Tarehe: 4:44:00 PM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 4:54:00 PM, Mtoa Maoni:- Simon Kitururu
Tarehe: 6:57:00 PM, Mtoa Maoni:- Egidio Ndabagoye
Tarehe: 2:07:00 AM, Mtoa Maoni:- mwandani
Tarehe: 4:31:00 PM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 5:17:00 PM, Mtoa Maoni:- MICHUZI BLOG
Tarehe: 9:37:00 AM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Tarehe: 9:30:00 PM, Mtoa Maoni:- Mjengwa
Tarehe: 9:09:00 AM, Mtoa Maoni:-
Tanzania mbili, umenena sawa Maggid. Natoa changamoto kwa Michuzi, ningependa atuwekee mfululizo wa picha zinazoonyesha Tanzania hizi mbili. Nawe Maggid pia una kamera yako, tuanzishieni mjadala kwa picha za Tanzania mbili. Jeff unajua angeweza kutuwekea picha za majengo marefu ya vioo na magari ya kifahari n.k. lakini akaamua kutuonyesha jambo lisiloongelewa sana: mafukara wa MArekani.
Tarehe: 1:35:00 PM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Tarehe: 3:27:00 AM, Mtoa Maoni:- Patrick G. Kamera
Jeff,
Kumbe una blog ya Kiswahili pia!
Duh! Poa sana ndio naicheki hapa, safi sana.
Kuhusu Marekani mbili hilo ni kweli kabisa kama ulivyojionea mwenyewe, kuna Wamarekani wanapigika vibaya ila hilo halitangazwi wala kuonyeshwa CNN, ila kuna kipindi cha "Feed the Children" siku nyingine wanaonyesha Marekani fulani hoi bin taabani tofauti kabisa na ile ya Hollywood inayouzwa duniani.
Tanzania pia tunaelekea hukohuko kama hatujafika, maana wenye navyo wanaendelea kuneemeka na wasionavyo rhumba linazidi kukolea. Tulikuwa nyumbani hivi karibuni tumejionea wenyewe.
Maswali yanakuja, tumejikutaje katika hali hiyo? Nini kifanyike kama kuna cha kufanya au ndio hivyo tena kila mtu kivyakevyake, mwenye nguvu mpishe, au...
Tarehe: 9:59:00 AM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Patrick,
Ahsante kwa kunitembelea hapa kwenye kiswahili pia.Kimsingi hii ndio blog yangu kuu,nakesha zaidi hapa kuliko hata kule kwenye kiingereza.
Mwanablog mwenzetu wa blog ya picha anayeitwa Maggid yeye anasema tayari zipo Tanzania mbili au hata tatu.Inasikitisha kuona kwamba tumeshafika huko na hakuna la maana linalofanyika ili kukomesha hali hiyo.
Patrick,tungefurahi kama ungetupa kidogo tathmini yako kuhusu ulichokiona Tanzania ulivyokwenda hivi karibuni.
Tarehe: 12:27:00 AM, Mtoa Maoni:- Patrick G. Kamera
Jeff,
Tanzania ziko mbili, si ajabu tatu kama alivyogusia Maggid.
Maendeleo kulingana na wengi yapo kwenye miji mikubwa ukianzia na Dar. Majengo kadhaa mapya, marefu, ya vioo na mahoteli mapya pia. Nyumba kubwakubwa, nzurinzuri na mageti ya kufungua kwa "remote", zenye walinzi wenye sare maalum na mitambo ya kulindia kama kamera na ving'ora na mikwara kadhaa. Maeneo ambayo ukipita mwenyewe unatia akili!
Maendeleo mengine ni kwa upande wa magari, yaani ni mengi sana ukilinganisha na wingi(sijui ni uchache) wa barabara zilizopo, hivyo foleni na misongamano ni ya kufa mtu, ni afadhali utembee utawahi unakokwenda.
Hili limechangiwa niliambiwa na maendeleo "kama ulaya tu" ambapo wafanyakazi kuweza kupata kitu kinachoitwa "soft loans" kuweza kununua magari mradi wana mshahara wa kiwango fulani, hivyo wengi wameichangamkia hiyo mikopo. Matokeo yake kila mtu ana gari pa kuendeshea hakuna, na bei ya petroli iko juu kuliko huku, lakini Wabongo wabishi sijaona, watu wanaburuza madude ya nguvu...
Vilevile kuna maduka makubwa yanayoitwa "supermarkets" kadhaa na Malls pia zipo. Hizo ni sehemu ambapo wachache wenye ahueni kiuchumi huonekana wakijivinjari humo. Kingine matumizi ya dola ya marekani wakati tuna shilingi yetu, kwenye masuala mengi tu unasikia hii ni dola kadhaa, hii dola kadhaa, ila ukilipia unalipa kwa shilingi lakini kwa kiwango cha dola cha siku hiyo utakachopewa hapo. Hii ni kuanzia kwenye kadi za simu.
Kila upande kuna mabango na matangazo makubwa ya biashara za simu, sigara na pombe, mabango yenye picha za Rais Kikwete pia yapo hapa na pale(sijui ni mabaki ya kampeni au ndio miondoko ya ki-Kim Il Sung hiyo!)
Hayo ndiyo baadhi ya maendeleo niliyoyaona Dar-es-Salaam.
Upande mwingine wa Dar hiyohiyo ambapo ndipo wananchi walio wengi wanapoishi hali ni tofauti kabisa, hilo rumba lake si la kitoto. Nafikiri unaelewa. Huko maji ya kununua kwa ndoo daima, kutoka bombani imekuwa historia ya hapo zamani za kale...kwa hakika karibu nchi nzima nadhani suala la maji kutoka bombani ni ndoto, umeme ndio wala usiseme, ila nasikia baada ya hizi mvua za juzijuzi mgao hakuna tena. Kwa wananch walio wengi umeme wala sio issue, maana wengi hawanao, ni mwendo wa vibatari, mishumaa, kama una jeuri karabai.
Kijijini nako hakuna nafuu, rumba liko palepale, na cha kutisha zaidi ni idadi ya watu wanaorudishwa au kurudi wenyewe kijijini mwao wakiwa katika hatua za mwisho za kuugua baada ya kuathirika. Hivyo misiba na mazishi imekuwa mingi mno kijijini hadi watu wanashindwa kuacha shughuli zao na kuja kuomboleza pamoja na wafiwa maana utaenda kwa nani utamwacha nani, yaani misiba inaelekea kuwa kama ya huku, familia za wafiwa na ndugu au rafiki wa karibu ambao wanalazimika kuja.
Na hii yote ni maendeleo!
Naona niishie hapo, nikikumbuka mengine nitaendelea kukuhabarisha.
Tarehe: 10:04:00 AM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Tarehe: 6:03:00 PM, Mtoa Maoni:-
Unajua Jeff nilipofika kwa Joji Kichaka nilitazama huku na kule nikaanza kujiuliza, "hivi wale watu weusi tuliokuwa tukiwaona kwenye gazeti la Ebony wako wapi?" Enzi zile nilidhani kuwa watu weusi wote ndio wanavyoishi kama picha za Ebony zinavyoonyesha. Kumbe masahibu ya weusi na weupe pia walio wengi hayaonyeshwi kwenye vyombo vya habari.
Jambo moja nililojifunza ni kuwa majumba makubwa ya vioo na magari ya kifahari, majumba ya kisasa ya muziki, redio, na luninga ni vipimo hadaa vya maendeleo. Ukipima maendeleo kwa kutazama vigezo hivyo, tuseme kwa Tanzania, utakuwa umedanganyika na pia kutowatendea haki wale wanaoishi bila huduma za afya, maji safi, shule zenye walimu na vifaa, barabara zinazopitika, miji misafi, wakulima wanaotegemea mvua za masika, vijiji visivyo na vituo vya afya, wapiga kura wanaodanganywa, n.k.
Marekani ndio hivyo nayo. Mfumo wa ubepari ukitumia nguvu ya vyombo vya habari na utamaduni maarufu vimetufanya tukashindwa kujua nini hasa maana ya maendeleo ya mwanadamu.
Jeff, msikilize John Edwards (aliyekuwa mgombea mwenza wa Kerry uchaguzi uliopita) ambaye ametangaza kugombea urais. John Edwards (ambaye yeye na mke wake ni wanablogu) amekuja safari hii na ujumbe mmoja mzito: Marekani mbili. Ulichozungumzia hapa ndicho anachoongelea huyu bwana. Anasema ndio ugonjwa mkuu wa Marekani. Nchi hii ni sawa na nchi mbili. Nchi ya wachache ambao maisha yao yanadhaniwa kuwa yanawakilisha maisha ya Wamarekani wote. Na wamarekani wengi ambao, ingawa unaweza kuona wana magari na wanaishi ndani ya nyumba, wanaandamwa na madeni hadi mvunguni. Jamaa mmoja aliyekuwa jirani yangu hivi sasa kawa ombaomba. Aliachishwa kazi, akawa anaumwa, mwenye nyumba hakusikia kitu anachotaka ni fedha yake. Akamletea polisi, huyo akatolewa nje. Sasa anaombaomba huku akitafuta kazi!
Ndio ulichosema hapo. Kuna nchi mbili Marekani. Pengine tatu. Ndio mabilioni hayo yanatumika "kueneza demokrasia" (demokrasia ya kuua kwa kamba ya katani kama vile tunaishi karne ya kwanza) kule Iraki.
Mkongo mmoja rafiki yangu alikuwa akisema Marekani ni sawa na barabara ya lami. Unapoendesha gari kwenye barabara ya lami wakati wa jua kali unaona kama barabarani mbele yako kuna maji. Ukifika hapo panapoonekana kama pana maji unakuta hakuna kitu. Kwa lugha yao wanaita "mirage." Ndio Marekani hiyo yenye Gary, Indiana na miji mingine ambayo wanaishi akina Cheney na wezi wenzake na vibosile vya makampuni makubwa yanayohonga wawakilishi hapa ili kusipitishwe sheria ya kima cha chini.