VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Wednesday, February 07, 2007
BARAFU BADO IMETANDA!

Kiwango cha baridi hivi leo kilikuwa centigrade -25 kiwango ambacho ni cha juu ukilinganisha na sehemu zingine za Canada ambapo viwango huenda mpaka centigrade -75 na kuendelea.Nimewahi kumwambia rafiki yangu mmoja kwamba haukuwa mpango wa mungu kwa mwanadamu kuishi kona hizi za dunia eti akabisha!.Maisha yaliwezekana vipi zama hizo upande huu wa dunia?Labda ndio maana inasemekana kwamba mabaki ya kwanza ya binadamu yalipatikana kule nyumbani kwetu na kwamba wahadzabe pengine ndio wa ukoo wa Adam na Hawa.

Ukiitizama picha iliyopo hapo juu kwa makini unaweza kuona mambo kadha wa kadha.Unaweza kuyatambua?


Kisha kama ulidhani wanasiasa wa Tanzania ndio pekee wanaokuwa vitimbakwila kwa kurukia chama kimoja mpaka kingine umekosea.
Wanasiasa ni wanasiasa tu siku zote.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 8:31 PM | Permalink |


Maoni: 4


  • Tarehe: 4:52:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Unknown

    niliyogundua mimi ni alama nyingi za miguu kwenye theluji.inaweza kuashiria kuwa watu hucheza hapo au hiyo ni njia.kitu kingine nilichoona ni kwamba hiki kibarabara kina ramaniramani kibao,inagwa sijaweza kugundua zinamaanisha nini.hata hivyo kilichonifurahisha katika picha hii ni jinsi hii miti ilivyo ya kijani pamoja na hali kuwa baridi hivyo.hii imenifanya nihisi labda kabla watu hawajahamia kwenye maeneo yenye baridi kama haya kulikuwa na miti ambayo ilifikishwa kwa upepo(mbegu zake).

     
  • Tarehe: 4:56:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Unknown

    pia haya majengo marefu yanafanana na majengo yaliyokuwa yanajengwa na wakomunist enzi za USSR kwa ajili ya makazi ya watu.majengo hayo yalikuwa yanatenganishwa kwa kuta za box tu hivyo kusababisha jirani kusikia kila kinachotokea nyumba ya pili.

     
  • Tarehe: 6:12:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mwandani

    Kweli wanasiasa wagumu kuwaamini. Naona wanaangalia maslahi

     
  • Tarehe: 7:27:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Jeff Msangi

    Zemarcopolo,
    Hivyo vijialama unavyovyiona kama ramani sio ramani bali ni mabaki ya maji yanayotokana na kuyeyuka kwa barafu.

    Majengo mengi ya huku Kaskazini bado yanajengwa na kitu kama maboxi ingawa nadhani kwa kutumia tekinolojia fulani fulani siku hizi sio rahisi sana kusikia jirani yako anasema nini.Niliwahi kuuliza kwanini nyumba za maboxi nikaambiwa ni kwa sababu ya hali ya hewa,iwe rahisi kuzipasha nyumba joto hususani katika majira ya baridi.Hili nadhani linawapa unafuu wajenzi kwa upande wa gharama.

    Mwandani,
    Hapo ndipo tunapokubaliana kwamba wanasiasa ni wanasiasa tu,popote pale duniani.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker