VIJIMAMBOZ PROUD AFRICAN KASRI LA MWANAZUO BONGOCELEBRITY NKYA MAWAZO NA MAWAIDHA JIKOMBOE MIRUKO NDABULI SHAMIM ZEZE DAMIJA MATERU MLOYI CHEMI CHE MPONDA BAKANJA MTAFITI LUKWARO MSANGI MDOGO MARK MSAKI DIRA YANGU MWAIPOPO KONA YANGU FURAHIA MAISHA YAKO DAMIJA MICHUZI FATHER KIDEVU MWANDANI NGURUMO FATMA KARAMA ZAINAB OMEGA NGOLE YAHYA CHARAHANI JARIDA LA UGHAIBUNI NYEMBO BWAYA BHALEZEE JUNGU KUU WATOTO WETU BLG BROTHER SAA YA UKOMBOZI NURU AKILINI TAFAKARI ZA MAISHA ALBERT WILSON UCHUMI MIDRAJI IBRAHIM Lucassano CHESI HAKI NGOWI KISIWA CHA AMANI Innocent Kahwa SULTAN TAMBA SIMON KITURURU MAVIZO MUSA NGARANGO KIJIWENI(NED) WATANZANIA JADOUNG METTY MAGGID MJENGWA SAHARAN VIBE MWENYE MACHO ABDALLAH MRISHO MYAFRICA SHERIA NA MAVAZI
NEW VISION UGANDA MONITOR UGANDA KENYAN NATION MEDIA EASTANDARD FROM AFRICA BUSINESS WEEK ALL AFRICA
MAGAZETI YA IPP UHURU NA MZALENDO BUSINESS TIMES DAILY NEWS TANZANIA DAIMA MWANANCHI BUNGE LA TANZANIA SERIKALI YA TANZANIA IPS INTERNATIONAL
AFRIKA HURU NINI KILITOKEA PAMBAZUKA DUNIA YETU GADO CARTOONS
SEND ME AN E-MAIL
Tuesday, April 24, 2007
UNAONA NINI KATIKA PICHA HII?

Pichani ni watoto-wanafunzi wa Shule ya Msingi Kibogwa iliyopo katika tarafa ya Matombo mkoani Morogoro.Itazame kwa makini picha hii, double click juu kwenye picha yenyewe ili uione vizuri zaidi. Huu ni mfano mmoja kati ya mingi sana nchini mwetu. Hivi ndivyo tunavyoiandaa Tanzania ya leo. Ewe raisi wa nchi,ewe waziri, ewe kiongozi,ewe mwananchi mwenzangu,unajisikiaje kuona hali kama hii? Nini thamani ya uongozi wako?Nini thamani ya ubinadamu wako?

Picha imepigwa na Mathew Kwembe na nimeipata kupitia kwa Yahya Charahani.
 
Muandishi: Jeff Msangi |Tarehe: 9:44 AM | Permalink |


Maoni: 19


  • Tarehe: 10:41:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Picha kama hizi tunazihitaji sana maana ni kielelezo cha ukweli unaofichwa na majengo marefu ya kisasa Dasalama na magari ya kifahari. Hawa ndio watanzania wenzetu waliosahaulika. Watanzania tunaopenda kuwasahau.

     
  • Tarehe: 10:45:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Jeff,

    Mimi kitu cha kwanza kilicho nishangaza kwenye picha hii ni kuwa hakuna mwalimu na pia hakuna miandiko kwenye bao. Sasa ninafaikira kama hawa wanafunzi teyari wana matatizo na vifaa vya shule kama madaftari,vitabu, madeski, viti na kadhalika, basi angalau kungekuwa kuna walimu ingesaidia kidogo. Nime sikiwa kuwa huko vijijini kwa sababu ya Ukimwi, walimu wengi sana wamefariki na kuwa ni tatizo kubwa sana kupata walimu wengine wipya. Kusema ukweli kama watu wanasema "the future is in the hands of the children" na future yenyewe ndioo hii tuta wategemea hawa vijana kuijenga Tanzania, basi tume umia sana na pia society yetu tume feli na tuna zidi kufeli.
    Ina sikitisha sana sana.

     
  • Tarehe: 11:00:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Aisee Jeff,
    Umenigusa kweli na picha hii. Ukweli ni kuwa mbunge anayeliongoza jimbo hilo la Moro Kusini Mh Hamza Mwenegowa aliwahikuwa naibu waziri wa Ujenzi katika serikali iliyopita.Hakika huwezi amini katika kipindi chote alichowahi kulitawala jimbo hilo tangu aliporithishwa na mbunge aliyemtangulia miaka mingi iliyopita hajawahi kufanya lolote.Katika uchaguzi wa mwaka 2000 muheshimiwa huyo aliongoza kwa kuranyingi sana katika tarafa hiyo ingawaje hakuna lolote jema analolifanya kwa watu hao. Ieleweke wasomi wengi wa asilia ya kiluguru wanatoka katika tarafa hiyo na hata wengine bado wanapeta katika medali ya utawala.Hebu watumie nakala hii iwatie aibu maana hata kamishina mkuu wa magereza nchini Tanzania ni mwenyeji wa mahali hapo, wachilia mshika fuko la misaada ya tanzania pale hazina ambaye ni mtu wa hapohapo.

     
  • Tarehe: 11:03:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Simon Kitururu

    Inasikitisha sana!Halafu ni ukweli karibu sisi Watanzania wengi wakawaida tuna mpaka ndugu kabisa ambao wanasoma katika mazingira haya.Nakumbuka vilevile mitaa hiyo.Niliwahi kufanikiwa kufanya kazi kama tour guide nilipokuwa O-level , Morogoro Sekondari. Kipindi hicho nilitembelea vijiji vingi sana Morogoro.Hali ilikuwa mara nyingi kama hivyo picha ionyeshavyo. Halafu pia unakuta watoto wengi ukiachilia kukosa vifaa vya shule, pia wana njaa.Kuna umuhimu wa kila mtu kujitahidi kusaidia, kwa sababu mchango wa kila mtu ni muhimu. Lakini kwa kila mtu binafsi kusaidia kienyejienyeji haitoshi. Inatakiwa kuwepo na mfumo (infrustructure) unaoweza kusaidia kutatua tatizo kama hili kwa muda mrefu.Inasikitisha kuwa katika mfumo wa elimu wa Tanzania, hata huko chuo kikuu kwenyewe matatizo bwelele.Halafu eti hawa wanafunzi wa vijijini , wasomao kwenye mazingira haya wanategemewa wanaweza kufika kwenye elimu ya juu!Inasikitisha kwa kweli.

     
  • Tarehe: 11:07:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    It's hard to believe that this is 21st century. I know it's true, can't say much. It is "nature's call".

     
  • Tarehe: 1:05:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Kwanza, asante Jeff kwa kutukumbusha yanayojiri kule tulikotoka. Hali hii ni yakusikitisha sana ukizingatia kuwa hao unaowaona hapo ndio taifa la kesho. Tulipopata uhuri Mwalimu Njerere alisema tulikuwa na maadui watatu: umasikini, ujinga na maradhi, na akatangaza vita dhidi ya maadui hao. Sasa kama vita dhidi ya umasikini na ujinga inapigwa kwa kuwasomesha watoto juu ya mawe, nafikiri huu ni unafiki usio na kifani. Tena Mwalimu alisema kwa vile wenzetu wa nchi zilizoendelea wametuacha mbali, inabidi sisi tukimbie wakati wao wanatembea. Sasa naona sisi tunawafanya taifa la kesho wakimbie kuelekea juu ya mawe wakati wenzetu wanatembea kwenye technolojia za kileo (’high-tech’). Tutafika kweli? Tulipoanza karne hii, Mheshimiwa Rais Mkapa naye alisema lazima ’tuanze karne hii ya sayansi na teknologia kwa mbwembwe’. Kama mbwembwe zenyewe ndio hizi, basi tuna matatizo makubwa. Sasa hivi nchi yetu imeingia kwenye Sera za uwekezaji. Tunaalika makampuni kutoka nje kuja kuwekeza kwenye migodi, mabenki, n.k. Kwa misemo ya kitaalamu, tunajenga kitu kinachoitwa ”financial capital”. Na pia tunajenga miundo mbinu kama barabara, mitangao ya simu, n.k: hii huitwa ’physical capital”. Haya yote ni muhimu kwa maendeleo, lakini tunasahau kwamba, kwa nchi yoyote kuweza kuendelea uwekezaji ulio muhimu sana ni ule wa kuwekeza katika watu, yaani ”human capital”, ambayo hufanyika kwa kuwaelimisha watu. Nchi zote zilizoendelea, ikiwa za Magharibi na hata hizi nchi za Asia zenye uchumi ukuao haraka (Asian Tigers) kama vile Korea, Taiwan, na Singapore, ziliwekeza sana katika elimu. Kwa hiyo kama sisi tutaendelea kudorora katika sekta hii, basi hata juhudi tunazofanya ni mbio za sakafuni ambazo huishia ukingoni. Mimi nakumbuka nilipokuwa nasoma Chuo Kikuu Sokoine (Morogoro), niligoma mara mbili na tulikaribia kufukuzwa chuo. Tatizo? Tulikuwa hatuna viti vya kutosha kwa hiyo wanafunzi wengine walikuwa wanahudhuria darasa na kumsikiliza mwalimu wakiwa wamesimama. Sasa kama wanafunzi wa chuo kikuu wanasoma hivyo, kweli tuko makini jamani? Ukienda kwenye shule za msingi najua ziko nyingi tu zenye hali ya kusikitisha. Nafikiri viongozi wa nchi yetu inabidi wakae chini wajiulize tena: je ile vita dhidi ya umasikini, ujinga na maradhi tunaishinda? Mimi nafikiri maadui hawa sasa wanatutafuna mpaka mifupa.

     
  • Tarehe: 4:05:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Mija Shija Sayi

    Kama ni kusema, tumesema sana lakini sioni dalili ya waliopewa jukumu la kusimamia maendeleo ya wananchi wakishughulika na lolote, hali ndo inazidi kuwa kama tunavyoiona picha.

    JUMUWATA, mnaonaje tukiamua kuonyesha mfano? tutengenezeni fungu la kuisaidia jamii.

    Hali hii inakatisha tamaa, ninaamini kati ya hao watoto kuna wenye vipaji maalumu, lakini kipaji bila kufufuliwa hufa bila taarifa.

    Kazi kwetu, ni lazima tufanye jambo.

     
  • Tarehe: 7:27:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    HIVI NI VITU VYA KAWAIDA,WATANZANIA ASILIMIA 99.92% WAMEIPITIA.HAKUNA KITAKACHO FANYIKA
    ILA WEWE ULIYEWEKA PICHA HII KATIKA BLOGU HII ULUDI TANZANIA NA UGOMBEE UBUNGE SEHEMU YEYOTE TANZANIA,ILI TUWEZE KUONA MAMBO YAKO.LAKINI HAPA NI UWANJA WA COMMENTS TU HAMNA CHA ZAIDI.COMMENTS SIKIFIKA 200 KUHUSU HILI SWALA LA MADENTI KUKAA CHINI.UTAANZA KUSIFIKIA BLOGU YAKO.MENGI YAMESEMWA NA MENGI HAYAJAFANYIKA,MIMI NINAVIONA NI KAWAIDA MPAKA MUDA WANGI UFIKAPO.
    WATANZANIA WENGI SANAAA KUANZIA MIAKA 1990-2007 WAPO NJE YA NCHI
    WAMEKATILIA NJE.NCHI INAYOONGOZA KWA WATANZANIA WENGI DUNIANI NI UINGEREZA IKIFUATIWA NA MAREKANI NA AUSTRALIA.SASA HAWA WATU WOTE WANAZALIANA NJE YA NCHI WAKIZEEKA HAWAWEZI KUIJENGA TANZANIA KWANI WALIKWISHA ISAHAU TANZANIA.
    WATOTO ZAO WOTE WAMEZALIA UGHAIBUNI.KWA HIYO SIO WATANZANIA .
    UKIWAAMBIA TWENDENI KUMSALIMIA BIBI YENU ,WANAKUJIBU WEWE BABA UMECHANGANYIWA!!!HEBE TUPELEKE DISNEY WORLD (FLORIDA)
    BARAKA UBAMA ALIZALIWA NJE YA KENYA.LAKINI LEO ANAGOMBEA UONGOZI NJE YA KENYA,HUU NI MFANO MZULI.BABA YAKE ALIPORUDI KENYA HAJAFANYA CHOCHOTE KWANI ALIPOTEZA MUDA MWINGI SANA NJE.
    KWA HIYO VIJANA WATANZANIA WENYE HASIRA NA MACHUNGU YA TANZANIA RUDINI NYUMBANI KWANI MUMEKWISHA YAONA MENGI HUKO NJE.HAKUNA KIONGOZI WASASA ATAIBADILISHA NCHI.

    NYERERE ALIKAA NJE YA NCHI NA KURUDI TANZANIA MARA MOJA,KWANI ALIKUWA NA UPEO.WATOTO ZAKE WALISOMA SHULE ZA SERIKALI,NDIO MAANA LEO TUNAONGEA KISWAHILI BILA HIVYO TUNGEKUWA TUNACHINJANA KILA KUNA KWA SASA KUNA MAKABIRA KAMA 159 TANZANIA LAKINI TEACHER ALITUTEACH LUGHA MOJA SOTE.

    KULIKUWA NA VITU VINGI SANA TANZANIA SASA VIMEPOTEA.KULIKUWA NA MADUKA YA RTC KILA MKOA KWISHIRIA MBALI,VIWANDA VYA KUTENGENEZE MAFUTA YA KUPIKIA KWISHIRIA MBALI,ALIJENGA SHULE NYINGI SANA ZA SEKONDARI SASA ZOTE ZINAYUMBA.

    UNAKUMBUKA USEMI HUU "TEMBEA UONE"JULIUS K.NYERERE
    SASA HIVI USEMI HUU UMEGEUKA UMEKUWA "ZAMIA UONE" JAKAYA M.KIKWETE AKIWAAMBIA WATANZANIA WA NJE WAZAMIE HUKOHUKO ILI WAO WAFAIDI

    RUDI NYUMBANI KAKA KUWA KAMA ISSA MICHUZI.
    KWAKHERINI
    WENU RAIS WA TANZANIA 2020-2040

     
  • Tarehe: 9:12:00 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Sam GM

    Jeff,

    Maswala mengine hayahitaji msaada toka UN au umoja wa ulaya kujenga shule inauzi kama viongozi wetu wanasema hawawezi endesha vokswagen kutokana na hadhi yao hivyo wanateketeza pesa kwenye mashangingi. Kama kungekuwa na utaratibu wa kupanga na kuyapitia yaliyopangwa kuhakikisha yanatekelezwa isingekuwa ngumu kujizatiti kwa vitu vidogo kama hivi.

     
  • Tarehe: 1:56:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Jeff
    Let's face it, hali ilivyo yeyote atakayeongoza ile nchi hawezi kufanya chochote bila kufanya mabadiliko ya kisheria. Lazima kuwe na chombo chenye madaraka ya zaidi ya Rais ambacho kitamuwajibisha yeyote atakaye vunja sheria au kutumia madaraka yake vibaya. Kama vile Marekani, kuwe na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wa ngazi ya juu wakitumia madaraka yao vibaya. Kwa sasa hata aje malaika, sisi ni binadamu lazima tuseme ukweli. Anayefuja mali ya umma, akiwa ndio alikufanyia kampeni na leo JK unaitwa Rais hata kama atahusika kwenye wizi wakati wa ununuzi wa mitambo ya RADA, umeme wa Richmond, aue kwa ukatili halafu isemwe hakukusudia (list inaendelea mpaka lyamba), yote ruksa tu. Let's face it nani atajaribu hata kuinua kidole?. Hali ilivyo Bongo, professionals wote wanahamia CCM kuwa wanasiasa, maana unakula unaiba hakuna atakayekufanya kitu. Kwa nini ukazanie ku-assemble SCANIA wakati "wakubwa" wakija watasema sasa Bakari ebu lete F*dh% halafu unabaki ukijiuliza hizo zilizokwenda nitazi-account vipi?. Mwishowe kiwanda kinafungwa, pengine wewe Bakari ndio utasemwa umekula hela. Kumbe wako wenyewe wananona tu. Ndio maana ma-professional walio na nyadhifa mbalimbali wamehamia kwenye siasa. Forget u-proffessor huku huna chakula nyumbani.
    Kwa taarifa yako kuna Proffessor mmoja wa SUA mkewe ni mkuu wa mkoa zzz amegombea
    Udiwani (Ni cheo kilicho chini ya mbunge). Unadhani anatafuta nini? Amechoka anataka kula. Ukitaka kula nenda CCM uwe M-blabla, maneno mengi ya kuwasifu wakubwa very soon utapewa ukuu wa wilaya au mkoa. Angalia wakuu wa mikoa na wilaya siku hizi ni vyeo wa kutupiwa tu. Wengine hawana hata form four.
    Nina uchungu na nchi yangu na wakati ukifika nitasaidia kadiri ninavyoweza, sitataka kutangaza ulimwengu ujue ila moyoni mwangu nitakuwa nimeridhika kuwa nimewasaidia wadogo zangu wanaoshinda barabarani wakiuza WhiteDent. Kweli nahuzunika ninapowaona watoto wanaotakiwa wawe darasani lakini wako barabarani. Sasa hawa wliokalia mawe, afadhali kidogo hata kama inatia aibu ni mwanzo mzuri.

     
  • Tarehe: 2:48:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    tatizo watu tunataka kuanza kujadili kitu ambacho tumeshaamini hakiwezekani kama kuna mtu aligombea kwenye hili jimbo na wananchi wakampa kura nyingi tu hapo kwenye hiyo tarafa basi story zote hizi tunazoweza kuandika ni kupotezeana muda kwani wenyeji wa hapo hawajui kipi cha kupewa kipao mbele sasa sisi watu baki tutafanyaje.miti ipo wananchi wapo viongozi wapo inakuwaje wasubili budget ya selikari ili wawekewe madawati kama ingekuwa swala la walimu sawa ila hilo ni uzembe wao.

     
  • Tarehe: 3:55:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger mloyi

    Naona hata hapa bado tunatupiana lawama, kama alivyosema raisi wa Tanzania 2020-2040, sijui yeye aliyepo Tanzania amefanya nini kuwaliwaza (hiki hakihitaji uwezo mkubwa wa kipesa) watoto hawa angalau waendelee na moyo wa kutafuta elimu ingawa tunapenda kuwasahau na tunataka wawe chini yetu au kwa jina maarufu "House boys/girls" wa kuangalia watoto na wajukuu wetu.
    Sijui labda ni muendelezo wa Hadithi ya Mlimani, masikini waligoma hawana 40% ya kuchangia elimu, sasa wanaambiwa ili waendelee na masomo wawe nayo hiyo 40% mkononi siku watakapo itwa masomoni tena! na hawa wanabidii ya kupata elimu na wamedhamiria kuipata tunawawekea vikwazo kama hivi, hali mbaya darasani. sijui kama tunania ya kuyafikia malengo ya millenia na elimu kwa wote. Labda imekuwa ni elimu kwa wenye uwezo, kuanzia msimgi mpaka chuo kikuu.
    Kingine ninachokiona hapa ni ubinafsi wa wazazi, inasikitisha kuwa mpaka kwa watoto wao wenyewe, wanakosa muda wa kuamua nini wafanye ili kurahississha masomo ya wanowao. Sidhani kama mkoa kama morogoro unaoongoza kwa kutoa mbao wazazi wanashindwa kutemgeneza mabenhi na meza za kienyeji, hata kwa kutumia mabanzi, kwa ajili ya shule yao, inasikitisha zaidi hii na inatia hasira!
    Labda utegemezi sasa umeingia kwenye akili zetu, hazitakuwa "classroom furniture" kama hazikutoka kwa "wahisani" wetu! Mhh, inabidi tutafute muda tuanze na kuzipima akili zetu wenyewe kabla hatujaanza kuongelea matatizo yetu maana akili zetu ndiyo zinaweza kuwa vyanzo vya matatizo yetu.

     
  • Tarehe: 3:55:00 AM, Mtoa Maoni:- Blogger Fikrathabiti

    Jeff,
    Kwanza nikushukuru kwa picha hii murua kabisa na naweza kusema ni BORA ya mwaka.Pili iwe changamoto kwa ndugu yetu MICHUZI anaetamba katika medani ya BLOG ZA PICHA.Ndugu michuzi hii nadhani ndo aina ya picha zinzopaswa kutamalaki katika kibaraza chako tando.

    Ndugu zangu,HAKI ELIMU walikua wanafanya kazi nzuri sana.Haya ni baadhi ya mambo waliyokua wanayaibua katika sekta ya elimu,achilia mbali uozo lukuki uliopo katika sekta hii muhimu kwa maendeleo ya nchi yeyote duniani.Nadhani mnajua kilichowakuta!!!!!walifungiwa!!!!eti kwasababu wanadhihaki maendeleo na juhudi za serikali katika ukuzaji wa sekta hiyo!!!! nadhani ndo maana hata jeff akawa na wasiwasi kua watu wasiandike majin ayao halisi wakati wa kutoa maoni!!!

    Ndugu zangu,hakuna sababu ya kuoneana haya kwa kipindi hiki..LETS FACE IT!!WATAWALA wetu ni aina ya watu wasiopenda kuambiwa ukweli katika mambo yaliyo wazi...hatuna budi kuendeleza mapambano yetu haya na kama ni KUTUNYONGA AU KUTUPOTEZA watajua wenyewe ila ujumbe ufike kwa kutumia nafasi yetu tuliyonayo kama wadau katika sekta ya habari...

    Naamini kua hicho ni kielelezo tu cha mengi mabaya na yanayotia kichefuchefu katka siasa zetu TANZANIA...mimi nadhani ifike mahali watawala wetu waache siasa katika mambo yanayogusa maisha ya watu moja kwa moja....

    Ndugu zangu,hivi majuzi tulikua na mjadala kuhusu viwango vya wanafunzi kufaulu wanaopaswa kujiunga na elimu ya juu...WATAWALA wet wakasema ni daraja la kwanza kwa wanaume na daraja la kwanza na la pili kwa wanawake...sasa jamani mazingira kama haya yanawahakikishia hao wanafunzi ambao ndo asilimia kubwa kufikia viwango hivyo!!!????? msingi ukiwa mbovu ni wazi kua huko juu nako kutakua ovyo.....

    Hivi ni kwanini serikali yetu ikose vipaumbele?????Elimu na mpira kipi bora???Mimi nadhani ni elimu kwanza na mengine baadae..Tukiwa na wasomi wazuri walioandaliwa katika mazingira mazuri ni wazi kua ushiriki wao katika masuala mbalimbali ya maendeleo utakua mzuri....Ubinafsi unaonyeshwa na viongozi wetu unatia hasira sana.

    Kuna haja ya kubadilika ndugu zangu....Hao vijana hapo juu ni wazi kua maisha yao yakiwa mabaya siku za usoni mtu wa kumlaumu ni serikali yake na si mwingine... Kubadili mazingira kama hayo si kazi kubwa ila inahitaji dhamira ya dhati katika kutekeleza...

    Picha hii inazua mjadala mpana sana ndugu zangu...nini kazi ya wabunge katika kutumikia wapiga kura wao???kazi yao imekua kukaa bungeni na kulilia gari zao ziwekwe bendera ya taifa na kupigiwa saluti huku wakiitwa WAHESHIMIWA!!!what the hell is this!!!!!!

    Naomba kuishia hapa kwa leo.....
    http://fikrathabiti.blogspot.com

     
  • Tarehe: 9:53:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Bwana Jeff!! Sijui cha kusema ila umetugusa sana!!
    Ninachoweza kusema ni kwamba hawa watoto hawa watoto ni waathirika wa mipango mibaya ambayo Mbunge kwa kushirikiana na wananchi anao uwezo kuwahamasisha wananchi wanajityolea na serikali ikamalizia kwani Mkoa wa Kilimanjaro umejengaje shule zao, nyingi ni kwa anjia ya michango ya wananchi!!! Nailaumu serikali lakini nakumbuka Hotuba moja ya Nyerere ya Mwaka 68 alikwenda kutembelea Sumbawanga wananchi wakamsomea hotuba yao wakaiomba Serikali isaidie kujenga Daraja la mto ambali lina urefu wa Mita nane!!! Nyerere aliposimama kuijibu ile hotuba alisema Jamani "...nilitegemea hata nikute mmesombamchnga ili nijue mnalitaka daraja kwani nyie Kondooo mfanyiwe kila kitu jamani?...." akatoa mifano kibao,,, ninachosema ni kwamba ni kazi ya Mbunge kuwahamasisha wananchi wake kwa kushirikiana na Serikali kila kitu kinawezekana!!
    Wabillah Tawfiq

     
  • Tarehe: 9:59:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    ndesanjo said...

    Picha kama hizi tunazihitaji sana maana ni kielelezo cha ukweli unaofichwa na majengo marefu ya kisasa Dasalama na magari ya kifahari. Hawa ndio watanzania wenzetu waliosahaulika. Watanzania tunaopenda kuwasahau.
    Kaka Ndesanjo hatusahau tunasahaulishwa na Picha tamu za Michuzi za akina Nakaaya Jd na ma Limo ya Bongo, Kaka hii inaitwa Editorial Pic kaka Picha inayosema kaka, picha hii ukimpa mtu najua hata Jeff angeichambua anaweza kutoka na makala hata ya page 40!!!
    Wabillah Tawfiq

     
  • Tarehe: 2:04:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    KWANZA KABISA NI ASANTE KWA HII PICHA,INAONYESHA UKWELI WA AINA FULANI, JINSI MIMI NINAVYOONA NI KUWA TUPO KWENYE VITA YA AINA FULANI HIVI,NCHI YENYE USALAMA,WANAFUNZI HAWAWEZI KUWA KWENYE HALI HII. SASA TUJIULIZE JE TUPO KWENYE VITA GANI?

     
  • Tarehe: 3:17:00 PM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Nina ona nini katika picha? Swali zuri. Jibu: Hali halisi ya Watanzania wengi walalahoi. Wapi MKUKUTA,MKURABITA, wapi...sikumbuki tena maneno mengine ya kisiasa yatumiwayo na serikali yetu kuombea fedha kwa wafadhili...!

     
  • Tarehe: 3:34:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    "...Mambo ya Bongo sasa hivi kiboko; kuna mashopingi moli kama ya mtoni, maubungo plaza, meifea plaza na maplaza mengine mengi tuuu! Maapatimenti, mariili esteti broka, mabangaloo, mafaivu staa hoteli, na maskai skrepa! halafu mabarabara ya kimtoni na madaraja kama lile la Kibiti, watasha wenyewe wanabloo! Na neshino stediumu mpya ikiisha litakuwa hamna tena Afrika nzima!

    Mademu siku hizi wanang'aaaa! Kuna maMiss kata, miss tarafa, miss wilaya, miss mkoa, miss Tanzania, mpaka miss yunivasi! Mafasheni shoo, madizaina, na mamodozi! Siku hizi mademu wanakutilia mavitu ya madizaina: jojo amani, guchi, siyo mitenge ya Sunguratex sijui Urafiki. Jamani Bongo tumetoka mbali, niliwahi kuchukua bonge la demu kufika homu chupi haivuki, mpira wa chupi umekatika akafunga fundo ilibidi alifungue kwa meno! Siku hizi maselebriti kibao: wa vipaji vya kitaaluma, kisanii, kimichezo, kisiasa, ua kwa majina ya ukoo. Kuna Matamasha, mabonanza, na makonseti hatari tupu!

    Redio stesheni za kumwaga siyo kama wakati ule idhaa tatu tu; taifa, biashara na eksteno sevisi iliyokuwa inafunguliwa kwa masaa maalumu na kipindi kimoja tu cha salamu siku za Jumapili mchana! Na tivii chaneli kibao siyo kama enzi zile tivii Zanzibar minara michache mitaa ya Upanga na Ostabei tena usalama wa taifa wasiione, ukionekana mnara utakuwa umeenda kinyume na Azimio la Arusha kwa kuwa bepari au kabaila kwa sababu ya kumiliki tivii! Siku nyungo kila nyumba. Mpaka vijijini wana nyungo. Nilikuwa Ng'apa, Lindi huko nikafikiri nitaikosa mechi ya Aseno na Livapuli, mshikaji baa zote zilikuwa zinaonyesha gemu, mashabiki wa ligi ya premia kapu na yuefa wapo mpaka Umachingani huko! Eee bwana na magari mengine yaliyopo Bongo hata ughaibuni hamna: sijui mabaluni, maviieksi, mashangingi, mamuso, mahama, mafoo whili draivu, maleksuzi, yaani wee acha tu!

    Elimu nayo sasa imepanda kuna mainteneshino skuli kuanzia nasari mpaka hai skuli. Siku hizi mtoto mdogo anaongea kingreza kama mzungu! Yunivesti siyo UDSM na SUA tu kuna mayunivesti kibao sijui Nyegezi, Sijui Mikocheni, Makumira, Tumaini, na jingine la nguvu linaangushwa Dodoma unaambiwa hilo yunivesti sijui litakuwa linachukuwa wanafunzi ngapi sijui kwa wakati mmoja! Yaani hilo yunivesti litakuwa kama Kembriji, Oksfodi, au Havadi! Eee bwana eee!

    Siku hizi simu siyo big dili! Unaambiwa nilikuwa Nanjumbu, Mtwara vijijini ndani ndani huko nikakikuta kibibi kizeeee utafikiri hakikuwahi kuwa kitoto kichanga! Unajua nini? Kilikuwa na kimobiteli cha Nokia hizi ndogo ndogo kinaongea sijui na nani? Mwenyewe nilizimia! Enzi za POSTA NA SIMU ilikuwa lazima uende kibanda cha simu tena ukikikuta simu nzima una bahati vinginevyo sumni yako inaliwa na simu haifanyi kazi. Ua ukitumia simu za nyumbani siyo laini kuingiliana! Au unaweza kujikuta unasikiliza simu tano kwa wakati mmoja! Siku hizi hela yako tu: kuna bazi, seliteli, voda, mobiteli lakini mimi naiona seliteli ndiyo kiboko lakini voda nao moto! Jamaa wa posta kweli walikuwa wanatuzingua barua unaituma Kibaha toka Dar inachukuwa mwezi! Siku hizi unatuma teksi meseji au ukiona namna gani vipi unaenda intaneti unatuma imeli!

    Mabenki ya kumwaga hakuna mpango wa kupangapanga foleni tangu asubuhi mpaka jioni. Mahospitali hela yako tu. Kuna mahospitali yana vifaa kupita Muhimbili. Unapigwa eksrei huku unajicheki kwenye skrini, unafanyiwa opresheni bila kupasuliwa, maamblensi mengine mabenzi yana huduma mpaka za kuzalishia!

    Usafiri siku hizi siyo sijui ATC, UDA, sijui KAMATA, nyooo! Siku hizi mtu unataka kwenda Mwanza unapaki begi lako unaenda eyapoti unachagua pipa gani udandie Prisisheni, Igo, eyaTanzania au bomba lolote tu! Mabasi siku hizi kuna malakshari yana maeyahostesi kama wa kwenye ndege! Mabasi yana vyoo, tivii, slipingi kochi yaani kama mtoni tu! Prezidenti naye ana pipa lake mwenyewe nasikia lina bafu na jim humo humo!

    Bia na fegi za kumwaga. Siku hizi hakuna ulanguzi wa bia wala fegi. Bia unakunywa unayoipenda mwenyewe. Miye bia ninayoipenda kesto (Castle). Bia na Fegi zinakosa maketi mpaka zinafanyiwa advataizment kila mahali. Mzee mzima alitaka kuleta mpango wa kufunga mabaa mapema, kipato cha taifa kikashuka wakamwambia asitishe zoezi lake. Taratibu wakamng'oa asilitie taifa hasara bure!

    Unafiki wa kuitana NDUGU imepigwa ribiti! Mzee mzima alipoingia madarakani akaona huu unafikitu. Wewe tangu lini Mchaga na Mpogolo wakawa ndugu? Au mbunge na mesenja au waziri na nesi udugu uko wapi? Lazima tukubali watu wengine ni WAHESHIMIWA na wengine watu tu!

    Mimi ughaibuni wala sikuzimii. Jamaa wanaenda ughaibuni nasikia wakifika huko wanabeba maboksi na kukosha vizee. Nanihii alikuwa na bonge la posti akajifanya kwenda ughaibuni kufanya mastazi. Kabla hajaondondoka alikuwa kavimba: mimba hiyoo, mashavu utafikiri anapuliza moto! Hiyo mastazi imemtokea puani: karudi mimba imekatika, kakondaa utafikiri Msudani ya Kusini, miguu kama mikono ya mawani, yaani utamuonea huruma! Unajua Bongo michoro yako tu! Misheni kibao inategemeana na wewe mwenyewe jinsi unavyopanga kete zako. Hapa hapa bongo kuna watu wanakwenda huko ughaibuni kila siku utafikiri andazi na kikombe cha chai! Hapa hapa Bongo kuna majamaa wanaishi kama mtoni: asubuhi wanapata brekifasti ya masoseji, hambagi, juisi na chai ya maziwa matupu au uji uliopikwa na unga wa keki ukatiwa na mapande ya siagi na krimu! Lanchi chikeni chipsi na kuku, dina steki hevi na grili pateto au raisi! Yaani wee acha tu, Bongo New York.

    Na manjagu wanakula mavitu hevi siyo kama enzi za Mahita tangu kaja Said Mwema manjagu wanatia vitu vya kimtoni 'maksi' sijui mabelti, mapikipiki, yaani we acha tu! Bongo niu yoki. Cheki mwenyewe hapo chini!


    Ofisa na askari wa Jeshi la Polisi wakisimamia bomoabomoa ya vibanda vya wafanyabiashara iliyofanyika jana katika eneo linalozunguka jengo la DDC Kariakoo katika barabara ya Kongo, Dar es Salaam. (Picha na Richard Mwaikenda).

     
  • Tarehe: 5:58:00 AM, Mtoa Maoni:- Anonymous Anonymous

    Je kati ya maadui wale watatu walioainishwa na Mwalimu Nyerere ni yupi tumemshinda? Kama elimu ndio kukaa chini ama kukalia maofali(kama ilivyo pichani), walimu wa UPE (sekondari, UKIMWI kila kona, kipindupindu kisichoisha Dar na kwingine, na umaskini wa kutupwa, je kazi ya "Watwawala" ni ipi? Chama kitaendelea kudumu tu pamoja na maadui hao hivyo hivyo.

     
   
 
Copyright 2006 © JEFF MSANGI. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu Idadi ya watu Idadi ya watu
eXTReMe Tracker