VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Friday, April 20, 2007
923 MILIONI WANAISHI KWENYE SLUMS,NINI MCHANGO WAKO?

Zaidi ya watu milioni 923 duniani wanaishi katika maeneo ambayo kwa kiingereza yanajulikana kama “slums”.Tafsiri rahisi ya neno slum ni makazi ya binadamu yasiyo na huduma muhimu za kijamii kama maji, vyoo, ulinzi na huduma nyingi nyinginezo za kiserikali na kijamii.Unaweza kujiuliza, kwa tafsiri kama hiyo hapo juu ni maeneo mangapi basi, kwa mfano nchini kwetu Tanzania ni slums?

Eneo liitwalo Kibera nchini Kenya, nje kidogo tu ya jiji la Nairobi ndilo linasemekana kuwa ni slum kubwa kushinda zote duniani.Karibuni watu robo tatu ya milioni wanaishi Kibera. Kule India eneo lijulikanalo kama Dhavari, pembezoni mwa jiji la Mumbai (zamani Bombay) na eneo liitwalo Orangi, pembezoni mwa jiji la Karachi nchini Pakistani yanafuatia kwa ukubwa wa slums kubwa zaidi duniani.Magharibi mwa Afrika,nchini Ghana, katika jiji liitwalo Tema kuna slums zijulikanazo kama Ashaiman.Ukubwa wa slums hizi inasemekana ni ukubwa wa jiji kabisa- slum city.Jijini Dar-es-salaam maeneo mengi ya nje ya jiji yanazidi kugeuka kuwa slums hususani tukizingatia ukosefu wa huduma muhimu za kijamii kama hizo nilizozitaja hapo juu.

Sababu kubwa ya kuwepo na kuongezeka kwa slums duniani ni umasikini jambo ambalo linachangiwa moja kwa moja na sera mbovu za kiserikali katika masuala ya uchumi, utandawazi ambao nchi zetu kwa mfano zinazidi kuukumbatia bila kufanya utafiti wa kina, sera za ubepari mamboleo zinazotungwa na mashirika kama IMF na wenzake nk. Ubinafsishaji wa mashirika ya umma kwa mfano ni sababu kubwa ya kuongezeka kwa ukosefu wa ajira= umasikini= kuishi kwenye slums. Kwa ufupi watu wengi wanavutwa kukimbilia mijini kwa sababu ya ukosefu wa huduma za jamii vijijini, ukosefu wa ajira nk jambo ambalo wanakutana nalo tena wanapofika mijini.Wakifika huko mijini wanakutana na mipango hovyo na sera mbovu zinazohusu makazi ya binadamu.

Yapo mambo kadha wa kadha ambayo sisi kama wananchi tunaweza kufanya ili kuhakikisha kwamba makadirio ya kwamba kama hatua za dhati zisipochukuliwa,ndani ya miaka 30 ijayo, takribani watu bilioni mbili watakuwa wanaishi katika slums, yanapunguzwa kama sio kusahaulika.Inawezekana kabisa nikawa mimi au wewe, ndugu na jamaa zetu,watoto wetu na hata wajukuu wetu. La kwanza ni kumuuliza mbunge wako juu ya mipango halisi ya serikali katika kutokomeza umasikini na kama wanayo mipango endelevu ya kuhakikisha kwamba idadi ya watu inaendana na huduma za jamii.Usingoje mpaka wakati wa uchaguzi kuhoji mambo haya.Pili ni kuunga mkono shughuli za mashirika yasiyo ya kiserikali kama lile la Shack/Slum Dwellers International (SDI). Tawi lao nchini Tanzania ni hili hapa.Mashirika kama UN Habitat ambalo linaongozwa na mtanzania mwenzetu, Prof.Anna Tibaijuka, nayo yanamipango fulani fulani mizuri ya makazi ya binadamu.

Pichani juu ni makazi ya binadamu jijini Dar-es-salaam, eneo lijulikanalo kama Magomeni Kota.Picha kwa hisani ya Maggid Mjengwa.



 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 10:31 AM | Permalink |


Maoni: 2


  • Tarehe: 3:19:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    tunaomba mchango wako hapa https://www2.blogger.com/comment.g?blogID=17229004&postID=2228567355941212162

     
  • Tarehe: 10:02:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Anony,
    Asante kwa kunialika ili nichangie katika hiyo link uliyonipa.Kwa bahati mbaya nimeshindwa kukipata vizuri kiungo hicho.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker