Tarehe: 3:32:00 PM, Mtoa Maoni:- MTANZANIA.
Tarehe: 1:22:00 PM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 1:45:00 AM, Mtoa Maoni:- Patrick G. Kamera
Jeff,
Wakati mwingine inabidi mtu ukubali yaishe maana ukibebea bango sana hizi sikukuu utajikuta unajenga hoja dhaifu kuzishutumu, halafu matokeo yake ukaonekana mlalamishi bure.
Kwa mfano unapodai kuwa kwa nini kuwe na siku moja tu ya kuonyeshana mapenzi na mwenzako ukimaanisha Valentine's day hiyo kwa inakuwa siyo sahihi na wote tunafahamu hilo, mapenzi mnaonyeshana kila siku ila hiyo siku moja ni kama tu ya kuenzi jambo hilo.
Hoja unayotoa ni sawa na kusema hata sikukuu zingine tusiziadhimishe mfano siku ya Kupambana na Ukimwi duniani ni Desemba mosi, lakini Ukimwi watu wanapambana nao kila leo sio siku hiyo tu(tena kadi za siku hiyo japo haijavuma sana si ajabu zikaanza kuuzwa) Hivyo Desemba mosi ni siku ya kuenzi hilo suala la kupambana na ukimwi.
Mfano mwingine, pamoja na kuwa kuna "Siku ya Wanawake" haina maana kuwa siku nyingine zote wanawake hawatakiwi kuthaminiwa. Mifano ipo mingi tu ambayo ukiangalia unaweza kuona uwiano.
Pili, katika ulimwengu wa leo karibu kila kitu ni biashara, pesa mbele. Wafanyabiashara hawajali ni siku gani we ukisema tu "siku fulani sikukuu" kosa... wao wanatafuta njia yoyote ile ya kutengeneza pesa.
Sijui kama kuna siku ya ku-blog duniani? kama haipo basi siajabu inakuja lakini haitakuwa na maana kwamba siku zingine zote hutakiwi ku-blog. Nadhani umenipata.
Cha msingi ni kuzitumia siku hizo kwa manufaa na siyo lazima uingie gharama yoyote ile.
Tarehe: 1:15:00 PM, Mtoa Maoni:- Jeff Msangi
Patrick,
Kwa bahati nzuri au mbaya msimamo wangu ni huu huu hata katika hizo sikukuu zingine ulizozitaja.Kwa makusudi au kwa kuzidiwa na utandawazi,tumezifanya siku hizo kupoteza maana.
Hoja ya msingi ni kwamba siku hizi zimeshapoteza maana tofauti na ilivyokuwa.Sio jambo baya kuwa na siku fulani ya maadhimisho au kilele.Tatizo linakuja kila kitu kinapogeuzwa kuwa "biashara" kama ilivyo hivi sasa.Tunajivika unafiki huku tukitambua.
Pia lazima tukumbuke kwamba kuna watu ambao husahau kila kitu kuhusu jambo fulani (mfano mapenzi kwa mwenzio,kwa wazazi,ukimwi,uungawana,amani,uhuru nk) mpaka siku ya maadhimisho.Badala ya mambo haya kuwa ya kudumu yanageuka kuwa ya mara moja kwa mwaka kivitendo na hata tafakuri.Hapo ndipo utakapokuta kwamba watu wanasahau kwamba harakati au mapambambao dhidi ya ukimwi kwa mfano ni za mwaka mzima na sio Desemba mosi peke yake.Mifano ni mingi Patrick.Siwezi kukubali yaishe kwa sababu naamini tunahitaji kukumbushana kwamba kwa namna fulani wanadamu tunapoteza muelekeo.
Tarehe: 11:48:00 AM, Mtoa Maoni:-
Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe cha kusimama peke yangu bila mwili wa kusimama na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na Dk DAWN, baada ya kumwambia. kuhusu hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kiukweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi huku akiniomba kuwa hatoniacha kamwe. tena. Miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
* upendo
inaelezea * inaelezea kivutio
* kama unataka ex wako nyuma
*acha talaka
*kuvunja mawazo
* huponya viharusi na magonjwa yote
* uchawi wa kinga
*Ugumba na matatizo ya ujauzito
* bahati nasibu
* bahati nzuri
Wasiliana na Dk Ediomo kwenye barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp:+2349046229159
Ni hatari Msangi!
Siku hii imegeuka kuwa siku ya maambukizo.