"You can become whoever or whatever you want to be,just put your mind into it".Nausikia msemo huu kila mara katika matamasha ya kuhamasisha vijana ninayohudhuria mara kwa mara hapa Marekani ya Kaskazini.Endapo unahisi kukata tamaa ya maisha ni dhahiri kwamba msemo kama huo hapo juu unaweza kubadilisha japo theluthi ya mawazo yako.
Pamoja na hayo sijawahi kufikiri au kudhani kwamba kumbe "kuwa chochote au yeyote" ni pamoja na kuweza kuwa kitu kama "Yesu" kama ambavyo jamaa mmoja anayeishi huko Houston,Texas,nchini Marekani anavyodai. Waumini wake wanazidi kuongezeka siku baada ya siku.Ile hadithi ya kufa,kufufuka na kisha kupaa mbinguni ya yule Mnazareti ni kama ngonjera kwa waumini hawa.Yesu wao yupo hai na anaishi,anadunda na kunywa mvinyo kwa raha zake.Some habari hii kwa undani hapa.
Nilimuona huyu Yesu wa Texas akihojiwa. Nikaona na hizo zawadi anazopewa na waumini wake.
Imani kitu hatari sana. Imani bila mantiki.