Wednesday, December 06, 2006
KUULIZA SWALI NI KOSA?
Leo katika gazeti la Tanzania Daima nimesoma habari hii ambayo imeniacha kinywa wazi, sio kwa usingizi mzito, bali kwa mshangao. Eti ni kosa kumuuliza mbunge wako swali na kwamba jamaa mmoja ambaye amefanya hivyo amejikuta akipewa adhabu. Bonyeza hapa usome habari nzima.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:20 AM
|
Permalink |
-
pale nchini kuna vitu vingi sana vya kurekebisha.vyombo vya sheria havitumiki kwa sababu haviaminiwi ndio maana mwananchi baada ya kushitaki mahakamani kuwa hajatendewa haki,inabidi amngoje mkuu wa mkoa ndio amwambie!
-
Nakubaliana kabisa na wewe Zemarcopolo,safari ya nchi yetu bado ni ndefu sana.Hili hunifanya hata nihoji uhuru tunaousheherekea wikiendi ijayo kwamba nini maana yake kama hata uhuru mdogo tu wa mwananchi kujielezea na kuhoji unakuwa mgumu kupatikana.Uhuru huu ni wa nani hasa?
-
Habari nyingine unaweza kusoma na kudhani kuwa ni riwaya tu kumbe kweli. Ingekuwa nchi nyingine nako ni hivi basi Bill Clinton alipokuwa akiulizwa maswali kuhusu kashfa ya nyumba ndogo huku nchi nzima ikitazama luninga, waliomuuliza maswali wangekuwa labda wamehukumiwa vifo.
-
Ni hali halisi iliyoyopo hapa bongo hiyo ya singida ni kiduchu tu kuna mengi sana ya ajabu tu yanayoumiza watu hapa nchini safari bado ni ndefu,watu wanaburuzwa sana hadi unaweza lia
-
JEFF!
UKISHANGAA YA MUSSA...
-
Mzee mzima Jeff haya ni baadhi tu ya mambo yanayovinjari hapa Tanzania sasa. Kila mwenye nafasi ni mkubwa na anatumia ukubwa wake kikweli kunyanyasa sisi watu duni. Samahani nimekuwa napita hapa mara kwa mara ila kompyuta haziruhusu kuchangia. Enewei siku njema pia.
pale nchini kuna vitu vingi sana vya kurekebisha.vyombo vya sheria havitumiki kwa sababu haviaminiwi ndio maana mwananchi baada ya kushitaki mahakamani kuwa hajatendewa haki,inabidi amngoje mkuu wa mkoa ndio amwambie!