidhani kama Tanzania ni kinyume cha sheria kuoa wake wengi siku moja