Wednesday, February 07, 2007
BARAFU BADO IMETANDA!
Kiwango cha baridi hivi leo kilikuwa centigrade -25 kiwango ambacho ni cha juu ukilinganisha na sehemu zingine za Canada ambapo viwango huenda mpaka centigrade -75 na kuendelea.Nimewahi kumwambia rafiki yangu mmoja kwamba haukuwa mpango wa mungu kwa mwanadamu kuishi kona hizi za dunia eti akabisha!.Maisha yaliwezekana vipi zama hizo upande huu wa dunia?Labda ndio maana inasemekana kwamba mabaki ya kwanza ya binadamu yalipatikana kule nyumbani kwetu na kwamba wahadzabe pengine ndio wa ukoo wa Adam na Hawa.
Ukiitizama picha iliyopo hapo juu kwa makini unaweza kuona mambo kadha wa kadha.Unaweza kuyatambua?
Kisha kama ulidhani wanasiasa wa Tanzania ndio pekee wanaokuwa vitimbakwila kwa kurukia chama kimoja mpaka kingine umekosea. Wanasiasa ni wanasiasa tu siku zote.
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 8:31 PM
|
Permalink |
-
niliyogundua mimi ni alama nyingi za miguu kwenye theluji.inaweza kuashiria kuwa watu hucheza hapo au hiyo ni njia.kitu kingine nilichoona ni kwamba hiki kibarabara kina ramaniramani kibao,inagwa sijaweza kugundua zinamaanisha nini.hata hivyo kilichonifurahisha katika picha hii ni jinsi hii miti ilivyo ya kijani pamoja na hali kuwa baridi hivyo.hii imenifanya nihisi labda kabla watu hawajahamia kwenye maeneo yenye baridi kama haya kulikuwa na miti ambayo ilifikishwa kwa upepo(mbegu zake).
-
pia haya majengo marefu yanafanana na majengo yaliyokuwa yanajengwa na wakomunist enzi za USSR kwa ajili ya makazi ya watu.majengo hayo yalikuwa yanatenganishwa kwa kuta za box tu hivyo kusababisha jirani kusikia kila kinachotokea nyumba ya pili.
-
Kweli wanasiasa wagumu kuwaamini. Naona wanaangalia maslahi
-
Zemarcopolo,
Hivyo vijialama unavyovyiona kama ramani sio ramani bali ni mabaki ya maji yanayotokana na kuyeyuka kwa barafu.
Majengo mengi ya huku Kaskazini bado yanajengwa na kitu kama maboxi ingawa nadhani kwa kutumia tekinolojia fulani fulani siku hizi sio rahisi sana kusikia jirani yako anasema nini.Niliwahi kuuliza kwanini nyumba za maboxi nikaambiwa ni kwa sababu ya hali ya hewa,iwe rahisi kuzipasha nyumba joto hususani katika majira ya baridi.Hili nadhani linawapa unafuu wajenzi kwa upande wa gharama.
Mwandani,
Hapo ndipo tunapokubaliana kwamba wanasiasa ni wanasiasa tu,popote pale duniani.
niliyogundua mimi ni alama nyingi za miguu kwenye theluji.inaweza kuashiria kuwa watu hucheza hapo au hiyo ni njia.kitu kingine nilichoona ni kwamba hiki kibarabara kina ramaniramani kibao,inagwa sijaweza kugundua zinamaanisha nini.hata hivyo kilichonifurahisha katika picha hii ni jinsi hii miti ilivyo ya kijani pamoja na hali kuwa baridi hivyo.hii imenifanya nihisi labda kabla watu hawajahamia kwenye maeneo yenye baridi kama haya kulikuwa na miti ambayo ilifikishwa kwa upepo(mbegu zake).