Tarehe: 9:26:00 PM, Mtoa Maoni:-
Tarehe: 6:47:00 PM, Mtoa Maoni:-
ukiwa europe maeneo ya UK deni linafutwa baada ya miaka 6 na unakuwa safi bila na ata deni moja baada ya hapo.
Njia nyingine ambayo kama hautaki kusubiri miaka 6 ni kujitangaza bankruptcy na kufutiwa madeni yote na kuanza upya ingawa itakuwa vigumu kupata mikopo tena.
Njia ya kwanza ukifuata utapata tena mikopo.
Tarehe: 5:12:00 AM, Mtoa Maoni:- MACHWEO
Ngurumo anashangaa kuhusu wafanyakazi wenye mshahara mdogo lakini wanamiliki zaidi ya kile kinachomaanisha mshahara wao! Nyote si wageni na wala si lengo langu kuonesha kuwa rushwa afrika inatula na kuwaneemesha wachache huku wengi tukiwa tunaumia kwa kukosa muhimu yaliyokombwa kwa rushwa. Mshahara kwa baadhi ya wafanyakazi si kitu, kinachothaminiwa sasa ni nafasi uliyopo inakuwezesha 'kuwasiliana'. Mikopo ipo lakini si wote wanaoweza kuipata hasa wale walio mbali na jiji na miji mikubwa
Tarehe: 2:21:00 AM, Mtoa Maoni:- Patrick G. Kamera
Mzee Jeff,
Sijaona sababu ya msingi ya "kukerwa" na mtu kukuambia mambo yake safi kwa kuwa kanunua au "kakopeshwa" nyumba.
Kama unavyofahamu piga ua ukiishi huku "ughaibuni" lazima utakuwa unalipa pango au mortgage, sasa kama utaishi miaka kadhaa, kipi bora, kupanga nyumba au "kukopa" nyumba? Vile vile kumbuka kuwa hiyo nyumba ukiamua kuiuza kabla ya kumaliza deni bado utaondoka na kianzio kizuri tu kwa hiyo bado utakuwa unapeta si unajua masuala ya equity(I guess ndio "mambo ya mtu kuwa safi" hayo) tofauti na ukipanga ambapo utaondoka mkavu!
Nakumbuka Tanzania tulikuwa na benki ya nyumba (THB) ambayo ilikuwa inatoa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba, leo hii ni historia...
Ujenzi wa nyumba Tanzania uzuri wake ni kuwa ukimaliza huna deni ila ukijenga kwa mshahara wa serikali kihalali si ajabu ukamaliza baada ya miaka kibao vilevile au ukahamia na wala usiimalizie nyumba ukakubali tu yaishe. Ila ukiwa na mshahara wa NGO au mashirika ya nje au ukiuza nyumba yako huku ukadondoka na kianzio chako basi ujenzi utamaliza mapema mradi kusiwepo na migogoro ya viwanja.
Kwa habari za runinga za magharibi kuhusu Afrika ni ukweli usiopingika kuwa hawataki kuonyesha mambo mazuri, wao wanataka watazamaji, wasikilizaji na wasomaji wao huku waendelee kuwa na picha potofu ya Afrika ili wao waendelee kupeta.
Hushangai wanaweza kuonyesha watu wako hoi bin taabani yaani hali mbaya kweli, mazingira machovu mno ila hawaonyeshi wao waandishi wa habari na wapiga picha wao wamefikia wapi na wanaishije kwenye hizo hizo nchi za Kiafrika wanajua wakifanya hivyo tu hata zile "hardship allowances" zitapungua kama siyo kufutika kabisa, hivyo wao pia wametanguliza maslahi yao binafsi mbele.
Nakumbuka Will Smith aliwahi kusema kwenye interview moja baada ya kutoka Afrika Kusini kuwa hakutegemea kuona maendeleo aliyoyaona maana alivyofundishwa toka mdogo shuleni ni kwamba Afrika kuchovu sana alisema "I was misinformed to the point of being lied to" na tangia hapo akaamua kuwa atakuwa anapeleka familia yake kutembea Afrika mara kwa mara ili watoto wake waujue ukweli na nadhani amenunua nyumba huko Afrika Kusini, sasa huyo ni mmoja tu, wako wengi bila shaka.
Tarehe: 2:51:00 AM, Mtoa Maoni:- mloyi
Imekuwa zaidi ya habari kubwa kupigwa kwa kibaraka wao zimbabwe! sijui kama wakitokea watu waanze kuandamana Newyork, Montreal, London na kwingine kwa aina hiyo kwa lengo la kuiangusha serikali kama watatoka salama!
Kumbuka historia ya London, Liverpool miaka ya mwisho ya sabini na mwanzoni mwa themanini, weusi walipoandamana kudai kutendewa haki kama wengine polisi walifanya nini? Marekani ndiyo usiseme, Juzijuzi kijana wa kibrazil katwangwa risasi kwa kukataa kusimama aliposimamishwa na polisi, mwaka jana/juzi ufaransa waliwafanyia nini wageni waliokuwa wanaandamana kupinga hali wanazowekwa, bado hatujasahau mambo ya Denmark wiki iliyopita wananchi walioandamana kupinga kuvunjiwa nyumba zao, Iraq na Afghanistan mambo yanyofanyika huko hawayasemi kwa undani. Haya yote hayakuwa habari kubwa ila ya kupigwa kwa Morgan ndiyo ipewwe nafasi kubwa kiasi hicho au ilitumika kufunika mambo ya Denmark?
Wanatakiwa wajue historia ya Zimbabwe na kwa nini Mugabe wanayemchukia anashinda uchaguzi ndiyo wafikie maamuzi yao.
Tarehe: 10:45:00 AM, Mtoa Maoni:-
Mloyi, UMENENA.
TUSIWE BENDERA KUFUATA UPEPO, MUGABE KWELI NI MZEE, LAKINI MSIMAMO WAKE, MIMI SINA WASIWASI NAO. HAPENDI VIBARAKA.
ETI THAMANI YA FEDHA IMESHUKA KWA ASILIMIA 1700.
SHVANGIRAI ATAIPANDISHA KWA VIPI!
YAANI KWA MISAADA! AU!
HAKUNA MWANAUME YEYOTE CHINI YA HII MBINGU ATAWEZA KUKUSAIDIA HIVI HIVI, LABDA NDUGU YAKO KWA BABA NA MAMA MJOMBA AU SHANGAZI. ETI bush AMSAIDIE sadamu sorry osama HIVIHIVI!!
NI SASA TU WANAMPENDA AKISHIKA MADARAKA WATAMPELEKESHA HADI AHISI JOTO.
Tarehe: 11:52:00 AM, Mtoa Maoni:-
Mtukweli...
'Mr. President how is Tanzania'
Jaribu kufikiria kile alichokuwa akikisema mh. JK ktk mfululizo wa ziara zake nje. Nakumbuka ya nchi za scandnavia. 'Tanzania imepiga hatua, tumepunguza vifo vya kina mama kwa asilimia ..., tumepunguza vifo vya watoto wanapozaliwa kwa asilimia..., tumepunguza maambukizi ya maleria kwa asilimia..., ukimwi bado ni janga la kutisha, nchi ilikumbwa na ukame uliyosababisha upungufu wa chakula, ukosefu wa umeme n.k' Maana ya kutamka haya ni kuwa mwisho wa siku unaambiwa chukua hizi 10bill. za ukimwi, hizi 5bill za maleria, si hapo amefanikisha ziara yake?
Nani unafikiri ataongelea mazuri ya kwetu wakati tunatangaza shida zetu kila kukicha. Hivi bonde la usangu kuzalisha chakula mpaka tukamtafute mtu Canada?
Ebu wale wataalam wa kuimbisha waniambie ukimtokea binti kwa sifa nyingi na pesa maana yake ni kuwa akuchukuliye hivyo au? kama tumetanguliza shida zetu nje nani akuelezee juu ya mazuri yako ya ndani? Ndugu yangu kweli mazuri yapo juu ya nchi yetu, may be kwenye utalii, ukimaliza utalii unaongelea lipi? Elimu, UD watu wanafurika class mpaka nje, Usafiri, tumekodi Air Malawi, Ferry shida, Barabara Foleni Hiyo kwa Dar, mikoani Rami unaisikia tu, Reli choka mbaya, Chakula hatuna uwakika wa miaka 2, Maji shida, vitu feki kibao, low quality za waindi kibao, Uwezo wa uvumilivu kwa wanasiasa ni 0 kila mmoja anataka kuwa CCM, Uwezo wa wannanchi kutetea haki zao na kuhoji bungeni 0,uchumi upo Dar tu? Huko upcountry hakuna Rais, wanaongozwa na media. Hivi unajua Bongo yetu Familia ya watu 50, akifaulu dogo kwenda sekondary uko bushi kwenye watu 49, kama wewe wa Dar ujatoa mkwanja hakuna shule? tena hela yenyewe elfu 20.
Hawa wa Magharibi huwenda hawakosei, maana hayo mabovu ndo yanacoverage kubwa, kwani ndugu yangu yakitoweka watabaki kimya si itakuwa heri kwetu?
Jeff, ni kweli. Unakumbuka Mwalimu Nyerere alikopa pesa benki kujenga nyumba yake ya Msasani? Deni lilikuwa gumu hadi 'akaona watoto watakufa njaa,' akaomba serikali iijenge na kuimiliki nyumba hiyo iwe ya rais, si Nyerere. Lakini serikali ya Mwinyi baaday eiliona aibu, ikampa kama zawadi nyumba hiyo. Nyerere alikuwa na uwezo wa kujenga bila mkopo, kwani raslimali za taifa zilikuwa nje nje, miongoni mwa wajinga. Hakufanya hivyo. Aliweka mfano ambao waliomfuata hawakuufuata. Siku hizi watu (maofisa wa serikali) wanaolipwa shilingi laki 2 kwa mwezi, wanajenga nyumba kubwa za kifahari bila mkopo benki na bila deni na mtu yeyote. Wanazipata wapi? Ni zao? hapo ndipo tulipo!