Friday, January 12, 2007
KITABU CHA BLOG NA TAJIRI MTOTO
Rafiki yangu mmoja amenipa zawadi ya kitabu kilichoko kwenye picha hapo juu.Kama kinavyoonekana kinaitwa The Rough Guide to Blogging mwandishi akiwa jamaa anayeitwa Jonathan Yang.Kitabu kipo kwenye mfululizo wa vitabu vya jamaa wa rough guides.Kwa mtazamo wangu, kama unataka kuzidisha maarifa yako juu ya kublog basi sio wazo baya kama katika hema za vitabu vyako hiki nacho kitakuwa kimojawapo. Naendelea kukisoma na kujifunza mambo lukuki.Kitabu kinapatikana katika maduka mengi ya vitabu yakiwemo yale ya mtandaoni kama Amazon.Wakati huo huo: Hivi ukizaliwa kwenye familia yenye hali duni kiuchumi inamaanisha na wewe utadumu kuwa duni na kisha kuiaga dunia ukiwa masikini? Yaani utaendeleza historia ya umasikini?Inawezekanaje basi kukata "mzizi wa fitina"? Hebu fuatilia maisha ya Dr.Farrah Gray,bwana mdogo ambaye aliukwaa umilionea akiwa na umri wa miaka 14 tu akiwa anatokea kwenye familia masikini huko kusini mwa jimbo la Illinois nchini Marekani. Fungua tovuti yake na kisha ukurasa wake wa wiki kisha usikate tamaa,inawezekana.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 7:47 PM
|
Permalink |
-
Habari ya mtoto huyu tajiri unaweza kudhani kuwa ni ya uongo. Bwana mdogo sana huyu. Lakini yote haya kweli. Nimemjulia kwako na nikarambaza intaneti nikapata habari zaidi juu yake.
Uhuru na tovuti yao...sio uhuru tu, hata magazeti yetu tovuti zao, mmh. Nimepandisha makala kuhusu hili. Huenda kesho asubuhi wataamka.
Habari ya mtoto huyu tajiri unaweza kudhani kuwa ni ya uongo. Bwana mdogo sana huyu. Lakini yote haya kweli. Nimemjulia kwako na nikarambaza intaneti nikapata habari zaidi juu yake.
Uhuru na tovuti yao...sio uhuru tu, hata magazeti yetu tovuti zao, mmh. Nimepandisha makala kuhusu hili. Huenda kesho asubuhi wataamka.