Saturday, February 10, 2007
NJIA YA CHINI KWA CHINI
Ingawa naamini kuna neno toshelezi au tafsiri ya moja kwa moja ya neno "tunnel", kamusi niliyonayo inaniambia kwamba tunnel kwa kiswahili ni "njia ya chini kwa chini". Pichani juu ni "njia ya chini kwa chini" inayoiunganisha majiji ya Windsor,Ontario,Canada na Detroit,Michigan,United States. Njia hii ya chini kwa chini ni ya pekee na kila siku hutumiwa na maelfu ya wakaazi wa Canada wanaovuka mpaka kuingia Marekani na hali kadhalika wakaazi wa marekani wanaovuka kuingia Canada.Inasemekana wapo watu kibao tu wanaishi Canada na kufanya kazi Marekani na pia wamarekani wanaofanya kazi Canada.Kumbuka kwamba nchi hizi zinaruhusu mtu kuwa na uraia wa nchi mbili mchakato ambao Tanzania inaufanyia kazi kwa mwendo wa kinyonga. Michuzi, Maggid na wengineo picha za namna hii mnaziitaje kwenye taaluma yenu?
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 10:33 PM
|
Permalink |
-
Jeff unasemaje kuhusu mtanzania aliye na uraia wa nchi mbili au zaidi kuwa rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania na amiri jeshi mkuu?
-
samahani,hapo juu isomeke jamhuri ya muungano.
-
Zemarcopolo,
Swali zuri sana.Binafsi nadhani mtu mwenye uraia wa nchi mbili asiruhusiwe hata kugombea uraisi achilia mbali kuwa raisi.Na sio uraisi tu bali pia vyeo au nafasi za kazi zozote tunazoweza kuziita "nyeti" ziendelee kushikiliwa na raia wa kuzaliwa huku tukihakikisha vigezo kama hicho cha kutokuwa na uraia wa nchi nyingine yeyote vikitiliwa mkazo na kwa makini.Kwa hali hiyo tume ya uchaguzi itakuwa haina budi kuongeza vipengele kama hivyo kama vile ambavyo hivi sasa bila digrii na umri fulani huruhusiwi kugombea uraisi.Nasikia hata ukiwa huna mke inakuwa ni tatizo kugombea achilia mbali kuongoza nchi.Kwa hiyo kwa maoni yangu,marufuku kuwa raia wa nchi mbili kama unatarajia kuongoza nchi au kuhodhi nafasi yoyote nyeti.
-
Labda niulize kwa vigezo vipi mtu aliyekuwa na uraia wa nchi mbili mojawapo ikiwa Tanzania asiweze kuwa raisi au kiongozi wowote wa juu katika serikali? Hasa ikizingatiwa huyu mtu uraia wake wa kuzaliwa na makuzi ni Tanzania?
-
Halifa,
Jibu rahisi nadhani ni maslahi ya taifa.
-
Waperu wanaweza kutupa jibu zuri la swali hili kwa sababu wana eksipiriensi ya Rais Alberto Fujimori aliyekuwa na uraia wa nchi mbili; Peru na Japan.
Wakati mwingine ukiangalia hata hao wazawa wanaongoza nchi zetu utafikiri hawaongozi kwao.
Masalaamia,
F MtiMkubwa Tungaraza.
-
Mbona kuna watu wenye urais wa nchi moja ambao wanaongoza bila kujali maslahi ya taifa? Hao je?
Jeff: picha hiyo nimeipenda sana maana iko katika hali ya kisanii zaidi.
-
Ndesanjo,
Hao ni wengi na ndio hawa tunaohangaika nao kila kukicha.Hukumu yao inachemka jikoni.
Shukrani kwa kuifagilia picha.
-
Hapo juu nilikosea neno "urais" lilipaswa kuwa "uraia."
Dawa yao sio utani inachemka. Ngoja tu.
Jeff unasemaje kuhusu mtanzania aliye na uraia wa nchi mbili au zaidi kuwa rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania na amiri jeshi mkuu?