VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Tuesday, March 13, 2007
BARIDI INAPOANZA KUPUNGUA.......

Hali ya hewa ni habari kubwa sana katika hizi nchi za magharibi.Kuna watu ambao hutazama luninga ili tu kupata utabiri wa hali ya hewa!Siku hizi hata mimi hujishtukia nikizingatia kwa makini utabiri wa hali ya hewa tofauti na nilivyokuwa kwetu.Sina uhakika kama huu ndio ule utaratibu wa "ukikuta wenzio ni chongo na wewe fumba jicho moja" au la!Usishangae sana basi kuona kwamba mara kwa mara nimekuwa nikikuhabarisha au kukuletea picha za hali ya hewa kutoka hapa.

Nilipokuwa Tanzania jamaa wa hali ya hewa walikuwa wakishaanza utabiri wao baada ya taarifa ya habari ungetarajia mambo mawili yatokee;nizime televisheni au nibadili channel.Inawezekana kwa sababu hadithi yao kila siku ilikuwa ni ile ile..."kanda za juu kusini mvua za hapa na pale, mikoa ya Dar-es-salaam,Pwani,Morogoro itapata mawingu na mvua za rasha rasha".Tofauti na kwetu ambapo masuala ya hali ya hewa huwekwa mwishoni hapa wakati mwingine(kama sio mwingi) hali ya hewa huwa ndio "breaking news".Huwa inatokea jamaa wakautisha umma mzima na wala hali ya hewa isiwe mbaya kama walivyosema.Bahati nzuri au mbaya ni kwamba utabiri wa hali ya hewa ni mojawapo ya taaluma chache sana duniani ambapo mtu anaweza kukosea na wala asiwajibike kwa yeyote.

Hivi sasa baridi imeanza kupungua.Majira ya baridi kali ndio yanayoyoma ili kupisha masika za huku kabla ya kuyakaribisha majira ya joto (summer). Jambo moja la aina yake huku ughaibuni ni jinsi maduka yanavyobadili bidhaa kuendana na majira yaliyopo. Hivi sasa ukienda madukani karibuni kila kitu cha kusaidia kupambana na baridi kama masweta,makoti nk vishaondolewa kwenye shelves. Msimu mpya vitu vipya.Hii ni tofauti kabisa na kwetu ambapo bidhaa nyingi hudunda dukani miaka nenda,miaka rudi mpaka atokee atakayezinunua. Hapa nakumbuka jinsi lile duka la "mangi" pale mtaani kwetu lilivyosheheni bidhaa hususani alipoacha kutukopesha!

Pichani juu ni mall kubwa ijulikanayo kama Eaton Centre iliyopo jijini Toronto ambayo huhesabika kama mojawapo ya vivutio vikubwa vya utalii.Huko ndipo wengi wanapoelekea ili kujiandaa kwa majira yanayokuja.Kazi kweli kweli.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 11:42 AM | Permalink |


Maoni: 1


   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker